< Ezekiel 39 >

1 “But as for you, son of man, prophesy against Gog, and you shall say: Thus says the Lord God: Behold, I am above you, O Gog, prince of the head of Meshech and Tubal.
“Kisha wewe, mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni kinyume nawe, Gogu, mkuu wa Mesheki na Tubali.
2 And I will turn you around, and I will lead you away, and I will cause you to rise up from the parts of the north. And I will bring you over the mountains of Israel.
Nitakugeuza na kukuongoza; nitakupandisha juu kutoka mbali kaskazini na kukuleta hata milima ya Israeli.
3 And I will strike your bow in your left hand, and I will cast away your arrows from your right hand.
Kisha nitaufunga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale kuanguka kutoka kwenye mkono wako wa kuume.
4 You will fall upon the mountains of Israel, you and all your companies, and your peoples who are with you. I have given you over to the wild animals, to the birds, and to every flying thing, and to the beasts of the earth, in order to be devoured.
Utaanguka juu ya milima ya Israeli-wewe na jeshi lako late na maaskari walio pamoja nawe. Nitawapatia ndege mbua na wanyama pori wa mashambani kwa ajili ya chakula.
5 You will fall upon the face of the field. For I have spoken, says the Lord God.
Utaanguka juu ya uso wa shamba, kwa kuwa mimi mwenyewe nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
6 And I will send a fire upon Magog, and upon those who are living confidently in the islands. And they shall know that I am the Lord.
Kisha nitapeleka moto juu ya Magogu na kwa wale waishio salama juu ya pwani, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
7 And I will make known my holy name in the midst of my people, Israel, and my holy name will no longer be defiled. And the Gentiles shall know that I am the Lord, the Holy One of Israel.
Kwa kuwa nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu tena jina langu takatifu litukanwe; mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe, Mtakatifu katika Israeli.
8 Behold, it approaches, and it is done, says the Lord God. This is the day, about which I have spoken.
Tazama! Siku inakuja, na itachukua nafasi-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
9 And the inhabitants from the cities of Israel will go forth, and they will kindle and burn the weapons, the shields and the spears, the bows and the arrows, and the staff and the lance. And they will kindle fires with them for seven years.
Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka nje na watatumia silaha kuwasha moto na kutengeneza moto na kuwachoma-ngao ndogo, ngao kubwa, pinde, mishale, rungu, na mikuki; watatengeneza mioto pamoja nao kwa muda wa siku saba.
10 And they will not carry wood from the countryside, and they will not cut from the forests. For they will kindle the weapons with fire. And they will prey upon those who had preyed upon them, and they will plunder those who had plundered them, says the Lord God.
Hawatakusanya kuni kutoka mashambani wala kukata miti kutoka kwenye misitu, kwa kuwa watazichoma hizo silaha; watawateka nyara wale watakaotaka kuwateka nyara-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
11 And this shall be in that day: I will give Gog a renowned place as a sepulcher in Israel, the valley of the wayfarers to the east of the sea, which will cause astonishment in those who pass by. And in that place, they will bury Gog and all his multitude, and it will be called the valley of the multitude of Gog.
Kisha itakuwa katika hiyo siku ambayo nitaifanya sehemu huko kwa ajili ya Gogu-kaburi la Israeli, bonde kwa ajili ya wale wanaosafiri hata mashariki ya bahari. Litawazuia wale wanaotegemea kupita. Huko watamzika Gogu pamoja na kundi lake lote. Watapaita bonde la Hamon-Gogu.
12 And the house of Israel will bury them, so that they may cleanse the land, for seven months.
Kwa muda wa siku saba nyumba ya Israeli itawazika ili kuitakasa nchi.
13 Then all the people of the earth will bury them, and this shall be for them a renowned day, on which I have been glorified, says the Lord God.
Kwa kuwa watu wa nchi watawazika; itakuwa siku ya kukumbukwa kwao wakati nitakapotukuzwa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
14 And they shall appoint men to continually examine the earth, so that they may seek out and bury those who have remained on the surface of the earth, so that they may cleanse it. Then, after seven months, they will begin to seek.
Kisha watawateua watu kuendelea kwenda kwenye nchi, kuwatafuta wale waliokuwa wakisafiri, lakini waliokufa na miili yao kubaki juu ya uso wa nchi, ili kwamba waweze kuwazika, kwa ajili ya kusafisha nchi. Katika siku ya mwisho ya mwezi wa saba wataanza kutafuta.
15 And they will go around, traveling the earth. And when they will have seen the bone of a man, they will station a marker beside it, until the undertakers may bury it in the valley of the multitude of Gog.
