< Numbers 26 >

1 After the blood of the guilty was shed, the Lord said to Moses, and to Eleazar the son of Aaron the priest:
Ilitokea baada ya tauni ambayo BWANA alimwambia Musa na Eliazari mwana wa Haruni kuhani, Alisema,
2 “Number the entire sum of the sons of Israel, from twenty years and above, by their houses and kinships, all who are able to go forth to war.”
Wahesabu watu wote wa Israeli, kuanzia miaka ishirini na zaidi, kwa jamaa ya familia zao wote ambao wanaweza kwenda kwenye vita kwa ajili ya Israeli.”
3 And so, Moses and Eleazar the priest, who were in the plains of Moab, above the Jordan, opposite Jericho, spoke to those who were
Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakawaambia katika uwanda wa Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko na kusema,
4 from twenty years and above, just as the Lord had commanded. And this is their number:
Wahesabuni watu, kuanzi umri wa miaka ishirini na zaidi kama BWANA alivyomwamuru Musa na watu wa Israeli walitoka katika nchi ya Misri.”
5 Ruben, the firstborn of Israel; his son, Hanoch, from whom is the family of the Hanochites; and Pallu, from whom is the family of the Palluites;
Reubeni ndiye aliyekuwa wa kwanza, Kutoka kwa mwana wake Hanoki ulitokea ukoo wa Wahanoki. Kutoka kwa Palu ulitokea ukoo wa Wapalu.
6 and Hezron, from whom is the family of the Hezronites; and Carmi, from whom is the family of the Carmites.
Kutoka Hezroni. ulitokea ukoo wa Wahezroni. Kutoka kwa Kami ulitokea ukoo wa Wakami.
7 These are the families of the stock of Ruben, whose number was found to be forty-three thousand and seven hundred thirty.
Hizi ndizo zilikuwa koo za uzao wa Reubeni, ambzo idadi yao ilikuwa wanaume 43, 730.
8 The son of Phallu: Eliab;
Eliabu alikuwa mwana wa Palu.
9 his sons, Nemuel and Dathan and Abiram. These are Dathan and Abiram, the leaders of the people, who rose up against Moses and Aaron in the sedition at Korah, when they rebelled against the Lord.
Wana wa Eliabu walikuwa ni Nemueli, Dathani. na Abiramu. Hawa ni walewale Dathani na Abiramu waliomfuata Kora waliompinga Musa na Haruni na kumpinga BWANA.
10 And the earth, opening its mouth, devoured Korah, with many others dying, when the fire burned two hundred fifty men. And a great miracle was wrought,
Pale ambapo dunia ilifungua kinywa na kuwameza pamoja na Kora wakati ambapo wafuasi wa Kora walikufa. Wakati ule, moto uliteketeza wanaume 250, amboa wlikuwa ishara ya onyo.
11 so that, when Korah perished, his sons did not perish.
Lakini uzao wa Kora haukufa.
12 The sons of Simeon, by their kinships: Nemuel, from him is the family of the Nemuelites; Jamin, from him is the family of the Jaminites; Jachin, from him is the family of the Jachinites;
Ukoo wa uzao wa Simeoni walikuwa hawa wafuatao: Kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli, kwa Jamini, ukoo wa Wajamini, kwa Jakini, ukoo wa Wajakini,
13 Sohar, from him is the family of the Soharites; Shaul, from him is the family of the Shaulites.
kwa Zera, ukoo wa Wazera, kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
14 These are the families of the stock of Simeon, whose entire number was twenty-two thousand two hundred.
Hizi ndizo koo za uzao wa Simeoni, idadi yao ilikuwa wanaume 22, 200.
15 The sons of Gad, by their kinships: Zephon, from him is the family of the Zephonites; Haggi, from him is the family of the Haggites; Shuni, from him is the family of the Shunites;
Koo za uzao wa Gadi zilikuwa hizi: Kwa Zefoni, Ukoo wa Wazefoni, kwa Hagi, ukoo wa Wahagi, kwa Shuni, ukoo wa Washuni,
16 Ozni, from him is the family of the Oznites; Eri, from him is the family of the Erites;
kwa Ozini, ukoo wa Waozini, kwa Eri, ukoo wa Waeri,
17 Arod, from him is the family of the Arodites; Areli, from him is the family of the Arelites.
kwa Arodi, ukoo wa Waarodi, kwa Areli, ukoo wa Waareli.
