< Judges 15 >

1 Then, after some time, when the days of the wheat harvest were near, Samson arrived, intending to visit his wife, and he brought her a kid from the goats. And when he wanted to enter her bedroom, as usual, her father prohibited him, saying:
Baada ya siku kadhaa, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mbuzi mdogo akaenda kumtembelea mkewe. Akajiambia mwenyewe, “Nitaenda kwenye chumba cha mke wangu.” Lakini baba yake hakumruhusu aingie.
2 “I thought that you would hate her, and therefore I gave her to your friend. But she has a sister, who is younger and more beautiful than she is. And she may be a wife for you, instead of her.”
Baba yake akasema, “Nilidhani umemchukia, hivyo nikampatia rafiki yako. Dada yake mdogo ni mzuri kuliko yeye, Mchukue badala yake.”
3 And Samson answered him: “From this day, there shall be no guilt for me against the Philistines. For I will do harm to you all.”
Samsoni akawaambia, 'Wakati huu sitakuwa na hatia juu ya Wafilisti wakati nikiwaumiza.'
4 And he went out and caught three hundred foxes. And he joined them tail to tail. And he tied torches between the tails.
Samsoni akaenda na kukamata mbweha mia tatu akawafunga pamoja kila jozi, mkia hadi mkia. Kisha akachukua taa na kuzifunga katikati ya kila mkia.
5 And setting these on fire, he released them, so that they might rush from place to place. And immediately they went into the grain fields of the Philistines, setting these on fire, both the grain that was already bound for carrying, and what was still standing on the stalk. These were completely burned up, so much so that the flame also consumed even the vineyards and the olive groves.
Alipokwisha kuviwasha moto vienge, akawaachia mbweha katika nafaka za Wafilisti zilizosimama, nao wakawasha moto nafaka zote zilizopandwa, na nafaka iliyosimama shambani, pamoja na mashamba ya mizabibu na mizeituni.
6 And the Philistines said, “Who has done this thing?” And it was said: “Samson, the son-in-law of the Timnite, because he took away his wife, and gave her to another. He has done these things.” And the Philistines went up and burned the woman as well as her father.
Wafilisti waliuliza, “Ni nani aliyefanya hili?” Wakaambiwa, “Samsoni, mkwe wa Mtimna alifanya hivyo kwa sababu Mtimna alimchukua mke wa Samsoni akampa rafiki yake.” Basi Wafilisti wakamwendea wakamchoma kwa moto yeye na baba yake.
7 And Samson said to them, “Even though you have done this, I will still fulfill vengeance against you, and then I will be quieted.”
Samsoni akawaambia, “Ikiwa ndivyo mnavyofanya, nitalipiza kisasi juu yenu, na baada ya hayo, nitaacha.”
8 And he struck them with a tremendous slaughter, so much so that, out of astonishment, they laid the calf of the leg upon the thigh. And descending, he lived in a cave of the rock at Etam.
Kisha akawakata vipande vipande, paja na mguu, kwa kuwauwa sana. Kisha akashuka chini akaishi katika pango katika mwamba wa Etamu.
9 And so the Philistines, ascending into the land of Judah, made camp at the place which was later called Lehi, that is, the Jawbone, where their army spread out.
Ndipo Wafilisti wakaja, wakajitahidi kupigana vita huko Yuda, wakaanzisha jeshi lao huko Lehi.
10 And some from the tribe of Judah said to them, “Why have you ascended against us?” And they responded, “We have come to bind Samson, and to repay him for what he has done to us.”
Watu wa Yuda wakasema, “Kwa nini mmekuja kutupiga?” Wakasema, “Tunashambulia ili tuweze kumkamata Samsoni, na tumtendee kama alivyotutendea.”
11 Then three thousand men of Judah descended to the cave of the rock at Etam. And they said to Samson: “Do you not know that the Philistines rule over us? Why would you want to do this?” And he said to them, “As they have done to me, so I have done to them.”
Kisha watu elfu tatu wa Yuda wakashuka hata kwenye pango la Eatamu, wakamwambia Samsoni, “Je, hujui kwamba Wafilisti hutawala juu yetu? Je! umetutendea nini?” Samsoni akawaambia, “Kwa kadili walivyonitendea mimi, vivyo hivyo nimewatendea wao.”
12 And they said to him, “We have come to bind you, and to deliver you into the hands of the Philistines.” And Samson said to them, “Swear and promise to me that you will not kill me.”
Wakamwambia Samsoni, “Tumeshuka kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kwamba hamtaniua ninyi wenyewe.”
13 They said: “We will not kill you. But we will deliver you tied.” And they bound him with two new cords. And they took him from the rock at Etam.
Wakamwambia, “La, tutakufunga tu kwa kamba na kukupeleka kwao. Tunakuahidi sisi hatutakuua.” Kisha wakamfunga na kamba mbili mpya na kumleta kutoka kwenye mwamba.
14 And when he had arrived at the place of the Jawbone, and the Philistines, shouting aloud, had met him, the Spirit of the Lord rushed upon him. And just as flax is usually consumed by a hint of fire, so were the ties with which he was bound broken and released.
Alipofika Lehi, Wafilisti walipiga kelele walipokutana naye. Kisha Roho wa Bwana akaja juu yake kwa nguvu. Kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa kama kitambaa cha kuteketezwa, na zikaanguka mikononi mwake.
15 And finding a jawbone which was laying there, that is, the jawbone of a donkey, snatching it up, he put to death a thousand men with it.
Samsoni alipata mfupa mbichi wa taya ya punda, naye akaichukua na kuua watu elfu kwa mfupa huo.
16 And he said, “With the jawbone of a donkey, with the jaw of the colt of a donkey, I have destroyed them, and I have struck down a thousand men.”
Samsoni akasema, “Kwa taya ya punda, chungu juu ya chungu, na njaa ya punda nimewaua watu elfu.”
17 And when he had completed these words, singing, he threw the jawbone from his hand. And called the name of that place Ramath-Lehi, which is translated as ‘the elevation of the jawbone.’
Samsoni alipomaliza kuzungumza, akatupa taya, na akaita mahali pale Ramath Lehi.
18 And being very thirsty, he cried out to the Lord, and he said: “You have given, to the hand of your servant, this very great salvation and victory. But see that I am dying of thirst, and so I will fall into the hands of the uncircumcised.”
Samsoni alikuwa na kiu sana akamwita Bwana na kusema, “Umempa mtumishi wako ushindi mkubwa. Lakini sasa nitakufa kwa kiu na kuanguka mikononi mwa wale wasiootahiriwa?”
19 And so the Lord opened a large tooth in the jawbone of the donkey, and water went out from it. And having drank it, his spirit was revived, and he recovered his strength. For this reason, the name of that place was called ‘the Spring called forth from the jawbone,’ even to the present day.
Na Mungu akapafungua mahali pa shimo palipo katika Lehi, na maji yakatoka. Alipokunywa, nguvu zake zikarejea na akahuishwa. Kwa hiyo aliita jina la mahali hapo Enhakore, na ni huko Lehi hadi leo.
20 And he judged Israel, in the days of the Philistines, for twenty years.
Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli katika siku za Wafilisti kwa miaka ishirini.

< Judges 15 >