< 1 Kings 16 >

1 And the word of Jehovah came to Jehu the son of Hanani against Baasha, saying,
Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema:
2 Forasmuch as I exalted thee out of the dust, and made thee prince over my people Israel, and thou hast walked in the way of Jeroboam, and hast made my people Israel to sin, provoking me to anger with their sins;
“Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.
3 behold, I will take away Baasha and his house, and will make thy house like the house of Jeroboam the son of Nebat.
Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati.
4 Him that dieth of Baasha in the city shall the dogs eat, and him that dieth of his in the field shall the fowl of the heavens eat.
Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”
5 And the rest of the acts of Baasha, and what he did, and his might, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
6 And Baasha slept with his fathers, and was buried in Tirzah; and Elah his son reigned in his stead.
Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 And also through the prophet Jehu the son of Hanani the word of Jehovah came against Baasha, and against his house, even for all the evil that he did in the sight of Jehovah, provoking him to anger with the work of his hands, in being like the house of Jeroboam; and because he had smitten him.
Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.
8 In the twenty-sixth year of Asa king of Judah, Elah the son of Baasha began to reign over Israel in Tirzah for two years.
Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.
9 And his servant Zimri, captain of half [his] chariots, conspired against him; and he was in Tirzah, drinking himself drunk in the house of Arza, who was the steward of his house in Tirzah;
Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa.
10 and Zimri went in and smote him, and killed him, in the twenty-seventh year of Asa king of Judah, and he reigned in his stead.
Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.
11 And it came to pass when he began to reign, as soon as he sat on his throne, he slew all the house of Baasha: he left him not a male, neither of his kinsmen nor of his friends.
Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki.
12 And Zimri destroyed all the house of Baasha, according to the word of Jehovah, which he spoke against Baasha through Jehu the prophet,
Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu:
13 for all the sins of Baasha, and the sins of Elah his son, which they sinned and wherewith they made Israel to sin, provoking Jehovah the God of Israel to anger with their vanities.
kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
14 And the rest of the acts of Elah, and all that he did, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
15 In the twenty-seventh year of Asa king of Judah, Zimri reigned seven days in Tirzah. Now the people were encamped against Gibbethon, which [belonged] to the Philistines.
Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti.
16 And the people that were encamped heard say, Zimri has conspired, and has also smitten the king; and all Israel made Omri, the captain of the host, king over Israel that day in the camp.
Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini.
17 And Omri went up from Gibbethon, and all Israel with him, and they besieged Tirzah.
Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa.
18 And it came to pass when Zimri saw that the city was taken, that he went into the citadel of the king's house, and burned the king's house over him with fire;
Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa,
19 and he died for his sins which he sinned in doing evil in the sight of Jehovah, in walking in the way of Jeroboam, and in his sin which he did, making Israel to sin.
kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.
20 And the rest of the acts of Zimri, and his conspiracy which he wrought, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
21 Then were the people of Israel divided into two parts: half of the people followed Tibni the son of Ginath, to make him king; and half followed Omri.
Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri.
22 But the people that followed Omri overcame the people that followed Tibni the son of Ginath; and Tibni died, and Omri reigned.
Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.
23 In the thirty-first year of Asa king of Judah, Omri began to reign over Israel, — twelve years; he reigned six years in Tirzah.
Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa.
24 And he bought the hill Samaria of Shemer for two talents of silver; and built on the hill, and called the name of the city that he built, after the name of Shemer, owner of the hill, Samaria.
Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.
25 And Omri wrought evil in the sight of Jehovah, and did worse than all that were before him.
Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia.
26 And he walked in all the way of Jeroboam the son of Nebat, and in his sins wherewith he made Israel to sin, provoking Jehovah the God of Israel to anger with their vanities.
Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
27 And the rest of the acts of Omri, what he did, and his might which he shewed, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
28 And Omri slept with his fathers, and was buried in Samaria; and Ahab his son reigned in his stead.
Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.
29 And Ahab the son of Omri began to reign over Israel in the thirty-eighth year of Asa king of Judah; and Ahab the son of Omri reigned over Israel in Samaria twenty-two years.
Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili.
30 And Ahab the son of Omri wrought evil in the sight of Jehovah more than all that were before him.
Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia.
31 And it came to pass, as if it was a light thing for him to walk in the sins of Jeroboam the son of Nebat, that he took as wife Jezebel the daughter of Ethbaal king of the Zidonians; and he went and served Baal and worshipped him.
Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu.
32 And he reared up an altar for Baal in the house of Baal, which he built in Samaria.
Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria.
33 And Ahab made the Asherah; and Ahab did more to provoke Jehovah the God of Israel to anger than all the kings of Israel that were before him.
Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
34 In his days Hiel the Bethelite built Jericho; he laid its foundation in Abiram his firstborn, and set up its gates in Segub his youngest, according to the word of Jehovah which he spoke through Joshua the son of Nun.
Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.

< 1 Kings 16 >