18 These are the families of Gad, whose entire number was forty thousand five hundred.
Hizi ndizo koo za uzao wa Gadi, idadi yao walikuwa wanaume 40, 500.
19 The sons of Judah: Er and Onan, who both died in the land of Canaan.
Wana wa Yuda walikwa Er na Onani, lakini hawa walifia katika nchi ya Kanaani.
20 And these were the sons of Judah, by their kinships: Shelah, from whom is the family of the Shelahites; Perez, from whom is the family of the Perezites; Zerah, from whom is the family of the Zerahites.
Koo zingine za uzao wa Yuda zilikuwa hizi: Kwa Shela, ukoo wa Washela, kwa Perezi, ukoo wa Waperezi, na kwa Zera, ukoo wa Wazera.
21 Moreover, the sons of Phares were: Hezron, from whom is the family of the Hezronites; and Hamul, from whom is the family of the Hamulites.
Uzao wa Perezi walikuwa hawa: Kwa Hezroni, ukoo wa Wahezroni, kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
22 These are the families of Judah, whose entire number was seventy-six thousand five hundred.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda, idadi yao ilikuwa wanaume 76, 500.
23 The sons of Issachar, by their kinships: Tola from whom is the family of the Tolaites; Puvah, from whom is the family of the Puvahites;
Koo za uzao wa Isakari zilikuwa hizi: Kwa Tola, ukoo wa Watola, kwa Puva, ukoo wa Wapuva,
24 Jashub, from whom is the family of the Jashubites; Shimron, from whom is the family of the Shimronites.
kwa Jashubu, ukoo wa Wajashubu, kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
25 These are the kinships of Issachar, whose number was sixty-four thousand three hundred.
Hizi ndizo zilikuwa koo za Isakari, Idadi yao ilikuwa wanaume 64, 300.
26 The sons of Zebulon by their kinships: Sered, from whom is the family of the Seredites; Elon, from whom is the family of the Elonites; Jahleel, from whom is the family of the Jahleelites.
Koo za uzao wa Zabuloni zilikuwa hizi: Kwa Seredi, ukoo wa Waseredi, kwa Eloni, ukoo wa Waeloni, kwa Jahaleeli, ukoo wa Wajahaleeli.
27 These are the kinships of Zebulun, whose number was sixty thousand five hundred.
Hizi ndizo zilikuwa koo za Zabuloni, idadi y ao ilikuwa wanaume 60, 500.
28 The sons of Joseph by their kinships: Manasseh and Ephraim.
Koo za uzao wa Ysufu zilikuwa Manase na Efraimu.
29 From Manasseh was born Machir, from whom is the family of the Machirites. Machir conceived Gilead, from whom is the family of the Gileadites.
Huu ndio uliokuwa uzao wa Manase: Kwa Machiri, ukoo wa Wamachiri (Machiri ndiye aliyekuwa baba wa Giliedi), kwa Giliedi, ukoo wa Wagiliedi.
30 Gilead had sons: Jezer, from whom is the family of the Jezerites; and Helek, from whom is the family of the Helekites;
Wazo wa Giliedi walikuwa hawa wfuatao: Kwa Lezeri, ukoo wa Walezeri, kwa Helweki, ukoo wa Waheleki, kwa Asrieli,
31 and Asriel, from whom is the family of the Asrielites; and Shechem, from whom is the family of the Shechemites;
ukoo wa Asrieli wa Waasrieli, kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu,
32 and Shemida, from whom is the family of the Shemidaites; and Hepher, from whom is the family of the Hepherites.
kwa Shemida, ukoo wa Washemida, kwa Hefa, ukoo wa Wahefa.
33 Now Hepher was the father of Zelophehad, who had no sons, but only daughters, whose names are these: Mahlah, and Noa, and Hoglah, and Milcah, and Tirzah.
Zelofehadi mwana wa Hefa hakuwa na watoto wa kiume bali alikuwa na mabinti. Majina ya binti zake yalikuwa Mahilahi, Noha, Hoglaha, Milika, na Tiriza.
34 These are the families of Manasseh, and their number was fifty-two thousand seven hundred.
Hizi ndizo koo za Manase, idadi yao ilikuwa wanaume 52, 700.
