< Acts 1 >

1 Certainly, O Theophilus, I composed the first discourse about everything that Jesus began to do and to teach,
Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo,
2 instructing the Apostles, whom he had chosen through the Holy Spirit, even until the day on which he was taken up.
hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 He also presented himself alive to them, after his Passion, appearing to them throughout forty days and speaking about the kingdom of God with many elucidations.
Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu.
4 And dining with them, he instructed them that they should not depart from Jerusalem, but that they should wait for the Promise of the Father, “about which you have heard,” he said, “from my own mouth.
Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake.
5 For John, indeed, baptized with water, but you shall be baptized with the Holy Spirit, not many days from now.”
Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
6 Therefore, those who had assembled together questioned him, saying, “Lord, is this the time when you will restore the kingdom of Israel?”
Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”
7 But he said to them: “It is not yours to know the times or the moments, which the Father has set by his own authority.
Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
8 But you shall receive the power of the Holy Spirit, passing over you, and you shall be witnesses for me in Jerusalem, and in all Judea and Samaria, and even to the ends of the earth.”
Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”
9 And when he had said these things, while they were watching, he was lifted up, and a cloud took him from their sight.
Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.
10 And while they were watching him going up to heaven, behold, two men stood near them in white vestments.
Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao,
11 And they said: “Men of Galilee, why do you stand here looking up toward heaven? This Jesus, who has been taken up from you into heaven, shall return in just the same way that you have seen him going up to heaven.”
wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”
12 Then they returned to Jerusalem from the mountain, which is called Olivet, which is next to Jerusalem, within a Sabbath day’s journey.
Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato kutoka mjini.
13 And when they had entered into the cenacle, they ascended to the place where Peter and John, James and Andrew, Philip and Thomas, Bartholomew and Matthew, James of Alphaeus and Simon the Zealot, and Jude of James, were staying.
Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 All these were persevering with one accord in prayer with the women, and with Mary, the mother of Jesus, and with his brothers.
Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.
15 In those days, Peter, rising up in the midst of the brothers, said (now the crowd of men altogether was about one hundred and twenty):
Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema,
16 “Noble brothers, the Scripture must be fulfilled, which the Holy Spirit predicted by the mouth of David about Judas, who was the leader of those who apprehended Jesus.
“Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.
17 He had been numbered among us, and he was chosen by lot for this ministry.
Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”
18 And this man certainly possessed an estate from the wages of iniquity, and so, having been hanged, he burst open in the middle and all his internal organs poured out.
(Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje.
19 And this became known to all the inhabitants of Jerusalem, so that this field was called in their language, Akeldama, that is, ‘Field of Blood.’
Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).
20 For it has been written in the book of Psalms: ‘Let their dwelling place be desolate and may there be no one who dwells within it,’ and ‘Let another take his episcopate.’
“Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi, “‘Mahali pake na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’ na, “‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’
21 Therefore, it is necessary that, out of these men who have been assembling with us throughout the entire time that the Lord Jesus went in and out among us,
Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu,
22 beginning from the baptism of John, until the day when he was taken up from us, one of these be made a witness with us of his Resurrection.”
kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”
23 And they appointed two: Joseph, who was called Barsabbas, who was surnamed Justus, and Matthias.
Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya.
24 And praying, they said: “May you, O Lord, who knows the heart of everyone, reveal which one of these two you have chosen,
Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25 to take a place in this ministry and apostleship, from which Judas prevaricated, so that he might go to his own place.”
ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.”
26 And they cast lots concerning them, and the lot fell upon Matthias. And he was numbered with the eleven Apostles.
Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.

< Acts 1 >