< 2 Kings 23 >

1 And they reported to the king what she had said. And he sent, and all the elders of Judah and Jerusalem were gathered to him.
Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
2 And the king ascended to the temple of the Lord. And with him were all the men of Judah and all who were living in Jerusalem: the priests, and the prophets, and all the people, from the small to the great. And in the hearing of everyone, he read all the words of the book of the covenant, which was found in the house of the Lord.
Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
3 And the king stood upon the step. And he struck a covenant before the Lord, so that they would walk after the Lord, and keep his precepts and testimonies and ceremonies, with all their heart and with all their soul, and so that they would carry out the words of this covenant, which had been written in that book. And the people agreed to the covenant.
Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
4 And the king instructed Hilkiah, the high priest, and the priests of the second order, and the doorkeepers, so that they would cast out of the temple of the Lord all the vessels which had been made for Baal, and for the sacred grove, and for the entire army of heaven. And he burned them outside of Jerusalem, in the steep valley of Kidron. And he carried their dust into Bethel.
Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
5 And he destroyed the soothsayers, whom the kings of Judah had appointed to sacrifice in the high places throughout the cities of Judah, and all around Jerusalem, along with those who were burning incense to Baal, and to the Sun, and to the Moon, and to the twelve signs, and to the entire army of heaven.
Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
6 And he caused the sacred grove to be carried away from the house of the Lord, outside of Jerusalem, to the steep valley of Kidron. And he burned it there, and reduced it to dust. And he cast the dust over the graves of the common people.
Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
7 Also, he destroyed the small places of the effeminate, which were in the house of the Lord, for which the women were weaving something like little houses in the sacred grove.
Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
8 And he gathered together all the priests from the cities of Judah. And he defiled the high places, where the priests were sacrificing, from Geba as far as Beersheba. And he tore down the altars of the gates at the entrance to the gate of Joshua, the leader of the city, which was to the left of the gate of the city.
Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
9 Yet truly, the priests of the high places did not ascend to the altar of the Lord in Jerusalem. For they would only eat from the unleavened bread in the midst of their brothers.
Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
10 Also, he defiled Topheth, which is in the steep valley of the son of Hinnom, so that no one would consecrate his son or his daughter, through fire, to Molech.
Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
11 Also, he took away the horses that the kings of Judah had given to the Sun, at the entrance to the temple of the Lord, beside the hallway of Nathan-melech, the eunuch, who was in Pharurim. And he burned the chariots of the Sun with fire.
Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
12 Also, the altars which were upon the roof of the upper room of Ahaz, which the kings of Judah had made, and the altars which Manasseh had made in the two courts of the temple of the Lord, the king destroyed. And he hurried from there, and he scattered their ashes into the torrent Kidron.
Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
13 Also, the high places which were in Jerusalem, to the right side of the Mount of Offense, which Solomon, the king of Israel, had built to Ashtoreth, the idol of the Sidonians, and to Chemosh, the offense of Moab, and to Milcom, the abomination of the sons of Ammon, the king defiled.
Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
14 And he crushed the statues, and he cut down the sacred groves. And he filled their places with the bones of the dead.
Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
15 Then too, the altar which was in Bethel, and the high place which Jeroboam, the son of Nebat, who caused Israel to sin, had made: both that altar and the high place he tore down, and burned, and reduced to dust. And then he also set fire to the sacred grove.
Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
16 And in that place Josiah, turning, saw the sepulchers which were on the mount. And he sent and took the bones from the sepulchers. And he burned them upon the altar, and he defiled it in accord with the word of the Lord, which was spoken by the man of God, who had predicted these events.
Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
17 And he said, “What is that monument that I see?” And the citizens of that city responded to him: “It is the sepulcher of the man of God, who came from Judah, and who predicted these events, which you have carried out concerning the altar of Bethel.”
Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
18 And he said: “Permit him. Let no one move his bones.” And his bones have remained untouched, with the bones of the prophet who had arrived from Samaria.
Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
19 Then too, all the shrines of the high places, which were in the cities of Samaria, which the kings of Israel had made to provoke the Lord, Josiah took away. And he acted toward them according to all the works that he had done in Bethel.
Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
20 And all the priests of the high places, who were in that place, he killed upon the altars. And he burned the bones of the men upon them. And he returned to Jerusalem.
Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
21 And he instructed all the people, saying: “Keep the Passover to the Lord your God, according to what has been written in the book of this covenant.”
Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
22 Now no similar Passover was kept, from the days of the judges, who judged Israel, and from all the days of the kings of Israel and the kings of Judah,
Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
23 as this Passover, which was kept to the Lord in Jerusalem, in the eighteenth year of king Josiah.
Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
24 Then too, Josiah took away those who divined by spirits, and the soothsayers, and the images of the idols, and the defilements, and the abominations, which had been in the land of Judah and Jerusalem, so that he might establish the words of the law, which were written in the book, which Hilkiah, the priest, found in the temple of the Lord.
Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
25 There was no king before him similar to him, who returned to the Lord with all his heart, and with all his soul, and with all his strength, in accord with the entire law of Moses. And after him, there rose up no one similar to him.
Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
26 Yet truly, the Lord did not turn away from the wrath of his great fury, his fury which was enraged against Judah because of the provocations by which Manasseh had provoked him.
Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
27 And so the Lord said: “And now I will remove Judah from my face, just as I removed Israel. And I will cast aside this city, Jerusalem, which I have chosen, and the house, about which I said: My name shall be there.”
Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
28 Now the rest of the words of Josiah, and all that he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Judah?
Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
29 During his days, Pharaoh Neco, the king of Egypt, ascended against the king of the Assyrians to the river Euphrates. And king Josiah went out to meet him. And when he had seen him, he was killed at Megiddo.
Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
30 And his servants carried him dead from Megiddo. And they took him to Jerusalem, and they buried him in his own sepulcher. And the people of the land took Jehoahaz, the son of Josiah. And they anointed him, and made him king in place of his father.
Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
31 Jehoahaz was twenty-three years old when he had begun to reign, and he reigned for three months in Jerusalem. The name of his mother was Hamutal, the daughter of Jeremiah, from Libnah.
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
32 And he did evil before the Lord, according to all that his fathers had done.
Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
33 And Pharaoh Neco bound him at Riblah, which is in the land of Hamath, so that he would not reign in Jerusalem. And he imposed a penalty on the land: one hundred talents of silver, and one talent of gold.
Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
34 And Pharaoh Neco appointed Eliakim, the son of Josiah, as king in place of Josiah his father. And he changed his name to Jehoiakim. Then he took Jehoahaz away, and he brought him into Egypt, and there he died.
Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
35 Now Jehoiakim gave silver and gold to Pharaoh, when he had taxed the land, according to each one who would contribute by the command of Pharaoh. And he exacted both silver and gold from the people of the land, from each one according to his ability, so that he would give to Pharaoh Neco.
Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
36 Jehoiakim was twenty-five years old when he had begun to reign, and he reigned for eleven years in Jerusalem. The name of his mother was Zebidah, the daughter of Pedaiah, from Rumah.
Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
37 And he did evil before the Lord, in accord with all that his fathers had done.
Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.

< 2 Kings 23 >