< 2 Kings 14 >

1 In the second year of Joash, the son of Jehoahaz, the king of Israel: Amaziah, the son of Jehoash, reigned as king of Judah.
Katika mwaka wa pili wa Yehoashi mwana wa Yehoazi, mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
2 He was twenty-five years old when he had begun to reign. And he reigned for twenty-nine years in Jerusalem. The name of his mother was Jehoaddin from Jerusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tanao wakati alipoanza kutawala; alitawala kwa mda wa miaka ishirini na tisa katika Yerusalemu.
3 And he did what is right before the Lord, yet truly, not like David, his father. He acted in accord with all the things that his father Jehoash did,
Mama yake alikuwa anaitwa Yehoyadani, wa Yerusalemu. Alifanya yale yaliyo mema usoni mwa macho ya Yahwe, sio kama baba yake Daudi. Alifanya kila kitu ambacho Yoashi, baba yake, alichukuwa amekifanya.
4 except for this alone: he did not take away the high places. For still the people were immolating, and burning incense, in the high places.
Lakini sehemu ya juu haikuondolewa. Watu wakaendelea kutoa dhabihu na kufukiza ubani katika sehemu mahala pa juu.
5 And when he had obtained the kingdom, he struck down those of his servants who had killed his father, the king.
Ikawa mara utawala wake ulipokuwa imara, aliwaua watumishi ambao waliokuwa wamemuua baba yake, mfalme.
6 But the sons of those who had been killed he did not put to death, in accord with what was written in the book of the law of Moses, just as the Lord instructed, saying: “The fathers shall not die for the sons, and the sons shall not die for the fathers. Instead, each one shall die for his own sin.”
Ila hakuwaweka watoto wa wale wauaji kwenye kifo; isipokuwa, alifanya kutokana na kile kilichokuwa kimeandikwa kwenye sheria, kwenye kitabu cha Musa, kama Yahwe alivyokuwa ameamuru, akisema, “Wababa wasife kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasife kwa ajili ya makosa ya wazazi wao. Isipokuwa, kila mtu atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
7 He struck down ten thousand men of Idumea, in the Valley of the Salt Pits. And he captured ‘the Rock’ in battle, and he called its name ‘Subdued by God,’ even to the present day.
Aliua maaskari elfu kumi wa Edomi kwenye bonde la chumvi; pia alimchukua Sela kwenye vita na kuiita Yoktheeli, ndivyo paitwavyo hadi leo.
8 Then Amaziah sent messengers to Joash, the son of Jehoahaz, the son of Jehu, the king of Israel, saying: “Come, and let us see one another.”
Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane kila mmoja macho kwa macho kwenye mashinadano.”
9 And Joash, the king of Israel, sent a reply to Amaziah, the king of Judah, saying: “A thistle of Lebanon sent to a cedar, which is in Lebanon, saying: ‘Give your daughter as wife to my son.’ And the beasts of the forest, which are in Lebanon, passed by and trampled the thistle.
Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akawatuma wajumbe kurudi kwa Amazia mfalme wa Yuda, akisema, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma kwa mwerezi katika Lebanuni, kusema, 'Mpatie mwanangu binti yako amuoe; lakini hayawani aliyekuwako Lebanoni akaukanyaga chini ule mbaruti.
10 You have struck and prevailed over Idumea. And your heart has lifted you up. Be content with your own glory, and be seated in your own house. Why would you provoke evil, so that you would fall, and Judah with you?”
Umempiga sana Edomu, na moyo wako umekuinua. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani, kwa nini unataka kujisababishia mataizo na kuanguka, wote wewe na Yuda pamoja nawe?”
11 But Amaziah was not quieted. And so Joash, the king of Israel, went up. And he and Amaziah, the king of Judah, saw one another at Beth-shemesh, a town in Judah.
Lakini Amazia hakutaka kusikia. Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth Shemeshi, ambayo ilikuwa ya Yuda.
12 And Judah was struck down before Israel, and they fled, each to their own tents.
Yuda walishindwa mbele ya Israeli, na kila mtu akakimbia nyumbani.
13 And truly, Joash, the king of Israel, captured Amaziah, the king of Judah, the son of Jehoash, the son of Ahaziah, at Beth-shemesh. And he brought him to Jerusalem. And he breached the wall of Jerusalem, from the gate of Ephraim as far as the gate of the Corner, four hundred cubits.
Yehoashi mfalme wa Israeli, akamchukua Amazia, mfalme wa Yuda mwana wa Yehoashi mwana wa Ahazia, huko Beth Shemeshi. Akaja Yerusalemu na kuuangusha chini ukuta wa Yerusalemu kutoka lango la Efraimu mpaka kwenye pembe ya lango, urefu wa mbali wa dhiraa mia nne.
