< Job 10 >

1 My soul is weary of my life. I will release my words against myself. I will speak in the bitterness of my soul.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 I will say to God: Do not be willing to condemn me. Reveal to me why you judge me this way.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 Does it seem good to you, if you find fault with me and oppress me, the work of your own hands, and assist the counsel of the impious?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 Do you have bodily eyes? Or, just as man sees, will you see?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 Are your days just like the days of man, and are your years as the times of humans,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 so that you would inquire about my iniquity and examine my sin?
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 And you know that I have done nothing impious, yet there is no one who can deliver from your hand.
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 Your hands have made me and formed me all around, and, in this way, do you suddenly throw me away?
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Remember, I ask you, that you have fashioned me like clay, and you will reduce me to dust.
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 Have you not extracted me like milk and curdled me like cheese?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 You have clothed me with skin and flesh. You have put me together with bones and nerves.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 You have assigned to me life and mercy, and your visitation has preserved my spirit.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 Though you may conceal this in your heart, yet I know that you remember everything.
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 If I have sinned, and you have spared me for an hour, why do you not endure me to be clean from my iniquity?
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 And if I should be impious, woe to me, and if I should be just, I will not lift up my head, being drenched with affliction and misery.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 And because of pride, you will seize me like a lioness, and having returned, you torment me to an extraordinary degree.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 You renew your testimony against me, and you multiply your wrath against me, and these punishments make war within me.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 Why did you lead me out of the womb? If only I had been consumed, so that no eye would ever see me!
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 I should have been as if I had not been: transferred from the womb to the tomb.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 Will not my few days be completed soon? Release me, therefore, so that I may lament my sorrows a little,
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 before I depart and return no more to a land that is dark and covered with the fog of death,
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 a land of misery and darkness, where the shadow of death, and nothing else but everlasting horror, dwells.
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Job 10 >