< Numbers 31 >

1 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
2 “First, avenge the sons of Israel from the Midianites, and then you shall be gathered to your people.”
“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
3 And immediately Moses said: “Arm the men among you for a battle, so that they may be able to fulfill the retribution of the Lord on the Midianites.
Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
4 Let one thousand men be chosen from each tribe of Israel, who shall be sent to war.”
Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
5 And they gave one thousand from each tribe, that is, twelve thousand foot soldiers for battle.
Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
6 And Moses sent them with Phinehas, the son of Eleazar the priest; also, he delivered to him the holy vessels, and the trumpets to sound.
Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
7 And when they had fought against the Midianites and had prevailed, they killed all the men.
Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
8 And they put to death by the sword their kings: Evi, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba, the five leaders of the nation, and also Balaam the son of Beor.
Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
9 And they seized their women and little ones, and all their cattle, and all their goods; whatever they were able to have, they despoiled.
Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
10 Both their cities and their villages, as well as their fortresses, they burned.
Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
11 And they carried away prey from everything that they had seized, both of men and of beasts.
Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
12 And they led these to Moses and Eleazar the priest, and to all the multitude of the sons of Israel. But the remainder of the articles they carried to the camp on the plains of Moab, next to the Jordan, opposite Jericho.
nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
13 Then Moses, and Eleazar the priest, and all the leaders of the assembly went out to meet them beyond the camp.
Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
14 And Moses, being angry with the leaders of the army, and the tribunes, and the centurions, who had arrived from the battle,
Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
15 said: “Why have you spared the females?
Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
16 Are not these the ones who deceived the sons of Israel at the suggestion of Balaam, and who caused you betray the Lord by the sin of Peor, because of which the people also were struck down?
“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
17 Therefore, put to death all of them: whatever is of the male sex, even among the little ones, and cut the throats of those women who have known men by sexual relations.
Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
18 But the young girls, and all female virgins, reserve for yourselves.
lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
19 And remain beyond the camp for seven days. Whoever has killed a man, or who has touched one that was killed, shall be purified on the third day and on the seventh day.
“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
20 And all of the spoils, whether it is a garment, or a vessel, or another useful thing, made from the pelts or hair of goats, or from wood, shall be expiated.”
Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
21 Likewise, Eleazar the priest spoke in this manner to the men of the army who had fought: “This is the precept of the law, which the Lord has commanded Moses:
Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
22 Gold, and silver, and brass, and iron, and lead, and tin,
Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
23 and all that may be able to pass through fire, shall be purified by fire. But whatever is not able to sustain fire shall be sanctified with the waters of expiation.
na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
24 And you shall wash your garments on the seventh day, and, after having been purified, you shall enter the camp.”
Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
25 And the Lord also said to Moses:
Bwana akamwambia Mose,
26 “Take the sum of those things which were captured, from man even to beast, you and Eleazar the priest, and the leaders of the common people.
“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
27 And you shall divide the prey equally, among those who went out to war and fought, and among the remainder of the multitude.
Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
28 And you shall separate a portion for the Lord from the portion of those who fought and were in the battle: one soul out of five hundred, as much from humans, as from oxen and donkeys and sheep.
Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
29 And you shall give it to Eleazar the priest, because these are the first-fruits of the Lord.
Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
30 Likewise, from the half of the portion belonging to the sons of Israel, you shall receive the fiftieth head of humans, and of oxen, and donkeys, and sheep, and of all living things, and you shall give these to the Levites who stand watch over the care of the tabernacle of the Lord.”
Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
31 And Moses and Eleazar did just as the Lord had instructed.
Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Now the prey which the army had seized was six hundred seventy-five thousand sheep,
Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
33 seventy-two thousand oxen,
ngʼombe 72,000,
34 sixty-one thousand donkeys,
punda 61,000,
35 and thirty-two thousand human lives, of the female sex, who had not known men.
na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
36 And one half of the portion was given to those who had been in the battle: three hundred thirty-seven thousand five hundred sheep.
Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
37 From these, for the portion of the Lord, there were accounted: six hundred seventy-five sheep;
ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
38 and from the thirty-six thousand oxen, seventy-two oxen;
ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
39 from the thirty thousand five hundred donkeys, sixty-one donkeys.
punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
40 From the sixteen thousand human souls, there fell to the portion of the Lord thirty-two souls.
Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
41 And Moses delivered the number of the first-fruits of the Lord to Eleazar the priest, just as had been commanded of him,
Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
42 from the one half portion belonging to the sons of Israel, which he had separated from the portion of those who had been in the battle.
Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
43 Yet truly, from the one half portion which fell to the remainder of the multitude, that is, from the three hundred thirty-seven thousand five hundred sheep,
nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
44 and from the thirty-six thousand oxen,
ngʼombe 36,000,
45 and from the thirty thousand five hundred donkeys,
punda 30,500,
46 and from the sixteen thousand persons,
na wanadamu 16,000.
47 Moses took the fiftieth head, and gave it to the Levites who stand watch at the tabernacle of the Lord, just as the Lord had instructed.
Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
48 And when the leaders of the army, and the tribunes, and the centurions had approached Moses, they said:
Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
49 “We, your servants, have taken a census of the number of the fighting men, whom we had under our hand, and indeed not one was lacking.
na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
50 For this reason, we offer as gifts to the Lord whatever gold each one was able to find amid the spoils, in anklets and arm bands, rings and bracelets, and little chains, so that you may intercede for us to the Lord.”
Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
51 And Moses and Eleazar the priest received all the gold in its various kinds,
Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
52 weighing sixteen thousand seven hundred fifty shekels, from the tribunes and the centurions.
Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
53 For whatever each one had taken away in the spoils was his own.
Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
54 And having been accepted, they took it into the tabernacle of the testimony, as a memorial of the sons of Israel before the Lord.
Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

< Numbers 31 >