35 Now the sons of Ephraim by their kinships were these: Shuthelah, from whom is the family of the Shuthelahites; Becher, from whom is the family of the Becherites; Tahan, from whom is the family of the Tahanites.
Koo za wana wa uzao wa Efraimu zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Shuthelaha, ukoo wa Washutheleha, kwa Becheri, ukoo wa Wabecheri, kwa Tahana, ukoo wa Watahana.
36 Furthermore, the son of Shuthelah was Eran, from whom is the family of the Eranites.
Uzao wa Shuthelaha walikuwa, kwa Erani, ukoo wa Waerani.
37 These are the kinships of the sons of Ephraim, whose number was thirty-two thousand five hundred.
Hizi ndizo koo za uzao wa Efraimu, idadi yao ilikuwa wanaume 32, 500. Huu ndio uzao wa Yusufu, uliohesabiwa toka kila koo zao.
38 These are the sons of Joseph by their families: the sons of Benjamin in their kinships: Bela, from whom is the family of the Belaites; Ashbel, from whom is the family of the Ashbelites; Ahiram, from whom is the family of the Ahiramites;
Koo za uzao wa Benjamini zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Bela ukoo wa Wabela, kwa Ashibeli, ukoo wa Washibeli, kwa Ahiramu, ukoo wa Wahiramu,
39 Shupham, from whom is the family of the Shuphamites; Hupham, from whom is the family of the Huphamites.
kwa Shefufamu, ukoo wa Washefumamu, kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
40 The sons of Bela: Arad and Naaman. From Arad, the family of the Aradites; from Naaman, the family of the Naamanites.
Wana wa Bela walikuwa ni Ardi na Naamani. Kutoka kwa Ardi ulijitokeza ukoo wa Waardi, na kutoka kwa Naamani ukajaitokeza ukoo wa Wanaamani.
41 These are the sons of Benjamin by their kinships, whose number was forty-five thousand six hundred.
Hizi ndizo koo za uzao wa Benjamini. Idadai yao ilikuwa wanaume 45, 600.
42 The sons of Dan by their kinships: Shuham, from whom is the family of the Shuhamites. These are the kinships of Dan by their families.
Kooo za uzao wa Dani zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo koo za uzao wa Dani.
43 All these were Shuhamites, whose number was sixty-four thousand four hundred.
Idadi ya koo zote za Washuhamu ilikuwa wanaume 64, 400.
44 The sons of Asher by their kinships: Imnah, from whom is the family of the Imnahites; Ishvi, from whom is the family of the Ishvites; Beriah, from whom is the family of the Beriahites.
Koo za uzao wa Asheri zilikuwa zifuatazo: Kwa Imna, ukoo wa Waimna, kwa Ishvi, ukoo wa Waishivi, kwa Beria, ukoo wa Waberia.
45 The sons of Beriah: Heber, from whom is the family of the Heberites; and Malchiel, from whom is the family of the Malchielites.
Uzao wa Beria walikuwa hawa: Kwa Heberi, ukoo wa Waheberi, kwa Malikieli, ukoo wa Wamalikieli.
46 Now the name of the daughter of Asher was Serah.
Jina la binti wa Asheri lilikuwa Sera.
47 These are the kinships of the sons of Asher, and their number was fifty-three thousand four hundred.
Hizi ndizo koo za uzao wa Asheri, idadi yao ilikuwa wanaume 53, 400.
48 The sons of Naphtali by their kinships: Jahzeel, from whom is the family of the Jahzeelites; Guni, from whom is the family of the Gunites;
Koo za uzao wa Naftali zilikuwa zifuatazo: Kwa Jahazeeli, ukoo wa Wajahazeel, kwa Guni, ukoo wa Waguni,
49 Jezer, from whom is the family of the Jezerites; Shillem, from whom is the family of the Shillemites.
kwa Jezeri, ukoo wa Wajezeri, kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
50 These are the kinships of the sons of Naphtali by their families, whose number was forty-five thousand four hundred.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za uzao wa Naftali, idadi yao walikuwa wanaume 45, 000.
51 This is the sum of the sons of Israel, who were counted: six hundred thousand and one thousand seven hundred thirty.
Hii ndiyo iliyokuwa jumla kuu ya wanaume wa Israeli: 601, 730.
