< Numbers 25 >

1 Now Israel, at that time, dwelt in Shittim, and the people were fornicating with the daughters of Moab,
Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
2 who called them to their sacrifices. And they ate, and they adored their gods.
kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
3 And Israel was initiated into Baal of Peor. And so the Lord, being angry,
Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
4 said to Moses, “Take all the leaders of the people, and hang them on gallows against the sun, so that my fury may be averted from Israel.”
BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
5 And Moses said to the judges of Israel, “Let each one kill his neighbors, who have been initiated into Baal of Peor.”
Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
6 And behold, one of the sons of Israel entered, in the sight of his brothers, to a prostitute of Midian, within view of Moses and of all the crowd of the sons of Israel, who were weeping before the door of the tabernacle.
Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
7 And when Phinehas the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, had seen it, he rose up from the midst of the multitude, and, seizing a dagger,
Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
8 he entered after the Israelite man, into the brothel, and he pierced both of them at the same time, specifically, the man and the woman at the location of their genitals. And the scourge ceased from among the sons of Israel.
Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
9 And there were slain twenty-four thousand men.
Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
10 And the Lord said to Moses:
BWANA akanena na Musa, akasema,
11 “Phinehas the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, has averted my wrath from the sons of Israel. For he was moved against them by my zeal, so that I myself, in my zeal, might not wipe away the sons of Israel.
“Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
12 Because of this, say to him: Behold, I give to him the peace of my covenant.
Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
13 And the covenant of the everlasting priesthood shall be as much for him as for his offspring. For he was zealous on behalf of his God, and he has made expiation for the wickedness of the sons of Israel.”
Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
14 Now the name of the Israelite man, who was killed with the Midianite woman, was Zimri the son of Salu, a leader from the kinship and tribe of Simeon.
Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
15 Moreover, the Midianite woman, who was put to death together with him, was called Cozbi the daughter of Zur, a most noble leader among the Midianites.
Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
16 And the Lord spoke to Moses, saying:
Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
17 “Let the Midianites perceive you as enemies, and strike them down,
“Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
18 for they, too, have behaved with hostility against you, and they have deceived you insidiously by means of the idol Peor, and by Cozbi, the daughter of a commander of Midian, their sister, who was struck down in the day of the scourge because of the sacrilege of Peor.”
kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”

< Numbers 25 >