< Joel 3 >

1 For, behold, in those days and in that time, when I will have converted the captivity of Judah and Jerusalem,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 I will gather all the Gentiles, and will lead them into the valley of Jehoshaphat. And there I will dispute with them over my people, and over Israel, my inheritance, for they have scattered them among the nations and have divided my land.
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 And they have cast lots over my people; and the boy they have placed in the brothel, and the girl they have sold for wine, so that they might drink.
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 Truly, what is there between you and me, Tyre and Sidon and all the distant places of the Philistines? How will you take vengeance on me? And if you were to revenge yourselves against me, I would deliver a repayment to you, quickly and soon, upon your head.
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 For you have carried away my silver and gold. And my desirable and most beautiful, you have taken into your shrines.
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 And you, sons of Judah and sons of Jerusalem, you have sold the sons of the Greeks, so that you might drive them far from their own territory.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Behold, I will raise them up from the place into which you have sold them, and I will turn back your retribution on your own head.
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 And I will sell your sons and your daughters into the hands of the sons of Judah, and they will sell them to the Sabeans, a distant nation, for the Lord has spoken.
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Proclaim this among the Gentiles: “Sanctify a war, raise up the strong. Approach, ascend, all men of war.
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Cut your ploughs into swords and your hoes into spears. Let the weak say, ‘For I am strong.’
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Break out and advance, all nations of the world, and gather together. There the Lord will cause all your strong ones to meet death.”
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 Let them arise and ascend to the valley of Jehoshaphat. For there I will sit, so as to judge all the nations of the world.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Send forth the sickles, because the harvest has matured. Advance and descend, for the press is full, the pressing room is overflowing. For their malice has been increasing.
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 Nations, nations in the valley of being cut to pieces: for the day of the Lord fittingly takes place in the valley of being cut to pieces.
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 The sun and the moon have been darkened, and the stars have withdrawn their splendor.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 And the Lord will roar from Zion and utter his voice from Jerusalem. And the heavens and the earth will be moved. And the Lord will be the hope of his people and the strength of the sons of Israel.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 And you will know that I am the Lord your God, dwelling on Zion, my holy mountain. And Jerusalem will be holy, and strangers will not cross through it anymore.
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 And it will happen, in that day, that the mountains will drip sweetness, and the hills will flow with milk. And the waters will pass through all the rivers of Judah. And a fountain will go forth from the house of the Lord, and it will irrigate the desert of thorns.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 Egypt will be in desolation, and Edom will be a wilderness destroyed, because of what they have unfairly done to the sons of Judah, and because they have shed innocent blood in their land.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 And Judea will be inhabited forever, and Jerusalem for generation upon generation.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 And I will cleanse their blood, which I had not cleansed. And the Lord will remain in Zion.
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”

< Joel 3 >