< Ezekiel 5 >

1 “And as for you, son of man, obtain for yourself a sharp knife for shaving hair, and you shall take it and draw it across your head and across your beard. And you shall obtain for yourself a balance for weighing, and you shall divide the hair.
“Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
2 A third part you shall burn with fire in the midst of the city, according to the completion of the days of the siege. And you shall take a third part, and you shall cut it with the knife all around. Yet truly, the other third, you shall scatter to the wind, for I will unsheathe the sword after them.
Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
3 And you shall take from there a small number. And you shall bind them in the end of your cloak.
Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
4 And again, you shall take from them, and you shall throw them into the midst of the fire, and you shall burn them with fire. And from it, there shall go forth a fire to the entire house of Israel.”
Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
5 Thus says the Lord God: “This is Jerusalem. I have placed her in the midst of the Gentiles and of the lands all around her.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
6 And she has despised my judgments, so as to be more impious than the Gentiles, and my precepts, more so than the lands that are all around her. For they have cast aside my judgments, and they have not walked in my precepts.”
Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
7 For this reason, thus says the Lord God: “Since you have surpassed the Gentiles who are all around you, and have not walked in my precepts, and have not accomplished my judgments, and have not even acted in accord with the judgments of the Gentiles who are all around you:
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
8 therefore, thus says the Lord God: Behold, I am against you, and I myself will accomplish judgments in your midst, in the sight of the Gentiles.
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
9 And I will do in you what I have not done before, and the likes of which I will not do again, because of all your abominations.
Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
10 Therefore, the fathers shall consume the sons in your midst, and the sons shall consume their fathers. And I will execute judgments in you, and I will winnow your entire remnant in every wind.
Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
11 Therefore, as I myself live says the Lord God, because you have violated my sanctuary with all your offenses and with all your abominations, I also will break into pieces, and my eye will not be lenient, and I will not take pity.
Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
12 One third part of you will die by pestilence or be consumed by famine in your midst. And one third part of you will fall by the sword all around you. Yet truly, one third part of you I will scatter to every wind, and I will unsheathe the sword after them.
Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
13 And I will fulfill my fury, and I will cause my indignation to rest upon them, and I will be consoled. And they shall know that I, the Lord, have spoken in my zeal, when I will have fulfilled my indignation in them.
“Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
14 And I will make you desolate, and a disgrace among the Gentiles, who are all around you, in the sight of all who pass by.
“Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
15 And you shall be a disgrace and a blasphemy, an example and an astonishment, among the Gentiles, who are all around you, when I will have executed judgments in you, in fury and in indignation and with rebukes of wrath.
Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
16 I, the Lord, have spoken. At that time, I will send among them the most grievous arrows of famine, which shall bring death, and which I will send so that I may destroy you. And I will gather a famine over you, and I will crush the staff of bread among you.
Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
17 And I will send among you famine and very harmful beasts, even unto utter ruin. And pestilence and blood shall pass through you. And I will bring the sword over you. I, the Lord, have spoken.”
Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”

< Ezekiel 5 >