< 1 Samuel 15 >

1 And Samuel said to Saul, Jehovah sent me to anoint thee king over his people, over Israel: now therefore hearken to the voice of the words of Jehovah.
Samweli akamwambia Sauli, “BWANA alinituma nikutie mafuta uwe mfalme wa watu wake Israeli. Basi sikiliza maneno ya BWANA.
2 Thus saith Jehovah of hosts: I have considered what Amalek did to Israel, how he set himself against him in the way, when he came up from Egypt.
Hivi ndivyo BWANA wa majeshi asemavyo, 'Nilichunguza jinsi Amaleki alivyomfanyia Israeli kwa kuwapinga njiani, walipopanda kutoka Misri.
3 Now go and smite Amalek, and destroy utterly all that they have, and spare them not, but slay both man and woman, infant and suckling, ox and sheep, camel and ass.
Sasa nenda umshambulie Amaleki na ukaangamize kabisa vitu vyote walivyo navyo. Usiwaache, ua wote mwanamme na mwanamke, mtoto na mtoto mchanga, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda.”'
4 And Saul summoned the people, and numbered them in Telaim, two hundred thousand footmen, and ten thousand men of Judah.
Sauli akwaita watu na kuwahesabu katika mji wa Talemu: watu mia mbili elfu waendao kwa miguu, na watu elfu kumi kutoka Yuda.
5 And Saul came to the city of the Amalekites, and set an ambush in the valley.
Kisha Sauli akaja hadi mji wa Amaleki akangoja huko bondeni.
6 And Saul said to the Kenites, Go, depart, and go down from among the Amalekites, lest I destroy you with them; for ye shewed kindness to all the children of Israel when they came up out of Egypt. And the Kenites departed from among the Amalekites.
Ndipo Sauli akawaambia Wakeni, “Nendeni, muondoke, mkajitenge na Waamaleki, nisije kuwaangamiza pamoja nao. Kwa maana ulionesha wema kwa watu wote wa Israeli, walipotoka Misri.” Kwa hiyo Wakeni wakajitenga na Waamaleki.
7 And Saul smote Amalek from Havilah as thou comest to Shur, which is opposite to Egypt.
Kisha sauli akawashambulia Waamaleki, kutoka Havila hadi kufika Shuri, ulio mashariki mwa Misri.
8 And he took Agag the king of Amalek alive, and utterly destroyed all the people with the edge of the sword.
Basi akamchukua Agagi mfalme wa Waamaleki akiwa hai; aliwaangamiza kabisa watu wote kwa ncha ya upanga.
9 And Saul and the people spared Agag, and the best of the sheep and oxen, and beasts of the second bearing, and the lambs, and all that was good, and would not devote them to destruction; but everything that was mean and weak, that they destroyed utterly.
Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi akiwa hai, pamoja na kondoo wazuri, ng'ombe, ndama wanono, na wanakondoo. Kila kitu kilichokuwa kizuri, hawakukiangamiza. Bali waliangamiza kabisa chochote kilichodharaulika na kisicho na thamani.
10 And the word of Jehovah came to Samuel, saying,
Baadaye neno la BWANA likamjia Samweli, kusema,
11 It repenteth me that I have set up Saul to be king; for he is turned away from following me, and hath not fulfilled my words. And Samuel was much grieved; and he cried to Jehovah all night.
“Inanihuzunisha kwamba nimemchagua Samweli awe mfalme, kwa maana aligeuka nyuma asinifuate na hakutekeleza maagizo yangu.” Samweli alikasirika; akamlilia BWANA usiku kucha.
12 And Samuel rose early to meet Saul in the morning. And it was told Samuel, saying, Saul came to Carmel, and behold, he set him up a monument, and has turned about, and passed on, and gone down to Gilgal.
Samweli aliamka mapema akutane na Sauli wakati wa asubuhi. Samweli aliambiwa, “Sauli alifika Karmeli na amejijengea ukumbusho kwa ajili yake, kisha aligeuka na kuendelea chini hadi Gilgali.” Ndipo
13 And Samuel came to Saul; and Saul said to him, Blessed art thou of Jehovah: I have fulfilled the word of Jehovah.
Samweli akamwendea Sauli, na Sauli akamwambia, “Umebarikiwa na BWANA! Nami nimetekeleza amri ya BWANA.”
14 And Samuel said, What [means] then this bleating of sheep in mine ears, and the lowing of oxen which I hear?
Samweli akasema, “Hicho kilio cha kondoo ni cha nini basi masikioni mwangu, na hiyo milio ya ng'ombe ninayosikia?
15 And Saul said, They have brought them from the Amalekites, because the people spared the best of the sheep and of the oxen, to sacrifice to Jehovah thy God; and the rest we have utterly destroyed.
Sauli akamjibu, “Wao wamewaleta kutoka kwa Waamaleki. Kwa sababu watu waliwaacha hai kondoo wazuri na ng'ombe, kwa ajili ya sadaka kwa BWANA Mungu wako. Zilizobaki tuliziangamiza kabisa.”
16 And Samuel said to Saul, Stay, that I may tell thee what Jehovah has said to me this night. And he said to him, Say on.
Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Subiri nitakumbia kile ambacho BWANA amekisema kwangu usiku.” Sauli akamwambia, “Sema!”
17 And Samuel said, Was it not when thou wast little in thine eyes that thou [becamest] the head of the tribes of Israel, and Jehovah anointed thee king over Israel?
