< Leviticus 18 >

1 And the Lord spoke to Moses, saying:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 Speak to the sons of Israel, and you shall say to them: I am the Lord your God.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 You shall not act according to the custom of the land of Egypt, in which you have lived; nor shall you behave according to the habit of the region of Canaan, into which I will lead you; neither shall you walk in their ordinances.
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 You shall accomplish my judgments, and you shall observe my precepts, and you shall walk in them. I am the Lord your God.
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 Keep my laws and judgments; when a man does these, he shall live by them. I am the Lord.
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 No man shall approach her who is a close blood-relative to him, so as to uncover her nakedness. I am the Lord.
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 You shall not expose the nakedness of your father, or the nakedness of your mother. She is your mother; you shall not uncover her nakedness.
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 You shall not expose the nakedness of your father’s wife; for it is the nakedness of your father.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 You shall not uncover the nakedness of your sister, whether from father or from mother, whether she was born at home or abroad.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 You shall not uncover the nakedness of your son’s daughter, or your daughter’s daughter; for it is your own nakedness.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 You shall not uncover the nakedness of your father’s wife’s daughter, whom she bore to your father, and who is your sister.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 You shall not expose the nakedness of your father’s sister; for she is the flesh of your father.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 You shall not uncover the nakedness of your mother’s sister, because she is the flesh of your mother.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 You shall not uncover the nakedness of your father’s brother, nor shall you approach his wife, who is joined to you by affinity.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 You shall not uncover the nakedness of your daughter-in-law, for she is your son’s wife; neither shall you expose her dishonor.
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 You shall not uncover the nakedness of your brother’s wife; for it is the nakedness of your brother.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 You shall not uncover the nakedness of your wife and her daughter. You shall not take her son’s daughter or her daughter’s daughter, so as to uncover her dishonor; for they are her flesh, and such sexual intercourse is incest.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 You shall not take your wife’s sister as a rival mistress; nor shall you uncover her nakedness, while your wife is still living.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 You shall not approach a woman who is undergoing menstruation, nor shall you uncover her foulness.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 You shall not have sexual intercourse with your neighbor’s wife, nor shall you be defiled by the mingling of seed.
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 You shall not give some of your seed to be consecrated to the idol Moloch, nor to pollute the name of your God. I am the Lord.
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 You shall not commit sexual acts with a male, in place of sexual intercourse with a female, for this is an abomination.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 You shall not commit sexual acts with any animal, nor shall you be defiled by it. A woman shall not lie down with a beast, nor commit sexual acts with it; for this is wickedness.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 Do not pollute yourselves with any of these things, by which all of the nations, which I will cast out in your sight, have been contaminated
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 and by which the land has been polluted. I will visit the wickedness of the land, so that it may vomit out its inhabitants.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 Keep my ordinances and judgments, and do not do any of these abominations: the native born, as well as the settler, who sojourns among you.
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 For all these detestable things were done by the inhabitants of the land who were here before you, and they have polluted it.
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 Therefore, beware, lest in a similar manner, it may vomit you out as well, if you do these same things, just as it vomited out the people who were before you.
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 Every soul who shall commit any of these abominations shall perish from the midst of his people.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Keep my commandments. Do not be willing to do the things which have been done by those who were before you, and do not be polluted by these things. I am the Lord your God.
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< Leviticus 18 >