< Esther 5 >

1 And so, on the third day, Esther had put on her royal apparel and was standing in the atrium of the king’s house, which was inside, opposite the king’s hall, while he was sitting on his throne in the council room of the palace, opposite the entrance of the house.
Baada ya siku tatu, Esta akajivika mavazi yake ya kimalkia na akasimama sehemu ya ndani ya ua wa ikulu ya mfalme, mbele ya nyumba ya mfalme. mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi na akitazama mlango wa kuingilia.
2 And when he saw Esther the queen standing there, she pleased his eyes, and he extended toward her the golden scepter, which he held in his hand, and she approached and kissed the top of his scepter.
Mfalme alipomwona malkia Esta alipata kibali kwa mfalme. Alimpa fimbo ya dhahabu mikononi mwa Esta. Hivyo Esta akamsogelea mfalme na kuishika fimbo ya utawala.
3 And the king said to her, “What do you wish, queen Esther? What is your request? Even if you ask for half of the kingdom, it will be given to you.”
Kisha mfalme akamwambia Malkia Esta, “Unahitaji upewe nini? Ombi lako ni lipi? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
4 But she responded, “If it pleases the king, I beg you to come with me today, and Haman with you, to the feast that I have prepared.”
Malkia Esta akamwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, naomba wewe na Hamani muhudhurie leo katika karamu niliyoiandaa kwa ajili yake.”
5 And immediately the king said, “Call Haman quickly, so that he may obey Esther’s will. And so the king and Haman came to the feast, which the queen had prepared for them.
Mfalme akasema, “Mleteni haraka Hamani sawa sawa na matakwa ya Malkia Esta.” Mfalme pamoja na Hamani wakahuduria katika karamu aliyoandaa malkia Esta.
6 And the king said to her, after he had drunk wine abundantly, “What are you asking for that should be given to you? And which things do you require? Even if you request half of my kingdom, you will obtain it.”
Mvinyo ulipohudumiwa katika karamu, mfalme akamuuliza Malkia Esta hitaji lako ni nini? Na ombi lako ni lipi? Utapewa hata nusu ya ufalme.”
7 Esther answered him, “My petition and prayer is this:
Esta akajibu mfalme, “Hitaji na ombi langu ni hili,
8 If I have found favor in the sight of the king, and if it pleases the king to give me what I ask, and to fulfill my petition, let the king and Haman come to the feast which I have prepared for them, and tomorrow I will open my mind to the king.”
kama ikikupendeza mfalme, kwa kunipa haja yangu na kuheshimu ombi langu, wewe na Hamani muhudhurie tena katika karamu nitakayoiandaa kesho na hapo ndipo nitakapo kuambia haja yangu.
9 And so Haman went out that day joyful and cheerful. And when he saw that Mordecai was sitting in front of the gate of the palace, and that he alone did not get up for him, but did not so much as move from the place where he sat, he was very indignant.
Hamani akaenda nyumbani kwakwe huku akiwa amejawa na furaha moyoni mwake. Lakini alipomwona Modekai katika lango la mfalme, modekai hasimami wala kutetemeka mbele zake, alijawa na ghadhabu kwa ajili ya Modekai.
10 But, concealing his anger and returning into his house, he gathered to him his friends and Zeresh, his wife.
Lakini akajizuia na akaenda nyumbani kwake. Akawaarika marafiki zake wakakusanyika pamoja na Zereshi, mkewe.
11 And he explained to them the greatness of his riches, and the influence of his sons, and how, with such glory, the king had elevated him above all his rulers and servants.
Hamani akawaeleza juu ya utukufu wa mali na idadi ya watoto aliokuwa nao, na vile alivyo juu kuliko wasimamizi na watumishi wote wa mfalme.
12 And after this, he said, “Also, queen Esther has called no one else to the feast with the king, except me. And I will be dining with the king again tomorrow.
Hamani akawambia, “Hata jana Malkia Esta aliandaa karamu kwa ajili ya mfalme na ni mimi tu na mfalme tulio hudhuria katika karamu aliyoiandaa Malkia Esta. Na hata kesho tuna mwaliko mwingine pamoja na mfalme.
13 And though I have all these things, I consider that I have nothing as long as I see Mordecai the Jew sitting in front of the king’s gate.”
Lakini haya yote sio kitu kama Modekai ataendelea kukaa katika lango la mfalme.
14 And Zeresh his wife and his other friends answered him, “Order a great beam to be prepared, having a height of fifty cubits, and in the morning speak to the king, so that Mordecai may be hanged from it, and so you will go joyfully with the king to the feast.” This advice pleased him, and so he ordered a high cross to be prepared.
Kisha Zereshi, mkewe Hamani akamwambia Mmewe na rafiki zake wote, “Andaeni mti wenye urefu wa futi hamsini. Na wakati wa ahsubuhi ongea na mfalme ili Modekai atundikwe katika mti huo. Kisha nenda kwa furaha na mfalme katika karamu aliyoiandaa Malkia.

< Esther 5 >