< Psalms 138 >

1 Of David himself. O Lord, I will confess to you with my whole heart, for you have heard the words of my mouth. I will sing psalms to you in the sight of the Angels.
Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2 I will adore before your holy temple, and I will confess your name: it is above your mercy and your truth. For you have magnified your holy name above all.
Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
3 On whatever day that I will call upon you: hear me. You will multiply virtue in my soul.
Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
4 May all the kings of the earth confess to you, O Lord. For they have heard all the words of your mouth.
Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5 And let them sing in accordance with the ways of the Lord. For great is the glory of the Lord.
Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
6 For the Lord is exalted, and he looks with favor on the humble. But the lofty he knows from a distance.
Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
7 If I wander into the midst of tribulation, you will revive me. For you extended your hand against the wrath of my enemies. And your right hand has accomplished my salvation.
Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8 The Lord will provide retribution on my behalf. O Lord, your mercy is forever. Do not disdain the works of your hands.
Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.

< Psalms 138 >