< Jeremiah 13 >

1 Thus says the Lord to me: “Go, and obtain for yourself a linen waistcloth. And you shall place it over your loins, and you shall not put it into water.”
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
2 And so I obtained a waistcloth, according to the word of the Lord, and I placed it around my loins.
Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
3 And the word of the Lord came to me a second time, saying:
Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
4 “Take the waistcloth, which you obtained, which is around your loins, and, rising up, go to the Euphrates, and hide it there in an opening of the rock.”
“Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
5 And so I went, and I hid it by the Euphrates, just as the Lord had instructed me.
Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
6 And it happened that, after many days, the Lord said to me: “Rise up, go to the Euphrates, and take from there the waistcloth, which I instructed you to hide there.”
Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
7 And so I went to the Euphrates, and I dug up and took the waistcloth from the place where I had hidden it. And behold, the waistcloth had rotted, so that it was not fit for any use.
Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
8 And the word of the Lord came to me, saying:
Ndipo neno la Bwana likanijia:
9 “Thus says the Lord: In the same way, I will cause the arrogance of Judah and the arrogance of Jerusalem to rot.
“Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
10 This most wicked people, they are not willing to listen to my words, for they walk in the depravity of their own heart, and they have gone after strange gods, so as to serve them and to adore them. And so, they will become like this waistcloth, which is not fit for any use.
Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
11 For just as the waistcloth clings to the loins of a man, so have I brought close to me the entire house of Israel and the entire house of Judah, says the Lord, so that they would be to me: a people, and a name, and a praise, and a glory. But they did not listen.
Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
12 Therefore, you shall speak to them this word: Thus says the Lord, the God of Israel: ‘Every bottle will be filled with wine.’ And they will say to you: ‘Are we ignorant that every bottle will be filled with wine?’
“Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
13 And you shall say to them: Thus says the Lord: Behold, I will fill all the inhabitants of this land, and the kings from the stock of David who sit upon his throne, and the priests, and the prophets, and all the inhabitants of Jerusalem, unto inebriation.
Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
14 And I will scatter them, a man from his brother, and fathers and sons similarly, says the Lord. I will not spare them, and I will not pardon them, and I will not take pity, so as not to destroy them.”
Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
15 Hear and pay close attention. Do not choose to lift yourself up, for the Lord has spoken.
Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
16 Give glory to the Lord your God, before darkness falls, and before your feet stumble on the darkened mountains. You will expect light, but he will turn it into the shadow of death and into utter darkness.
Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
17 But if you will not listen to this, then my soul will weep in secret before the face of your pride. It will weep bitterly, and my eyes will flow with tears, because the flock of the Lord has been taken captive.
Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
18 “Say to the king and to the female ruler: Humble yourselves, sit down. For the crown of your glory has gone down from your head.
Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
19 The cities of the south have been closed, and there is no one who may open them. All of Judah has been taken away into complete captivity.
Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
20 Lift up your eyes and see, you who are arriving from the north. Where is the flock that was given to you, your famous cattle?
Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
21 What will you say when he visits upon you? For you have taught them against you, and you have instructed them with your own head. Will not pains take hold of you, as with a woman in labor?
Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
22 But if you say in your heart, ‘Why have these things happened to me?’ it is because of the greatness of your iniquity that your shame has been uncovered and the soles of your feet have been defiled.
Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
23 If the Ethiopian is able to change his skin, or the leopard is able to change his spots, then you also may be able to do well, though you have learned evil.
Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
24 And I will scatter them like chaff, which is carried away by the wind in the desert.
“Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
25 This is your lot, and this is the portion of your measure from me, says the Lord, because you have forgotten me, and you have had confidence in what is false.
Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
26 Therefore, I have even bared your thighs before your face, and your shame has been seen.
Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
27 For I have seen your adulteries, and your neighing for the wickedness of your fornication, and your abominations upon the hills in the field. Woe to you, Jerusalem! How much longer before you will be made clean after me?”
uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”

< Jeremiah 13 >