< Isaiah 9 >

1 In the earlier time, the land of Zebulun and the land of Naphtali were lifted up. But in the later time, the way of the sea beyond the Jordan, the Galilee of the Gentiles, was weighed down.
Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:
2 The people who walked in darkness have seen a great light. A light has risen for the inhabitants of the region of the shadow of death.
Watu wanaotembea katika giza wameona nuru kuu, wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.
3 You have increased the nation, but you have not increased the rejoicing. They will rejoice before you, like those who rejoice at the harvest, like the victorious exulting after capturing the prey, when they divide the spoils.
Umelikuza taifa, na kuzidisha furaha yao, wanafurahia mbele zako, kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
4 For you have prevailed over the yoke of their burden, and over the rod of their shoulder, and over the scepter of their oppressor, as in the day of Midian.
Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani, umevunja nira iliyowalemea, ile gongo mabegani mwao na fimbo yake yeye aliyewaonea.
5 For every violent plunder with a tumult, and every garment mixed with blood, will be burned up and will become fuel for the fire.
Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani, na kila vazi lililovingirishwa katika damu vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa, vitakuwa kuni za kuwasha moto.
6 For unto us a child is born, and unto us a son is given. And leadership is placed upon his shoulder. And his name shall be called: wonderful Counselor, mighty God, father of the future age, Prince of Peace.
Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
7 His reign will be increased, and there will be no end to his peace. He will sit upon the throne of David and over his kingdom, to confirm and strengthen it, in judgment and justice, from now even unto eternity. The zeal of the Lord of hosts shall accomplish this.
Kuongezeka kwa utawala wake na amani hakutakuwa na mwisho. Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi na juu ya ufalme wake, akiuthibitisha na kuutegemeza kwa haki na kwa adili, tangu wakati huo na hata milele. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utatimiza haya.
8 The Lord sent a word to Jacob, and it fell upon Israel.
Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
9 And all the people of Ephraim will know it. And the inhabitants of Samaria will say it, in the arrogance and haughtiness of their heart:
Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
10 “The bricks have fallen, but we will build with squared stones. They have cut down the sycamores, but we will replace them with cedars.”
“Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
11 And the Lord will raise up the enemies of Rezin over him, and he will turn his adversaries into a tumult:
Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
12 the Syrians from the east and the Philistines from the west. And they will devour Israel with their whole mouth. After all this, his fury was not turned away; instead, his hand was still extended.
Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
13 And the people did not return to the One who struck them, and they did not seek the Lord of hosts.
Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga, wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.
14 And so, the Lord will disperse, away from Israel, the head and the tail, he who bows down and he who refrains, in one day.
Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia, tawi la mtende na tete katika siku moja.
15 The long-lived and honorable, he is the head; and the prophet who teaches lies, he is the tail.
Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa, nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.
16 And those who deceitfully praise this people, and those who are praised, will be thrown down violently.
Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha, nao wale wanaoongozwa wamepotoka.
17 For this reason, the Lord will not rejoice over their youths. And he will not take pity on their orphans and widows. For each one is a hypocrite, and each one is wicked, and every mouth has spoken foolishness. After all this, his fury was not turned away; instead, his hand was still extended.
Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana, wala hatawahurumia yatima na wajane, kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu, na kila kinywa kinanena upotovu. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
18 For impiety has been kindled like a fire: it will devour brier and thorn, and it will burn in the dense forest, and it will be interwoven with the ascending smoke.
Hakika uovu huwaka kama moto; huteketeza michongoma na miiba, huwasha moto vichaka vya msituni, hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.
19 The earth has been shaken by the wrath of the Lord of hosts, and the people will become like fuel for the fire. A man will not spare his own brother.
Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote nchi itachomwa kwa moto, nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto. Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.
20 And he will turn toward the right, and he will be hungry. And he will eat toward the left, and he will not be satisfied. Each one will eat the flesh of his own arm: Manasseh Ephraim, and Ephraim Manasseh, and together they will be against Judah.
Upande wa kuume watakuwa wakitafuna, lakini bado wataona njaa; upande wa kushoto watakuwa wakila, lakini hawatashiba. Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:
21 After all this, his fury was not turned away; instead, his hand was still extended.
Manase atamla Efraimu, naye Efraimu atamla Manase; nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.

< Isaiah 9 >