< Zechariah 5 >

1 And I turned and lifted up my eyes. And I saw, and behold, a book flying.
Nikatazama tena: na hapo mbele yangu kulikuwa na kitabu kilichoruka!
2 And he said to me, “What do you see?” And I said, “I see a book flying. Its length is twenty cubits, and its width is ten cubits.”
Akaniuliza, “Unaona nini?” Nikamjibu, “Naona kitabu kinachoruka chenye, urefu wa dhiraa ishirini na upana wa dhiraa kumi.”
3 And he said to me, “This is the curse that goes forth over the face of the whole earth. For every thief will be judged, just as it has been written there, and everyone who swears by this, will be judged in like manner.”
Akaniambia, “Hii ni laana inayotoka kwenda juu ya nchi yote, kwa kuwa kufuatana na yale yaliyoandikwa katika upande mmoja, kila mwizi atafukuziwa mbali, pia kufuatana na yaliyo upande wa pili, kila aapaye kwa uongo atafukuziwa mbali.
4 I will bring it forth, says the Lord of hosts, and it will approach to the house of the thief, and to the house of him who swears falsely by my name, and it will remain in the midst of his house and will consume it, with its wood and its stones.
Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, ‘Nitaituma hiyo laana, nayo itaingia katika nyumba ya mwizi na nyumba ya huyo aapaye kwa uongo kwa Jina langu. Itabaki katika nyumba yake na kuiharibu, pamoja na mbao zake na mawe yake.’”
5 And the angel had departed, who was speaking with me. And he said to me, “Lift up your eyes, and see what this is, that goes forth.”
Kisha yule malaika aliyekuwa akizungumza nami akanijia na kuniambia, “Tazama juu uone ni nini kile kinachojitokeza.”
6 And I said, “What, then, is it?” And he said, “This is a container going forth.” And he said, “This is their eye in all the earth.”
Nikamuuliza, “Ni kitu gani?” Akanijibu, “Ni kikapu cha kupimia.” Kisha akaongeza kusema, “Huu ni uovu wa watu katika nchi nzima.”
7 And behold, a talent of lead was being carried; and behold, one woman sitting in the middle of the container.
Kisha kifuniko kilichotengenezwa kwa madini ya risasi kilichokuwa kimefunika kile kikapu, kiliinuliwa na ndani ya kile kikapu alikuwako mwanamke ameketi!
8 And he said, “This is impiety.” And he cast her into the middle of the container, and he sent the weight of lead into its mouth.
Akasema, “Huu ni uovu,” tena akamsukumia ndani ya kikapu na kushindilia kifuniko juu ya mdomo wa kikapu.
9 And I lifted up my eyes and I saw. And behold, two women were departing, and a spirit was in their wings, and they had wings like the wings of a kite, and they lifted up the container between earth and heaven.
Kisha nikatazama juu: na pale mbele yangu, walikuwepo wanawake wawili, wakiwa na upepo katika mabawa yao! Walikuwa na mabawa kama ya korongo, nao wakainua kile kikapu na kuruka nacho kati ya mbingu na nchi.
10 And I said to the angel who was speaking with me, “Where are they taking the container?”
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Wanakipeleka wapi hicho kikapu?”
11 And he said to me, “To a house that may be built for it in the land of Shinar, and so that it may be established and set there upon its own base.”
Akanijibu, “Wanakipeleka katika nchi ya Babeli na kujenga nyumba kwa ajili yake. Itakapokuwa tayari, kikapu kitawekwa pale mahali pake.”

< Zechariah 5 >