< Genesis 36 >

1 Now these are the generations of Esau, who is Edom.
Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
2 Esau took wives from the daughters of Canaan: Adah the daughter of Elon the Hittite, and Oholibamah the daughter of Anah, the daughter of Zibeon the Hivite,
Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
3 and Basemath, the daughter of Ishmael, sister of Nebaioth.
Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
4 Then Adah bore Eliphaz. Basemath conceived Reuel.
Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
5 Oholibamah conceived Jeush, and Jalam, and Korah. These are the sons of Esau, who were born to him in the land of Canaan.
Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
6 Then Esau took his wives, and sons, and daughters, and every soul of his house, and his substance, and cattle, and whatever he was able to obtain in the land of Canaan, and he went into another region, withdrawing from his brother Jacob.
Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
7 For they were very wealthy and were not able to live together. Neither was the land of their sojourn able to sustain them, because of the multitude of their flocks.
Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
8 And Esau lived at mount Seir: he is Edom.
Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
9 So these are the generations of Esau, the father of Edom, at mount Seir,
Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
10 and these are the names of his sons: Eliphaz the son of Adah, the wife of Esau, likewise Reuel, the son of Basemath, his wife.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
11 And Eliphaz had sons: Teman, Omar, Zepho, and Gatam, and Kenez.
Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
12 Now Timna was the concubine of Eliphaz, the son of Esau. And she bore him Amalek. These are the sons of Adah, the wife of Esau.
Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
13 And the sons of Reuel were Nahath and Zerah, Shammah and Mizzah. These are the sons of Basemath, the wife of Esau.
Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
14 Likewise, these were the sons of Oholibamah, the daughter of Anah, the daughter of Zibeon, the wife of Esau, whom she bore to him: Jeush, and Jalam, and Korah.
Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
15 These were leaders of the sons of Esau, the sons of Eliphaz, the firstborn of Esau: leader Teman, leader Omar, leader Zepho, leader Kenez,
Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
16 leader Korah, leader Gatam, leader Amalek. These are the sons of Eliphaz, in the land of Edom, and these the sons of Adah.
Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
17 Likewise, these are the sons of Reuel, the son of Esau: leader Nahath, leader Zerah, leader Shammah, leader Mizzah. And these were the leaders of Reuel, in the land of Edom. These are the sons of Basemath, the wife of Esau.
Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
18 Now these are the sons of Oholibamah, the wife of Esau: leader Jeush, leader Jalam, leader Korah. These were the leaders of Oholibamah, the daughter of Anah and the wife of Esau.
Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
19 These are the sons of Esau, and these were their leaders: this is Edom.
Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
20 These are the sons of Seir, the Horite, the inhabitants of the land: Lotan, and Shobal, and Zibeon, and Anah,
Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
21 and Dishon, and Ezer, and Dishan. These were the leaders of the Horites, the sons of Seir, in the land of Edom.
Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
22 Now Lotan produced sons: Hori and Heman. But the sister of Lotan was Timna.
Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
23 And these are the sons of Shobal: Alvan, and Manahath, and Ebal, and Shepho, and Onam.
Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
24 And these are the sons of Zibeon: Aiah and Anah. This is the Anah who found the hot springs in the wilderness, when he was pasturing the donkeys of his father Zibeon.
Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
25 And he had a son Dishon, and a daughter Oholibamah.
Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
26 And these are the sons of Dishon: Hemdan, and Esheban, and Ithran, and Cheran.
Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
27 Likewise, these are the sons of Ezer: Bilhan, and Zaavan, and Akan.
Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
28 Then Dishan had sons: Uz and Aran.
Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
29 These were the leaders of the Horites: leader Lotan, leader Shobal, leader Zibeon, leader Anah,
Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
30 leader Dishon, leader Ezer, leader Disan. These were leaders of the Horites who ruled in the land of Seir.
Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
31 Now before the sons of Israel had a king, the kings who ruled in the land of Edom were these:
Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
32 Bela the son of Beor, and the name of his city was Dinhabah.
Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
33 Then Bela died, and Jobab, the son of Zerah from Bozrah, reigned in his place.
Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
34 And when Jobab was dead, Husham of the land of the Temanites reigned in his place.
Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
35 Likewise, this one having died, Hadad the son of Bedad reigned in his place. He struck down Midian in the region of Moab. And the name of his city was Avith.
Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
36 And when Adad was dead, Samlah of Masrekah reigned in his place.
Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
37 Likewise, this one being dead, Shaul of the river Rehoboth, reigned in his place.
Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
38 And when he also had passed away, Baal-hanan, the son of Achbor, succeeded to the kingdom.
Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
39 Likewise, this one being dead, Hadar reigned in his place; and the name of his city was Pau. And his wife was called Mehetabel, the daughter of Matred, daughter of Mezahab.
Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
40 Therefore, these were the names of the leaders of Esau, by their families, and places, and in their vocabulary: leader Timna, leader Alvah, leader Jetheth,
Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
41 leader Oholibamah, leader Elah, leader Pinon,
Oholibama, Ela, Pinoni,
42 leader Kanez, leader Teman, leader Mibzar,
Kenazi, Temani, Mbza,
43 leader Magdiel, leader Iram. These were the leaders of Edom living in the land of their rule: this is Esau, the father of Idumea.
Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.

< Genesis 36 >