14 And he took away all the gold and silver, and all the vessels, which were found in the house of the Lord and in the treasuries of the king, and he returned to Samaria with hostages.
Akachukua dhahabu na fedha zote, na vitu vyote ambavyo vilipatikana katika nyumba ya Yahwe, na vitu vya thamani kwenye nyumba ya mfalme, pamoja na mateka pia, na kurudi samaria.
15 But the rest of the words of Joash, which he accomplished, and his strength, with which he fought against Amaziah, the king of Judah, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Yehoashi, yote aliyoyafanya, ushujaa wake, na jinsi alivyopigana na Amazia mfalme wa Yuda, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Israeli?
16 And Joash slept with his fathers, and he was buried in Samaria, with the kings of Israel. And Jeroboam, his son, reigned in his place.
Kisha Yehoashi akalala na wazee wake na ailizikwa katika Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, na Yeroboamu, mwanaye, akawa mfalme katika eneo lake.
17 Now Amaziah, the son of Jehoash, the king of Judah, lived for fifteen years after the death of Joash, the son of Jehoahaz, the king of Israel.
Amazia mwana wa Yoashi, mfalme wa Yuda, akaishi miaka kumi na tano baada ya Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mfalme wa Israeli.
18 And the rest of the words of Amaziah, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Judah?
Kama ilivyo kwa mambo mengine yanayomhusu Amazia, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?
19 And they made a conspiracy against him in Jerusalem. And he fled to Lachish. And they sent after him, to Lachish, and they killed him there.
Wakafanya njama dhidi ya Amazia katika Yerusalimu, akakimbilia Lakishi. Akakimbia hadi Lakishi, lakini wakawatuma watu kumfuata hadi Lakishi na kumuua huko.
20 And they carried him away on horses. And he was buried in Jerusalem with his fathers, in the city of David.
Wakamrudisha kwa farasi, na alizikwa pamoja na wazee wake katika mji wa Saudi.
21 Then all the people of Judah took Azariah, at sixteen years from birth, and they appointed him as king in place of his father, Amaziah.
Watu wote wa Yuda wakamchukua Uzaria, ambaye alikuwa na umri wa miaka kumi na minne, na walimfanya kuwa mfalme katika nyumba ya kifalme wa baba yake Uzaria.
22 He built up Elath, and he restored it to Judah, after which the king slept with his fathers.
Alikuwa Uzaria ambaye alijenga Elathi na kuirudisha kwa Yuda, baada ya mfalme Uzaria akalala pamoja na mababu zake.
23 In the fifteenth year of Amaziah, the son of Jehoash, the king of Judah: Jeroboam, the son of Joash, the king of Israel, reigned, in Samaria, for forty-one years.
Katika mwaka wa kumi na tano wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala katika Samaria; alitawala kwa muda wa miaka arobaini na moja.
24 And he did what is evil before the Lord. He did not withdraw from all the sins of Jeroboam, the son of Nebat, who caused Israel to sin.
Akafanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Hakuziacha dhambi zake za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye aliisababisha Israeli kuasi.
25 He restored the borders of Israel, from the entrance of Hamath as far as the Sea of the Wilderness, in accord with the word of the Lord, the God of Israel, which he spoke through his servant, the prophet Jonah, the son of Amittai, who was from Gath, which is in Hepher.
Akairudisha mipaka ya Israeli kutoka Lebo Hamathi mpaka kwenye Bahari ya Araba, kufuata amri ya neno la Yahwe, Mungu wa Israeli, ambalo aliongea kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, yule nabii, ambaye alitokea Gathi Heferi.
26 For the Lord saw the exceedingly bitter affliction of Israel, and that they were being consumed, even to those who were enclosed in prison, and even to the least ones, and that there was no one who would help Israel.
Kwa kuwa Yahwe aliyaona mateso ya Israeli, ambayo yalikuwa makali kwa kila mmoja, wote mtumwa na asyemtumwa, na kwamba hapakuwa na ulinzi kwa ajili ya Israeli.
27 But the Lord did not say that he would wipe away the name of Israel from under heaven. So instead, he saved them by the hand of Jeroboam, the son of Joash.
Basi Yahwe akasema kwamba hatoweza kulifuta jina la Israeli chini ya mbingu; badala yake, aliwaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
28 But the rest of the words of Jeroboam, and all that he did, and his strength, with which he went to battle, and the manner in which he restored Damascus and Hamath to Judah, in Israel, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Yeroboamu, yote aliyoyafanya, ushujaa wake, jinsi alivyo pigana vita na kuipata tena Damaskasi na Hamathi, ambayo ilikuwa ya Yuda, kwa Israeli, je hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
29 And Jeroboam slept with his fathers, the kings of Israel. And Zechariah, his son, reigned in his place.
Yeroboamu akalala na mababu zake, pamoja na mfalme wa Israeli, na Zekaria mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.

< 2 Kings 14 >