< 2 Chronicles 22 >

1 Then the inhabitants of Jerusalem appointed his youngest son, Ahaziah, as king in his place. For the robbers of the Arabians, who had fallen upon the camp, had put to death all those who were greater by birth before him. And so Ahaziah, the son of Jehoram, reigned as king of Judah.
Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
2 Ahaziah was forty-two years old when he had begun to reign, and he reigned for one year in Jerusalem. And the name of his mother was Athaliah, the daughter of Omri.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
3 But he too went forth in the ways of the house of Ahab. For his mother impelled him to act impiously.
Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
4 And so he did evil in the sight of the Lord, just as the house of Ahab did. For after the death of his father, they were counselors to him, to his destruction.
Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
5 And he walked in their counsels. And he went with Joram, the son of Ahab, the king of Israel, to war against Hazael, the king of Syria, at Ramoth Gilead. And the Syrians wounded Joram.
Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
6 And he returned, so that he might be cured at Jezreel. For he had received many wounds in the above-stated battle. And so Ahaziah, the son of Jehoram, the king of Judah, descended, so that he might visit Joram, the son of Ahab, at Jezreel, while he was ill.
Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
7 Indeed, it was the will of God against Ahaziah that he would go to Joram, and when he had gone, that he also would go out with him against Jehu, the son of Nimshi, whom the Lord had anointed to destroy the house of Ahab.
Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
8 Therefore, when Jehu was overthrowing the house of Ahab, he found the leaders of Judah, with the sons of the brothers of Ahaziah, who were ministering to him, and he put them to death.
Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
9 Also, while he himself was seeking Ahaziah, he found him to be hiding in Samaria. And having been led to him, he killed him. And they buried him, because he was the son of Jehoshaphat, who had sought the Lord with all his heart. But there was no longer any hope that someone from the stock of Ahaziah would reign.
Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
10 For indeed, his mother, Athaliah, seeing that her son had died, rose up and killed the entire royal stock of the house of Jehoram.
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
11 But Jehosheba, the daughter of the king, took Joash, the son of Ahaziah, and stole him from the midst the king’s sons when they were being slain. And she hid him with his nurse in a bedroom. Now Jehosheba, the one who had hidden him, was the daughter of king Jehoram, and the wife of the high priest Jehoiada, and the sister of Ahaziah. And because of this, Athaliah did not kill him.
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
12 Therefore, he was with them, hidden in the house of God, for six years, while Athaliah reigned over the land.
Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

< 2 Chronicles 22 >