< 1 Thessalonians 5 >

1 But concerning the times and the seasons, brethren, ye have no need that ye should be written to,
Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
2 for ye know perfectly well yourselves, that the day of [the] Lord so comes as a thief by night.
kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
3 When they may say, Peace and safety, then sudden destruction comes upon them, as travail upon her that is with child; and they shall in no wise escape.
Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
4 But ye, brethren, are not in darkness, that the day should overtake you as a thief:
Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
5 for all ye are sons of light and sons of day; we are not of night nor of darkness.
Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
6 So then do not let us sleep as the rest do, but let us watch and be sober;
Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
7 for they that sleep sleep by night, and they that drink drink by night;
Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
8 but we being of [the] day, let us be sober, putting on [the] breastplate of faith and love, and as helmet [the] hope of salvation;
Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
9 because God has not set us for wrath, but for obtaining salvation through our Lord Jesus Christ,
Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
10 who has died for us, that whether we may be watching or sleep, we may live together with him.
Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
11 Wherefore encourage one another, and build up each one the other, even as also ye do.
Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
12 But we beg you, brethren, to know those who labour among you, and take the lead among you in [the] Lord, and admonish you,
Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
13 and to regard them exceedingly in love on account of their work. Be in peace among yourselves.
Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
14 But we exhort you, brethren, admonish the disorderly, comfort the faint-hearted, sustain the weak, be patient towards all.
Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
15 See that no one render to any evil for evil, but pursue always what is good towards one another and towards all;
Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
16 rejoice always;
Furahini siku zote;
17 pray unceasingly;
ombeni bila kukoma;
18 in everything give thanks, for this is [the] will of God in Christ Jesus towards you;
shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
19 quench not the Spirit;
Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
20 do not lightly esteem prophecies;
msiyadharau maneno ya unabii.
21 but prove all things, hold fast the right;
Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
22 hold aloof from every form of wickedness.
Jiepusheni na uovu wa kila namna.
23 Now the God of peace himself sanctify you wholly: and your whole spirit, and soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
24 He [is] faithful who calls you, who will also perform [it].
Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
25 Brethren, pray for us.
Ndugu, tuombeeni.
26 Greet all the brethren with a holy kiss.
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
27 I adjure you by the Lord that the letter be read to all the [holy] brethren.
Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
28 The grace of our Lord Jesus Christ [be] with you.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.

< 1 Thessalonians 5 >