< Leviticus 10 >

1 And the sons of Aaron, Nadab and Abihu, picking up their censers, placed fire in them and incense upon them, offering in the sight of the Lord a strange fire, such as was not instructed of them.
Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
2 And fire coming out from the Lord destroyed them, and they died in the sight of the Lord.
Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
3 And Moses said to Aaron: “This is what the Lord has spoken: ‘I will be sanctified in those who approach me, and I will be glorified in the sight of all the people.’” And upon hearing this, Aaron was silent.
Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
4 Then Moses called Mishael and Elzaphan, the sons of Uzziel, the paternal uncle of Aaron, and he said to them, “Go and take your brothers from the sight of the Sanctuary, and carry them beyond the camp.”
Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
5 And moving quickly, they took them as they lay, vested with linen tunics, and cast them outside, just as had been commanded them.
Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
6 And Moses said to Aaron, and to his sons, Eleazar and Ithamar: “Do not uncover your heads, and do not rend your garments, lest perhaps you may die, and indignation may rise up over the entire assembly. Let your brothers, and all the house of Israel, bewail the burning that the Lord has kindled.
Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
7 But you shall not depart from the door of the tabernacle; otherwise, you shall perish. For certainly the oil of holy anointing is upon you.” And they did all things according to the precept of Moses.
Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
8 The Lord also said to Aaron:
Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
9 “You shall not drink wine, nor anything that is able to inebriate you or your sons, when you enter into the tabernacle of the testimony, lest you die. For it is an everlasting precept in your generations.
“Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
10 And so may you have the knowledge to discern between holy and profane, between polluted and clean.
ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
11 And so may you teach the sons of Israel all my ordinances, which the Lord has spoken to them by the hand of Moses.”
ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
12 And Moses spoke to Aaron, and to his sons, Eleazar and Ithamar, who were remaining: “Take the sacrifice which remains from the oblation of the Lord, and eat it without leaven next to the altar, because it is the Holy of holies.
Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
13 For you shall eat it in a holy place, which is given to you and to your sons, from the oblations of the Lord, just as has been instructed me.
lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
14 Likewise, the breast which is offered, and the shoulder which is separated, you shall eat in a most clean place, you and your sons, and your daughters with you. For these have been set aside for you and your children from the victims which benefit the sons of Israel.
Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
15 Since they have lifted up in the sight of the Lord, the shoulder, and the breast, and the fat that is burned on the altar, these also belong to you and to your sons as a perpetual law, just as the Lord has instructed.”
Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
16 Meanwhile, when Moses was searching for the he-goat, which had been offered for sin, he discovered it burned up. And being angry against Eleazar and Ithamar, the sons of Aaron who were remaining, he said:
Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
17 “Why did you not eat the sacrifice for sin in the holy place, which is the Holy of holies, and which was given to you, so that you might carry the iniquity of the people, and might pray for them in the sight of the Lord,
“Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
18 especially since none of its blood has been brought into the holy places, and since you should have eaten it in the Sanctuary, as was instructed me?”
Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
19 Aaron responded: “This day, the victim for sin has been offered, and the holocaust in the sight of the Lord. But you see what has happened to me. How could I eat it, or please the Lord in the ceremonies, having a sorrowful mind?”
Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
20 But when Moses had heard this, he was satisfied.
Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.

< Leviticus 10 >