< Leviticus 3 >

1 But if his oblation will be a sacrifice of peace offerings, and he wishes to offer it from the oxen, whether male or female, he shall offer what is immaculate, in the sight of the Lord.
Kama mtu atoa dhabihu ambayo ni matoleo ya amani ya mnyama kutoka katika kundi, dume au jike, lazima atatoa mnyama asiyena kasoro mbele ya Bwana.
2 And he shall place his hand upon the head of his victim, which shall be immolated at the entrance of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron, the priests, shall pour the blood all around the altar.
Ataweka mikono yake juu ya sadaka yake na atamchinja mbele ya mlango wa hema ya kukutania. Kisha wana wa Haruni makuhani watanyunyizia damu yake katika pande za madhabahu.
3 And they shall offer from the sacrifice of peace offerings, as an oblation to the Lord: the fat which covers the vital organs, and whatever fat is interior,
Mtu akitoa dhabihu ya amani itolewayo kwa moto kwa ajili ya Bwana. Mafuta yanayofunika au yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
4 the two kidneys with the fat that covers the sides, and the mesh of the liver with the two little kidneys.
figo mbili na mafuta yaliyofunika kiunoni na yanayozunguka ini, pamoja na figo atayatoa pamoja.
5 And they shall burn them upon the altar as a holocaust, placing fire under the wood, as an oblation of a most sweet odor to the Lord.
Wana wa Haruni watayachoma hayo katika madhabahu pamoja na sadaka ya kutekezwa, juu ya kuni zilizo kwenye moto. Zitaleta harufu nzuri mbele ya Bwana; itakuwa sadaka ya itolewayo kwake kwa moto.
6 Yet truly, if his oblation and the sacrifice of peace offerings will be from the sheep, whether he will offer a male or a female, they shall be immaculate.
Kama dhabihu ya amani ya mtu itolewayo kwa Bwana ni kutoka katika mifugo ni mbuzi au kondoo ni dume au jike, atatoa dhabihu isiyo na kasoro.
7 If he will offer a lamb in the sight of the Lord,
Kama atatoa mwanakondoo kwa ajili ya dhabihu yake, atamtoa mbele za Bwana.
8 he shall place his hand upon the head of the victim. And it shall be immolated at the vestibule of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron shall pour its blood all around the altar.
Ataweka mkono wake juu ya ya kichwa cha dhabihu yake na atamchinja mbele ya hema ya kukutania. Ndipo wana wa Haruni watanyunyizia damu pande za madhabahu.
9 And they shall offer from the victim of peace offerings, as a sacrifice to the Lord: the fat, and the entire rump
Mtu akitoa sadaka ya dhabihu ya amani kama sadaka ya kusogezwa kwa moto kwa Bwana. Mafuta, mafuta ya mkia yatakatwa hapo karibu na mfupa wa kiuno, na mafuta yanayofunika matumbo na mafuta yaliyo katika matumbo,
10 with the kidneys, and the fat that covers the abdomen, and all the vital organs, and both the little kidneys with the fat that is near the sides, and the mesh of the liver with the little kidneys.
na figo zote mbili na mafuta yanayofunika yaliyo karibu na kiuno kitambi kilicho karibu na ini na figo ataziondoa zote.
11 And the priest shall burn them upon the altar, as fuel for the fire and as an oblation of the Lord.
Na kuhani atayatekeza yote kwa moto katika madhabahu kama sadaka ya chakula isogezwayo kwa moto kwa Bwana.
12 If his oblation will be a goat, and he will offer it to the Lord,
Kama matoleo ya mtu ni mbuzi, ndipo ataitoa mbele ya Bwana.
13 he shall place his hand upon its head, and he shall immolate it at the entrance of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron shall pour its blood all around the altar.
Ataweka mikono yake juu ya kichwa cha mbuzi na atamchinja mbele ya hema ya kukutania. Ndipo wana wa Haruni watanyunyizia damu pande zote za madhabahu.
14 And they shall take from it, to feed the Lord’s fire: the fat which covers the abdomen, and that which covers all the vital organs,
Mtu akitoa dhabihu kwa Bwana kwa njia ya moto. Ataondoa mafuta yanayozunguka matumbo, na mafuta yote yanayozunguka matumbo.
15 the two little kidneys with the mesh that is over them near the sides, and the fat of the liver with the little kidneys.
Ataondoa pia figo mbili na mafuta yanayozunguka, ambayo yanazunguka kiuno na kitambi cha maini pamoja na figo.
16 And the priest shall burn them upon the altar, as nourishment for the fire and as a most sweet odor. All the fat shall be for the Lord;
Kuhani atateketeza yote juu ya madhabahu kama matoleo ya chakula yatolewayo kwa moto, ni sadaka ya kuleta harufu nzuri sana. Mafuta yote ni ya Bwana.
17 by a perpetual law, in your generations and in all of your habitations, neither blood nor fat shall you eat at all.
Itakuwa ni amri ya kudumu kwa kizazi cha watu katika maeneo yote mtakapotengeneza makazi, kwamba hamtakula mafuta au damu.”'

< Leviticus 3 >