< Proverbs 21 >

1 Just as with the dividing of the waters, so also is the heart of the king in the hand of the Lord. He shall bend it whichever way he wills.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Every way of a man seems right to himself. But the Lord weighs hearts.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 To do mercy and judgment is more pleasing to the Lord than sacrifices.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 To lift up the eyes is to enlarge the heart. The lamp of the impious is sin.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 The intentions of the robust continually bring forth abundance. But all the lazy are continually in need.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 Whoever gathers treasures by a lying tongue is vain and heartless. And he will stumble into the snares of death.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 The robberies of the impious will drag them down, because they were not willing to do judgment.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 The perverse way of a man is foreign. But whoever is pure: his work is upright.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 It is better to sit in a corner of the attic, than with a contentious woman and in a shared house.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 The soul of the impious desires evil; he will not take pity on his neighbor.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 When the pestilent is punished, a little one will become wiser. And if he pursues what is wise, he will receive knowledge.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 The just thinks carefully about the house of the impious, so that he may draw the impious away from evil.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 Whoever blocks his ears to the outcry of the poor shall also cry out himself, and he will not be heeded.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 A surprise gift extinguishes anger. And a gift concealed in the bosom extinguishes the greatest indignation.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 It is gladness for the just to do judgment; and it is dread for those who work iniquity.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 A man who wanders astray from the way of doctrine will linger in the company of the giants.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 Whoever loves a feast will be in deprivation. Whoever loves wine and fatness will not be enriched.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 The impious is given over instead of the just, and the iniquitous is given over in place of the upright.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 It is better to live in a deserted land, than with a quarrelsome and emotional woman.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 There is desirable treasure, as well as oil, in the habitations of the just. And the imprudent man will waste it.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 Whoever follows justice and mercy shall discover life, justice, and glory.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 The wise has ascended the city of the strong, and he has torn down the bulwark of its confidence.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 Whoever guards his mouth and his tongue guards his soul from anguish.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 A proud and arrogant one is also called ignorant, if he, in anger, acts according to pride.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 Desires kill the lazy, for his hands are not willing to work at all.
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 He covets and desires all day long. But whoever is just shall distribute and shall not cease.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 The sacrifices of the impious are abominable, because they are offered out of wickedness.
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 A lying witness will perish. An obedient man shall speak of victory.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 The impious man insolently hardens his face. But whoever is upright corrects his own way.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 There is no wisdom, there is no prudence, there is no counsel, which is against the Lord.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 The horse is prepared for the day of battle. But the Lord bestows salvation.
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Proverbs 21 >