< Numbers 10 >

1 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose:
2 “Make for yourself two trumpets of ductile silver, with which you may be able to call together the multitude when the camp is to be moved.
“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
3 And when you sound the trumpets, all the multitude shall gather to you at the door of the tabernacle of the covenant.
Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
4 If you sound it only once, the leaders and the heads of the multitude of Israel shall come to you.
Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
5 But if the sound of the trumpets is prolonged, but with interruptions, those who are toward the east side shall move the camp first.
Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
6 Then, at the second sounding of the trumpet with the same cadence, those who live toward the south shall take up their tents. And the remainder shall act in like manner, when the trumpets shall reverberate for a departure.
Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
7 But when the people are to be gathered together, the sound of the trumpets shall be simple, and the sounds shall not be separated.
Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
8 Now it is the sons of Aaron the priest who shall sound the trumpets. And this shall be an everlasting ordinance, in your generations.
“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
9 If you go forth to war from your land, against the enemies who set out against you, you shall sound the trumpets repeatedly, and there shall be a remembrance of you before the Lord your God, so that you may be rescued from the hands of your enemies.
Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
10 If at any time you will have a banquet, and on feast days, and on the first days of the months, you shall sound the trumpets over the holocausts and the peace-offering victims, so that they may be for you as a remembrance by your God. I am the Lord your God.”
Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
11 In the second year, in the second month, on the twentieth day of the month, the cloud was lifted up from the tabernacle of the covenant.
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
12 And the sons of Israel set out by their companies from the desert of Sinai, and the cloud rested in the wilderness of Paran.
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
13 And the first to move their camp, according to the command of the Lord by the hand of Moses,
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
14 were the sons of Judah by their companies, whose leader was Nahshon the son of Amminadab.
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15 In the tribe of the sons of Issachar, the leader was Nathanael the son of Zuar.
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16 In the tribe of Zebulon, the leader was Eliab the son of Helon.
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
17 And the tabernacle was taken down, because the sons of Gershon and Merari, who carry it, were departing.
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
18 And the sons of Ruben also set out, by their companies and ranks, whose leader was Elizur the son of Shedeur.
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
19 And in the tribe of Simeon, the leader was Shelumiel the son of Zurishaddai.
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
20 And in the tribe of Gad, the leader was Eliasaph the son of Reuel.
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
21 Then the Kohathites also set out, carrying the Sanctuary. The tabernacle was carried, all the while, until they arrived at the place for setting it up.
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
22 The sons of Ephraim also moved their camp by their companies, and the leader of their army was Elishama the son of Ammihud.
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
23 And in the tribe of the sons of Manasseh, the leader was Gamaliel the son of Pedahzur.
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
24 And in the tribe of Benjamin, the leader was Abidan the son of Gideoni.
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
25 The last of all the camp to set out were the sons of Dan by their companies, and the leader of their army was Ahiezer the son of Ammishaddai.
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
26 And in the tribe of the sons of Asher, the leader was Pagiel the son of Ochran.
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
27 And in the tribe of the sons of Naphtali, the leader was Ahira the son of Enan.
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
28 These were the camps and departures of the sons of Israel by their companies, when they went forth.
Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
29 And Moses said to Hobab the son of Raguel the Midianite, his kinsman: “We are setting out to the place which the Lord will give to us. Come with us, so that we may do good to you. For the Lord has promised good things to Israel.”
Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
30 And he answered him, “I will not go with you, but I will return to my own land, in which I was born.”
Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
31 And he said: “Do not choose to leave us. For you know in which places in the desert we ought to make camp, and so you shall be our guide.
Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
32 And if you come with us, whatever will be best among the riches which the Lord will deliver to us, we will give to you.”
Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
33 Therefore, they set out from the Mountain of the Lord on a journey of three days. And the ark of the covenant of the Lord preceded them, for three days, in order to provide a place for the camp.
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
34 Likewise, the cloud of the Lord was over them, throughout the day, while they proceeded.
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
35 And when the ark was lifted up, Moses said, “Rise up, O Lord, and let your enemies be scattered, and let those who hate you flee from your face.”
Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
36 And when it was set down, he said: “Return, O Lord, to the multitude of the army of Israel.”
Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

< Numbers 10 >