< Isaiah 32 >

1 Behold, the king will reign in justice, and the princes will rule in judgment.
Tazama, mfalme atatawala kwa haki, wakuu wataongoza kwa haki.
2 And a man will be like someone hidden from the wind, who conceals himself from a storm, or like rivers of waters in a time of thirst, or like the shadow of a rock that juts out in a desert land.
Kila mmoja atakuwa kama makazi kutoka kwenye upepo na kimbilio kutoka kwenye dhoruba, kama mifereji kwenye sehemu kavu, kama kivuli kwenye mwamba mkubwa katika nchi iliyochoka.
3 The eyes of those who see will not be obscured, and the ears of those who hear will listen closely.
Halafu macho ya waie wanaoona hayataona giza, na masikio ya wale wanosikia yatasikia vizuri.
4 And the heart of the foolish will understand knowledge, and the tongue of those with impaired speech will speak quickly and plainly.
Wenye upele watafikiria kwa makini kwa uelewa wao, na wenye kigugumizi watazungumza dhahiri na kwa urahisi.
5 He who is foolish will no longer be called leader, nor will the deceitful be called greater.
Mjinga hataitwa tena muheshimiwa, wala muongo hataitwa mkuu.
6 For a foolish man speaks foolishness and his heart works iniquity in order to accomplish deception. And he speaks to the Lord deceitfully, so as to empty the soul of the hungry and to take away drink from the thirsty.
Maana mjinga anazungumza ujinga, na moyo wake unapanga maovu na matendo ya wasiomcha Mungu, na anaongea mambo mabaya kuhusu Yahwe. Na anawafanya wenye njaa kuwa tupu na wenye kiu kukosa maji
7 The tools of the deceitful are very wicked. For they have concocted plans to destroy the meek by lying words, though the poor speak judgment.
Njia ya muongo ni maovu. Anajua kubuni mipango mibaya ya kuwalagai masikini kwa uongo, na hata kama masikini atazungumza ukweli.
8 Yet truly, the prince will plan things that are worthy of a prince, and he will stand above the rulers.
Lakini watu wa heshima wanapanga mipango ya kuheshimika; na kwa sabaubau ya matendo ya wenye heshima tuatasimama.
9 You opulent women, rise up and listen to my voice! O confident daughters, play close attention to my eloquence!
Nyanyukeni juu, enyi wanawake mlio wepesi, na sikilizeni sauti yangu; enyi mabinti msiowangalifu, nisikilizeni mimi.
10 For after a year and some days, you who are confident will be disturbed. For the vintage has been completed; the gathering will no longer occur.
Maana kwa mda mfupi zaidi ya mwaka ujasiri wenu utavunjika, nyie wanawake msiojali, maana mavuno ya zabibu yatakwama, mavuno hayatakuwepo.
11 Be stupefied, you opulent women! Be disturbed, O confident ones! Strip yourselves, and be confounded; gird yourselves at the waist.
Tetemekeni, enyi wanawake, mliowadhaifu; taabikeni enyi msikuwa wangalifu; ondoeni nguo zenu nzuri mbaki wazi;
12 Mourn over your breasts, over the delightful country, over the fruitful vineyard.
Vaeni nguo za magunia katika viuno vyenu. Ole watakaojichukulia mashamba mazuri, kwa mzabibu ulio zaa sana.
13 Thorn and brier will rise up, over the soil of my people. How much more over all the houses of gladness, over the city of exultation?
Kwenye aridhi ya watu wangu kutamea miiba na mbigiri, hata juu ya nyumba za furaha na mji ulio na shangwe.
14 For the house has been forsaken. The multitude of the city has been abandoned. A darkness and a covering have been placed over its dens, even unto eternity. It will be the gladness of wild donkeys and the pasture of flocks,
Maana jumba litaachwa, mji uliosongamana utakuwa faragha; kilima na mnara vitakuwa mapango daima, furaha ya punda, malisho ya mifugo;
15 until the Spirit is poured over us from on high. And the desert will be a fruitful field, and the fruitful field will be considered as a forest.
mpaka roho itushukie sisi kutoka juu, na jangwa litakuwa shamba linalozaa, na shamba linalozaa litachukuliwa kama msitu.
16 And judgment will live in solitude, and justice will be seated in a fruitful place.
Wenye haki wataishi jangwani; na wenye haki wataishi katika shamba linalozaa matunda.
17 And the work of justice will be peace. And the service of justice will be quiet and secure, forever.
Kazi ya mwenye haki itakuwa ni ya amani; na matokeo ya wenye haki, ni utulivu na kujiamini daima.
18 And my people will be seated in the beauty of peacefulness, and in the tabernacles of faithfulness, and in the opulence of restfulness.
Watu wangu wataishi katika makao ya amani, na katika nyumba salama na mahali tulivu pa kupumzikia.
19 But hail will be in the descent of the forest, and the city will be brought exceedingly low.
Lakini hata kama ni mvua ya mawe na msitu umeharibiwa, na mji umeteketezwa,
20 Blessed are you who sow over any waters, sending the feet of the ox and the donkey there.
yule ambae anaye panda pembezoni mwa mifereji atabarikiwa, na yule atakaye wapeleka ng'ombe na punda kuchunga.

< Isaiah 32 >