< 1 Corinthians 1 >

1 Paul, [a] called apostle of Jesus Christ, by God's will, and Sosthenes the brother,
Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
2 to the assembly of God which is in Corinth, to [those] sanctified in Christ Jesus, called saints, with all that in every place call on the name of our Lord Jesus Christ, both theirs and ours:
Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
3 Grace to you and peace from God our Father, and [the] Lord Jesus Christ.
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
4 I thank my God always about you, in respect of the grace of God given to you in Christ Jesus;
Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
5 that in everything ye have been enriched in him, in all word [of doctrine], and all knowledge,
Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
6 (according as the testimony of the Christ has been confirmed in you, )
kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
7 so that ye come short in no gift, awaiting the revelation of our Lord Jesus Christ;
Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
8 who shall also confirm you to [the] end, unimpeachable in the day of our Lord Jesus Christ.
Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 God [is] faithful, by whom ye have been called into [the] fellowship of his Son Jesus Christ our Lord.
Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
10 Now I exhort you, brethren, by the name of our Lord Jesus Christ, that ye all say the same thing, and that there be not among you divisions; but that ye be perfectly united in the same mind and in the same opinion.
Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
11 For it has been shewn to me concerning you, my brethren, by those of [the house of] Chloe, that there are strifes among you.
Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
12 But I speak of this, that each of you says, I am of Paul, and I of Apollos, and I of Cephas, and I of Christ.
Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
13 Is the Christ divided? has Paul been crucified for you? or have ye been baptised unto the name of Paul?
Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 I thank God that I have baptised none of you, unless Crispus and Gaius,
Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
15 that no one may say that I have baptised unto my own name.
Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
16 Yes, I baptised also the house of Stephanas; for the rest I know not if I have baptised any other.
(Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17 For Christ has not sent me to baptise, but to preach glad tidings; not in wisdom of word, that the cross of the Christ may not be made vain.
Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
18 For the word of the cross is to them that perish foolishness, but to us that are saved it is God's power.
Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
19 For it is written, I will destroy the wisdom of the wise, and set aside the understanding of the understanding ones.
Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
20 Where [is the] wise? where scribe? where disputer of this world? has not God made foolish the wisdom of the world? (aiōn g165)
Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn g165)
21 For since, in the wisdom of God, the world by wisdom has not known God, God has been pleased by the foolishness of the preaching to save those that believe.
Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
22 Since Jews indeed ask for signs, and Greeks seek wisdom;
Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
23 but we preach Christ crucified, to Jews an offence, and to nations foolishness;
Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
24 but to those that [are] called, both Jews and Greeks, Christ God's power and God's wisdom.
Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
25 Because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men.
Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
26 For consider your calling, brethren, that [there are] not many wise according to flesh, not many powerful, not many high-born.
Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
27 But God has chosen the foolish things of the world, that he may put to shame the wise; and God has chosen the weak things of the world, that he may put to shame the strong things;
Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
28 and the ignoble things of the world, and the despised, has God chosen, [and] things that are not, that he may annul the things that are;
Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
29 so that no flesh should boast before God.
ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
30 But of him are ye in Christ Jesus, who has been made to us wisdom from God, and righteousness, and holiness, and redemption;
Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
31 that according as it is written, He that boasts, let him boast in [the] Lord.
Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”

< 1 Corinthians 1 >