52 And the Lord spoke to Moses, saying:
BWANA akanena na Musa akamwambia,
53 “The land shall be divided to these, as their possessions, according to the number of their names.
Ile ardhi itagawanywa kati ya wanaume hawa kama urithi wao kwa kufuata idadi ya majina yao.
54 To the greater number you shall give a greater portion, and to the lesser number, a lesser portion. To each one, just as they have now been counted, a possession shall be delivered.
Kwa zile koo kubwa utawagawia urithi mkubwa, na kwa koo ndogo ndogo utawagawia urithi kidogo. Kwa kila familia utawapa urithi kufuata idadi ya wanaume waliohesabiwa.
55 Yet only in so far as the land is divided by lot to a tribe and to families.
Lakini ardhi itagawiwa kwa kupigiwa kura. Watairithi nchi kama itakavyogawiwa kwa kufuata koo za mababu.
56 Whatever the lot will happen to be, it shall be accepted, either by the greater, or by the lesser.
Urithi huu utagiwiwa kufuata koo kubwa na ndogo, watagawiwa kwa kufuata kura zitakavyokuwa.
57 Likewise, this is the number of the sons of Levi by their families: Gershon, from whom is the family of the Gershonites; Kohath, from whom is the family of the Kohathites; Merari, from whom is the family of the Merarites.
Koo za Walawi, zilizohesabiwa kwa kufuata ukoo kwa ukoo, walikuwa hivi: Kwa Gerishoni, ukoo wa Wagerishoni, kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi, kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
58 These are the families of Levi: The family of Libni, the family of Hebroni, the family of Mahli, the family of Mushi, the family of Korah. Yet truly, Kohath conceived Amram,
Koo za walawi zilikuwa hzi: ukoo wa Walibni, Ukoo wa Wahebroni, ukoo wa Wamahali, ukoo wa Wamushi, na ukoo wa Wakora. Kohathi alikuwa wa uzao wa Amramu.
59 who had a wife, Jochebed, the daughter of Levi, who was born to him in Egypt. She bore, to her husband Amram: sons, Aaron and Moses, as well as their sister, Miriam.
Jina la mke wa Amramu lilikuwa Jokibed, wa ukoo wa Lawi, aliyekuwa amezaliwa kwa Walawi kule Misri. Alimzalia Amramu watoto wao, ambao walikuwa ni Haruni, Musa, na Miriamu dada yao.
60 From Aaron were born Nadab and Abihu, and Eleazar and Ithamar.
Kwa Haruni alizaliwa Nadabu na Abihu, Eliazari na Ithamari.
61 Of these, Nadab and Abihu died, when they had offered strange fire before the Lord.
Nadabu na Abihu walikufa walipotoa sadaka kwa BWANA sadaka ya moto isiyokubalika.
62 And these were all who were numbered: twenty-three thousand of the male gender, from one month and above. For they were not counted among the sons of Israel, neither was a possession given to them with the others.
Waume walioheabaiwa miionigoni mwao walikuwa elfu ishirini na tatu, hawa nia wale wa umri wa mwezi mmoja na zaidi. Lakini hawakuhesabiwa kati ya wazawa wa Israeli kwa sababu hawakupewa urithi miongoni mwa wana wa Israeli.
63 This is the number of the sons of Israel, who were enrolled by Moses and by Eleazar the priest, in the plains of Moab, above the Jordan, opposite Jericho.
Hawa nadio wale walihesabiwa na Musa na Eliazari kuhani. Waliwahesabu watu wa Israeli katika uwanda wa Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko.
64 Among these, not one of them was numbered before, by Moses and Aaron in the desert of Sinai.
Lakini miongoni mwa hawa hapakuwa na mwanamume aliyehasabiwa na Musa na Haruni kuhani wakati wana wa uzao wa Israeli walipohesabiwa katika jangwa la Sinai.
65 For the Lord had foretold that all would die in the wilderness. And not one of them remained, except Caleb the son of Jephunneh, and Joshua the son of Nun.
Kwa BWANA alikuwa amesema kuwa kwa hakika watu hao wote wangefia jangwani. Hapakuwa na mtu aliyebaki miongoni mwao, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Joshua mwana wa Nuni.

< Numbers 26 >