< Isaiah 18 >

1 Woe to the land, that winged cymbal, which is beyond the rivers of Ethiopia,
Ole kwa nchi ya wezi wa mabawa, iliyoko mbali kupitia mito ya Ethiopia;
2 which sends ambassadors by sea and in vessels of papyrus above the waters. Go forth, O swift Angels, to a nation which has been convulsed and torn apart, to a terrible people, after whom there is no other, to a nation apprehensive and downtrodden, whose land the rivers have spoiled.
wanowatuma mabalozi wao kwa kupitia bahari, na vyombo vya majani juu ya maji. Nendeni enyi wajumbe wepesi, kwa watu warefu na laini waishio kwenye nchi, kwa watu wanogopa mbali na karibu, taifa lenye nguvu, wakanyagao watu, ambao mito imegawanya nchi yao.
3 All inhabitants of the world, you who dwell upon the earth: when the sign will have been elevated on the mountains, you will see, and you will hear the blast of the trumpet.
Watu wote wakaao duniani nao wakaao katika nchi, pale ishara itakaponyanyuliwa juu ya milima, angalia; na sikilizeni mbiu itakapopulizwa.
4 For the Lord says this to me: I will be quiet, and I will consider in my place, as the light at midday is clear, and as a cloud of dew in the day of the harvest.
Yahwe asema hivi, ''nitachunguza kimyakimya kutoka nyumbani kwangu, kama kupika joto kwenye jua, na kama ukungu kwenye joto la mavuno.
5 For before the harvest, all was flourishing. And it will spring forth with an untimely completion, and its little branches will be pruned with a curved blade. And what is left over will be cut away and shaken off.
Kabla ya mavuno, pale kipindi cha maua kinapoisha, na maua yako tayari kuwa zabibu. Atakata matawi kwa kupogoa ndoano, na atakatiwa chini na kuchukua matawi yaliyotawanyika.
6 And together they will be abandoned to the birds of the mountains and to the wild beasts of the earth. And the birds will be continuously on them in the summer, and all the wild beasts of the earth will winter over them.
Wataachwa kwa pamoja maana ndege wa milimani na wanyama wa duniani. Ndege watatua kwao majira ya joto, na wanyama wote watakuwa kwao kipindi cha baridi.''
7 In that time, a gift will be carried to the Lord of hosts, from a people divided and torn apart, from a terrible people, after whom there has been no other, from an apprehensive nation, apprehensive and downtrodden, whose land the rivers have ruined, and it will be carried to the place of the name of the Lord of hosts, to mount Zion.
Kwa mda huo kodi italetwa kwa Yahwe wa majeshi kwa watu warefu na laini, kwa watu wanohofia umbali na ukaribu, taifa imara na kukanyagwa chini, ambayo nchi yao imegawanjwa na mito, Kwa sehemu ya jina la Yahwe wa majeshi, mpaka mlima Sayuni.

< Isaiah 18 >