< 1 Thessalonians 5 >

1 But concerning the times and the seasons, brethren, ye have no need that ye should be written to,
Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2 for ye know perfectly well yourselves, that the day of [the] Lord so comes as a thief by night.
Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3 When they may say, Peace and safety, then sudden destruction comes upon them, as travail upon her that is with child; and they shall in no wise escape.
Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4 But ye, brethren, are not in darkness, that the day should overtake you as a thief:
Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5 for all ye are sons of light and sons of day; we are not of night nor of darkness.
Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6 So then do not let us sleep as the rest do, but let us watch and be sober;
Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7 for they that sleep sleep by night, and they that drink drink by night;
Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8 but we being of [the] day, let us be sober, putting on [the] breastplate of faith and love, and as helmet [the] hope of salvation;
Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9 because God has not set us for wrath, but for obtaining salvation through our Lord Jesus Christ,
Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10 who has died for us, that whether we may be watching or sleep, we may live together with him.
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11 Wherefore encourage one another, and build up each one the other, even as also ye do.
Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12 But we beg you, brethren, to know those who labour among you, and take the lead among you in [the] Lord, and admonish you,
Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13 and to regard them exceedingly in love on account of their work. Be in peace among yourselves.
Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14 But we exhort you, brethren, admonish the disorderly, comfort the faint-hearted, sustain the weak, be patient towards all.
Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15 See that no one render to any evil for evil, but pursue always what is good towards one another and towards all;
Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16 rejoice always;
Furahini daima,
17 pray unceasingly;
salini kila wakati
18 in everything give thanks, for this is [the] will of God in Christ Jesus towards you;
na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19 quench not the Spirit;
Msimpinge Roho Mtakatifu;
20 do not lightly esteem prophecies;
msidharau unabii.
21 but prove all things, hold fast the right;
Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22 hold aloof from every form of wickedness.
na epukeni kila aina ya uovu.
23 Now the God of peace himself sanctify you wholly: and your whole spirit, and soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 He [is] faithful who calls you, who will also perform [it].
Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25 Brethren, pray for us.
Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26 Greet all the brethren with a holy kiss.
Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27 I adjure you by the Lord that the letter be read to all the [holy] brethren.
Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28 The grace of our Lord Jesus Christ [be] with you.
Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< 1 Thessalonians 5 >