Samweli akasema, “Ingawa wewe ni mdogo machoni pako mwenyewe, je, hukufanywa mkuu wa kabila za Israeli? Na BWANA akakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli;
18 And Jehovah sent thee on a way and said, Go and utterly destroy the sinners the Amalekites, and fight against them until they be consumed.
BWANA alikutuma katika safari yako akisema, 'nenda na uangamize kabisa wenye dhambi, Waamaleki, na upigane dhidi yao hadi wameangamizwa.'
19 Why then didst thou not hearken to the voice of Jehovah, but didst fall upon the spoil, and didst evil in the sight of Jehovah?
Kwa nini basi haukuitii sauti ya BWANA, bali badala yake ulishikilia nyara na ukafanya uovu machoni pa BWANA?”
20 And Saul said to Samuel, I have indeed hearkened to the voice of Jehovah, and have gone the way which Jehovah sent me, and have brought Agag the king of Amalek, and have utterly destroyed the Amalekites.
Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Kweli kabisa niliitii sauti ya BWANA, Na nimeifuata njia ambayo BWANA alinituma. Nimemteka Agagi, mfalme wa Waamaleki, na kuwaangamiza kabisa Waamaleki.
21 But the people took of the spoil, sheep and oxen, the choicest of the devoted things, to sacrifice to Jehovah thy God in Gilgal.
Lakini watu walichukua baadhi ya nyara-kondoo na ng'ombe, na vitu vizuri vilivyokusudiwa kuangamizwa, ili wavitoe dhabihu kwa BWANA, Mungu wako, huko Gilgali.”
22 And Samuel said, Has Jehovah delight in burnt-offerings and sacrifices, As in hearkening to the voice of Jehovah? Behold, obedience is better than sacrifice, Attention than the fat of rams.
Samweli akajibu, “Je, BWANA hufurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama ilivyo kuitii sauti yake? Utii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia ni bora kuliko mafuta ya beberu.
23 For rebellion is [as] the sin of divination, And selfwill is [as] iniquity and idolatry. Because thou hast rejected the word of Jehovah, He hath also rejected thee from being king.
Kwa maana uasi ni sawa na dhambi ya uchawi, na ukaidi ni sawa na uovu na udhalimu. Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, naye pia amekukataa usiwe mfalme.”
24 And Saul said to Samuel, I have sinned, for I have transgressed the commandment of Jehovah, and thy words; for I feared the people, and hearkened to their voice.
Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi; kwa maana nimevunja amri ya BWANA na maneno yako, kwa sababu niliwaogopa watu na kuitii sauti yao.
25 And now, I pray thee, forgive my sin, and turn again with me, that I may worship Jehovah.
Sasa, tafadhali nisamehe dhambi yangu, na urudi nami ili nipate kumcha BWANA.”
26 And Samuel said to Saul, I will not turn again with thee; for thou hast rejected the word of Jehovah, and Jehovah has rejected thee from being king over Israel.
Samweli akamwambia Sauli, “Sitarudi pamoja na wewe; kwa sababu umekataa neno la BWANA, naye BWANA amekukataa usiwe mfalme juu ya Israeli.”
27 And as Samuel turned to go away, [Saul] laid hold upon the skirt of his mantle, and it rent.
Samweli alipogeuka kuondoka, Sauli akashika pindo la kanzu yake, na likachanika.
28 Then Samuel said to him, Jehovah has rent the kingdom of Israel from thee to-day, and has given it to thy neighbour, who is better than thou.
Samweli akamwambia, “BWANA ameuchana ufalme wa Israeli kutoka kwako leo na amempa ufalme huo jirani yako, aliye bora kuliko wewe.
29 And also the Hope of Israel will not lie nor repent; for he is not a man, that he should repent.
Pia, yeye ni Uwezo wa Israeli hatasema uongo wala kubadili nia yake; kwa sababu si mwanadamu, kwamba abadili nia yake.”
30 And he said, I have sinned; honour me now, I pray thee, before the elders of my people, and before Israel, and turn again with me, that I may worship Jehovah thy God.
Kisha Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali nipe heshima wakati huu mbele ya wakuu wa watu wangu na mbele ya Israeli. Urudi tena pamoja nami, kusudi niweze kumcha BWANA, Mungu wako.”
31 So Samuel turned again after Saul; and Saul worshipped Jehovah.
Hivyo Samweli akamrudia tena Sauli, na Sauli akamcha BWANA.
32 And Samuel said, Bring ye near to me Agag the king of Amalek. And Agag came to him gaily. And Agag said, Surely the bitterness of death is past.
Kisha Samweli akasema, “Mmlete hapa kwangu Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akafika kwake akiwa amefungwa minyororo na kusema, “Hakika uchungu wa kifo umepita.”
33 And Samuel said, As thy sword has made women childless, so shall thy mother be childless above women. And Samuel hewed Agag in pieces before Jehovah in Gilgal.
Naye Samweli akamjibu, “Jinsi upanga wako ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto miongoni mwa wanawake.” Kisha Samweli akamkata Agagi vipande vipande mbele za BWANA huko Gilgali.
34 And Samuel went to Ramah; and Saul went up to his house to Gibeah of Saul.
Samweli akaenda Rama, na Sauli akapanda kwenda nyumbani kwake Gibea ya Sauli.
35 And Samuel saw Saul no more until the day of his death; for Samuel mourned over Saul; and Jehovah repented that he had made Saul king over Israel.
Samweli hakumuona tena Sauli hadi siku ya kifo chake, lakini alimwombolezea Sauli. Na BWANA alijuta kwa kumfanya Sauli awe mfalme juu ya Israeli.

< 1 Samuel 15 >