< Joshua 13 >

1 Joshua was old and advanced in age, and the Lord said to him: “You have grown old, and are aged, and a very wide land remains, which has not yet been divided by lot,
Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
2 specifically, all of Galilee, Philistia, and all of Geshur;
Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
3 from the muddy river, which irrigates Egypt, as far as the border of Ekron toward the north, the land of Canaan, which is divided among the rulers of Philistia: the Gazites, and the Ashdodites, the Ashkelonites, the Gathites, and the Ekronites;
(tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
4 truly, to the south are the Hivites, all the land of Canaan, and Mearah of the Sidonians, as far as Aphek and the borders of the Amorite
Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
5 and his confines; also, the region of Lebanon toward the east, from Baalgad, under mount Hermon, until you enter into Hamath;
nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
6 all who live in the mountains from Lebanon, as far as the waters of Misrephoth, and all the Sidonians. I am the One who will wipe them out, before the face of the sons of Israel. Therefore, let their land become a part of the inheritance of Israel, just as I have instructed you.
Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
7 And now, divide the land as a possession to the nine tribes, and to the one half tribe of Manasseh.”
Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
8 With them, Reuben and Gad have possessed the land, which Moses, the servant of the Lord, delivered to them beyond the river Jordan, on the eastern side:
Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
9 from Aroer, which is situated on the bank of the torrent Arnon and in the midst of the valley, and all the plains of Medeba, as far as Dibon;
kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
10 and all the cities of Sihon, the king of the Amorites, who reigned in Heshbon, even to the borders of the sons of Ammon;
miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
11 and Gilead, as well as the borders of Geshur and Maacati, and all of mount Hermon, and all of Bashan, as far as Salecah;
Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
12 the entire kingdom of Og in Bashan, who reigned at Ashtaroth and Edrei, (he was among the last of the Rephaim). And Moses struck and destroyed them.
ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
13 And the sons of Israel were not willing to destroy Geshur and Maacati, and so they have lived in the midst of Israel, even to the present day.
Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
14 But to the tribe of Levi, he did not give a possession. Instead, the sacrifices and victims of the Lord, the God of Israel, these are his inheritance, just as he spoke to him.
Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
15 Therefore, Moses gave a possession to the tribe of the sons of Reuben, according to their families.
Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
16 And their border was from Aroer, which is situated on the bank of the torrent Arnon, and in the midst of the valley of the same torrent, with all the flatlands that lead to Medeba;
Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
17 and Heshbon, and all their villages, which are in the plains; also Dibon, and Bamothbaal, and the town of Baalmeon,
Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
18 and Jahaz, and Kedemoth, and Mephaath,
na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
19 and Kiriathaim, and Sibmah, and Zereth-shahar on the mountain of the steep valley;
na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
20 Bethpeor, and the descending slopes of Pisgah, and Beth-jeshimoth;
Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
21 and all the cities of the plain, and all the kingdoms of Sihon, the king of the Amorites, who reigned at Heshbon, whom Moses struck down with the leaders of Midian: Evi, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba, the commanders of Sihon, inhabitants of the land.
miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
22 And the sons of Israel killed Balaam, the son of Beor, the seer, with the sword, along with the others who were slain.
Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
23 And the river Jordan was made the border of the sons of Reuben; this is the possession of the Reubenites, by their families, in cities and villages.
Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
24 And Moses gave to the tribe of Gad and his sons, by their families, a possession, of which this is the division:
Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 the border of Jazer, and all the cities of Gilead, and one half part of the land of the sons of Ammon, as far as Aroer, which is opposite Rabbah;
Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
26 and from Heshbon as far as Ramath, Mizpeh, and Betonim; and from Mahanaim as far as the borders of Debir;
kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
27 also, in the valley Beth-haram and Beth-nimrah, and Succoth, and Zaphon, the remaining part of the kingdom of Sihon, the king of Heshbon; the limit of this also is the Jordan, as far as the furthest part of the sea of Chinnereth, beyond the Jordan on the eastern side.
Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
28 This is the possession of the sons of Gad, by their families, in their cities and villages.
Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
29 He also gave, to the one half tribe of Manasseh and to his sons, a possession according to their families,
Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
30 the beginning of which is this: from Mahanaim, all of Bashan, and all the kingdoms of Og, the king of Bashan, and all the villages of Jair, which are in Bashan, sixty towns;
Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
31 and one half part of Gilead, and Ashtaroth, and Edrei, the cities of the kingdom of Og in Bashan, to the sons of Machir, the son of Manasseh, to one half part of the sons of Machir, according to their families.
nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
32 Moses divided this possession, in the plains of Moab, beyond the Jordan, opposite Jericho on the eastern side.
Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 But to the tribe of Levi he did not give a possession. For the Lord, the God of Israel, is himself their possession, just as he spoke to him.
Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.

< Joshua 13 >