Kama hawa watu wapitao kwenye nchi, watakapoona mfupa wowote wa binadamu, wataweka alama kwa huo, hadi wachimba kaburi watakapokuja na kuizika katika bonde la Hamoni Gogu.
16 And the name of the city will be: the Multitude. And they shall cleanse the earth.
Kutakuwa na mji huko unaitwa Hamona. Wataitakasa nchi kwa njia hii.
17 As for you, then, son of man, thus says the Lord God: Say to every flying thing, and to all the birds, and to all the beasts of the field: Assemble! Hurry! Rush together from every side to my victim, which I have immolated for you, a great victim upon the mountains of Israel, so that you may consume flesh, and drink blood!
Kwako wewe, mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Waambie ndege wote wenye mabawa na wanyama wote wa porini katika mashamba, 'Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kutoka pande zote kwenda kwenye dhabihu yote ambayo mimi mwenyewe ninayoifanya kwa ajili yako, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli, ili kwamba mle nyama na kunywa damu.
18 You shall eat the flesh of the powerful, and you shall drink the blood of the princes of the earth, of rams and lambs and he-goats and bulls, and of fattened birds and all that is fat.
Mtakula nyama ya walio hodari na kunywa damu ya wakuu wa dunia; watakuwa kondoo waume, wana kondoo, mbuzi, na ng'ombe, wote walikuwa wanene katika Basheni.
19 And you shall consume the fat unto satiation, and you shall drink the blood unto inebriation, from the victim that I will immolate for you.
Kisha mtakula mafuta hata kuridhika kwenu; mtakunywa damu hadi kulewa; hii itakuwa dhabihu nitakayoichinja kwa ajili yenu.
20 And you shall be satiated, upon my table, from horses and powerful horsemen, and from all the men of war, says the Lord God.
Mtatosheka kwenye meza yangu pamoja na farasi, magari ya farasi, shujaa, na kila mtu wa vita-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
21 And I will set my glory among the Gentiles. And all the nations shall see my judgment, which I have accomplished, and my hand, which I have laid upon them.
Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao.
22 And the house of Israel shall know that I am the Lord, their God, from that day and thereafter.
Nyumba ya Israeli itajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao kutoka hiyo siku na kuendelea.
23 And the Gentiles shall know that the house of Israel was taken captive because of their own iniquity, because they abandoned me. And so I concealed my face from them, and I delivered them into the hands of their enemies, and they all fell by the sword.
Mataifa yatajua kwamba nyumba ya Israeli wameenda uhamishoni kwa sababu ya udhalimu wao kwa kunisaliti, hivyo naficha uso wangu kwao na kuwaweka kwenye mkono wa maadui zao ili kwamba wote waanguke kwa upanga.
24 I have acted toward them in accord with their uncleanness and wickedness, and so I concealed my face from them.
Nimewafanyia kutokana na uchafu wao na dhambi zao, nitakapokuwa nimeuficha uso wangu kwao.
25 Because of this, thus says the Lord God: Now I will lead back the captivity of Jacob, and I will take pity upon the entire house of Israel. And I will act with zeal on behalf of my holy name.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Sasa nitawarudisha watu wa Yakobo, na kuwa na huruma juu ya nyumba yote ya Israeli, wakati nitakapoona wivu kwa ajili ya jina langu.
26 And they shall bear their shame and all their transgression, by which they betrayed me, though they were living in their own land confidently, dreading no one.
Kisha watabeba aibu yao na uhaini mkubwa walio nihaini. Watayasahau haya yote watakapopumzika katika nchi yao katika usalama, wala hakuna mtu atakaye waogofya.
27 And I will lead them back from among the peoples, and I will gather them together from the lands of their enemies, and I will be sanctified in them, in the sight of the many nations.
Wakati nitakapokuwa nimewarudisha kutoka kwa watu na kuwakusanya kutoka kwenye nchi za maadui zao, nitajionyesha mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi.
28 And they shall know that I am the Lord, their God, because I carried them away to the nations, and I gathered them upon their own land, and I did not abandon any of them there.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe Mungu wao, kwa kuwa nimewapeleka utumwani kati ya mataifa, lakini kisha nitawakusanya kuwarudisha hata nchi yao. Sitamuacha hata mmoja wao kati ya mataifa.
29 And I will no longer conceal my face from them, for I have poured out my Spirit upon the entire house of Israel, says the Lord God.”
Sitawaficha uso wangu kwao wakati nitakapomwaga Roho wangu katika nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 39 >