< Isaiah 46 >

1 Bel has been broken. Nebo has been crushed. Their idols have been placed upon beasts and cattle, your grievous heavy burdens, even unto exhaustion.
Beli huaguka chini, Nebo husujudu; miungu yao imebebwa na wanyama na mzigo wa mnyama. Sanamu hizi mlizobeba ni mzigo mzito kwa wanyama kuchoka.
2 They have been melted down, or have been smashed together. They were not able to save the one who carried them, and their life will go into captivity.
Kwa pamoja wanashuka chini; hawawezi kuziokoa sanamu zao, na wao wenyewe wameenda uhamishoni.
3 Listen to me, house of Jacob, all the remnant of the house of Israel, who are carried in my bosom, who were born from my womb.
Nisikilizeni mimi, nyumba ya Yakobo, wote mliobaki kwenye nyumba ya Israeli mliochukuliwa na mimi kutoka kabla amjazaliwa, mlichukuliwa mkiwa tumboni.
4 Even to your old age, I am the same. And even with your grey hairs, I will carry you. I have made you, and I will sustain you. I will carry you, and I will save you.
Hata kwa njie wazee Mimi ndiye, mpaka mmeshapata mvi nitawachukua. Nimewaumba ninyi na nitawabeba ninyi; Nitwachukua nyie na nitawakomboa nyie.
5 To whom would you liken me, or equate me, or compare me, or consider me to be similar?
Je utanifananisha mimi na nani? na mimi nimefanana na nani, ili utulinganishe?
6 You take gold from a bag, and you weigh silver on a scale, so as to hire a goldsmith to make a god. And they fall prostrate and adore.
Watu humwaga dhahabu kutoka kwenye mabegi yao na uzito wa fedha kwenye uzani. Humuajiri mfua dhahabu, na hutengeneza kuwa dhahabu; na huinama chini na kuzisuju.
7 They carry him on their shoulders, supporting him, and they set him in his place. And he will stand still and will not move from his place. But even when they will cry out to him, he will not hear. He will not save them from tribulation.
Wanazinyanyua juu ya mabega yao na kuzibeba; wanaziweka katika sehemu yake, na itasimama katika eneo lake na alitasogea kutoka pale, hulilia, lakini haiwezi kujibu wala kumuokoa yeyote kwenye matatizo.
8 Remember this, and be confounded. Return, you transgressors, to the heart.
Tafakari kuhusu hivi vitu; katu usivipuuzie, enyi waasi!
9 Remember the past ages. For I am God, and there is no other god. There is no one like me.
Tafakari kuhusu vitu vya awali, nyakati zile zilizopita, Maana mimi ni Mungu, na hakuna mwingine, Mimi ni Mungu na hakuna kama mimi.
10 From the beginning, I announce the last things, and from the start, the things that have not yet been done, saying: My plan will stand firm, and my entire will shall be done.
Mimi ninatangaza mwisho kutoka mwanzo, na kabla ya kitu ambacho hakijatokea; Ninasema, ''Mpango wangu utatokea na nitafanya kama ninavyotamani.''
11 I call a bird from the east, and from a far away land, the man of my will. And I have spoken it, and I will carry it out. I have created, and I will act.
Nitamuita ndege wa mawindo kutoka mashariki, Mtu ambaye ni chaguo langu kutoka nchi ya mbali; Ndio nimesema; na pia nitayatimiza haya, nimekusudia, na pia nitafanya hivyo.
12 Hear me, you who are hard of heart, who are far from justice!
Nisikilize mimi, enyi watu makaidi, ambao mko mbali na kutenda mema.
13 I have brought my justice near. It will not be far away, and my salvation will not be delayed. I will grant salvation in Zion, and my glory in Israel.
Ninaileta haki yangu karibu; na wala sio mbali, na wokovu wangu hausubiri; na nitatoa wokovu wangu kwa Sayuni na uzuri wangu kwa Israeli.

< Isaiah 46 >