< 1 Samuel 9 >

1 Now there was a man of Benjamin, whose name was Kish, the son of Abiel, the son of Zeror, the son of Becorath, the son of Aphiah, the son of a man of Benjamin, strong and robust.
Basi kulikuwa na mtu mmoja kutoka Benyamini, mtu mashuhuri. Jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini.
2 And he had a son called Saul, an elect and good man. And there was not a man among the sons of Israel better than he was. For he stood head and shoulders above all the people.
Huyu alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Sauli, kijana mzuri wa uso. Hapakuwapo mwanaume mzuri wa uso kuliko huyu miongoni mwa watu wote wa Israeli. Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine.
3 Now the donkeys of Kish, the father of Saul, had become lost. And Kish said to his son Saul, “Take with you one of the servants, and rising up, go out and seek the donkeys.” And when they had passed through mount Ephraim,
Na punda wa Kishi, baba yake na Sauli walipotea. hivyo Kishi akamwambia Sauli mwanawe, “Mchukue mmoja wa watumishi; uamke uende kuwatafuta punda,”
4 and through the land of Shalishah, and had not found them, they crossed also through the land of Shaalim, and they were not there, and through the land of Benjamin, and they found nothing.
Sauli akapita katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu na akaenda akapita katika nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona. Kisha walipita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Baadaye alipita katika nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwaona wale punda.
5 And when they had arrived in the land of Zuph, Saul said to the servant who was with him, “Come, and let us return, otherwise perhaps my father may forget the donkeys, and become anxious over us.”
Na walipofika nchi ya Sufu, Sauli alimwambia mtumishi wake aliyekuwa naye, “Njoo na turudi, pengine baba aweza kuacha kuchunga punda na kuanza kutuhofia sisi.”
6 And he said to him: “Behold, there is a man of God in this city, a noble man. All that he says, happens without fail. Now therefore, let us go there. For perhaps he may tell us about our way, because of which we have arrived.”
Lakini mtumishi akamwmbia, “Sikiliza, Yupo mtu wa Mungu katika mji huu. Naye ni mtu wa kuheshimiwa sana; kila asemalo huwa kweli. Hebu twende huko; labda anaweza kutuambia tupitie wapi katika safari yetu.”
7 And Saul said to his servant: “Behold, let us go. But what will we bring to the man of God? The bread in our sacks has run out. And we have no small gift that we might give to the man of God, nor anything at all.”
Ndipo Sauli akamwambia mtumish iwake, “Lakini kama tukienda kwake, twaweza kumpelekea nini? Maana hata mkate katika mfuko wetu umekwisha, na hakuna zawadi ya kumpelekea mtumishi wa Mungu. Tuna kitu gani?
8 The servant again responded to Saul, and he said: “Behold, there is found in my hand a coin of the fourth part of a stater. Let us give it to the man of God, so that he may reveal to us our way.”
Huyo mtumishi akamjibu Sauli na kusema, “Hapa, ninayo robo ya shekeli ya fedha ambayo nitampa mtumishi wa Mungu, atuambie ni njia ipi yatupasa tuiendee.”
9 (In past times, in Israel, anyone going to consult God would speak in this way, “Come, and let us go to the seer.” For one who is called a prophet today, in past times was called a seer.)
(Zamani katika Israeli, mtu alipotaka kujua neno kuhusu mapenzi ya Mungu, alisema, “Njoo, haya twende kwa mwonaji.” Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji).
10 And Saul said to his servant: “Your word is very good. Come, let us go.” And they went into the city, where the man of God was.
Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, “Umesema vyema. Haya, njoo twende.” Basi wakaenda katika mji ambao mtu wa Mungu alikuwamo.
11 And as they were ascending the slope to the city, they found some young women going out to draw water. And they said to them, “Is the seer here?”
Walipopanda mlima kuelekea mjini, walikutana na wasichana wakienda kuteka maji; Sauli na mtumishi wake wakawauliza, “Mwonaji hupo hapa?”
12 And responding, they said to them: “He is. Behold, he is ahead of you. Hurry now. For he came into the city today, since there is a sacrifice for the people today, on the high place.
Nao wakawajibu, na kusema, “Yupo; tazameni, yuko mbele yenu. Harakisheni, kwa maana anakuja mjini leo, sababu leo watu wanatoa dhabihu zao mahali pa juu.
13 Upon entering the city, you should find him immediately, before he ascends to the high place for the meal. And the people will not eat until he has arrived. For he blesses the victim, and thereafter those who were called will eat. Now therefore, go up. For you will find him today.”
Mara tu mtakapoingia mjini mtamuona, kabla hajapanda mahali pa juu kla chakula. Watu hawatakula hata atakapokuja, kwa sababu ndiye ataibariki dhabihu; na baadaye wale ambao wamealikwa hula. Basi pandeni, mtamuona sasa hivi.”
14 And they ascended into the city. And as they were walking in the midst of the city, Samuel appeared, advancing to meet them, so that he might ascend to the high place.
Kwa hiyo walikwea kwenda mjini. Walipokuwa wakiingia mjini, walimuona Samweli akija mbele yao, akipanda kwenda mahali pa juu.
15 Now the Lord had revealed to the ear of Samuel, one day before Saul had arrived, saying:
Siku moja kabla Sauli hajafika, BWANA alikuwa amemfunulia Samweli:
16 “Tomorrow, at the same hour that it is now, I will send to you a man from the land of Benjamin. And you shall anoint him to be the leader over my people Israel. And he will save my people from the hand of the Philistines. For I have looked with favor upon my people, because their outcry has reached me.”
“Kesho wakati kama huu nitakutumia mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe utamtia mafuta awe mfalme juu ya watu wangu Israeli. Atawaokoa watu wangu kutoka mkono wa Wafilisti. Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu na kilio cha kutaka msaada kimenifikia.”
17 And when Samuel had caught sight of Saul, the Lord said to him: “Behold, the man about whom I spoke to you. This one shall rule over my people.”
Samweli alipomuona Sauli, BWANA akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekwambia habari zake! Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
18 Then Saul drew near to Samuel, at the middle of the gate, and he said, “Tell me, I beg you: where is the house of the seer?”
Ndipo Sauli akaja karibu na Samweli katika lango na kusema, “Niambie nyumba ya Mwonaji iko wapi?
19 And Samuel responded to Saul, saying: “I am the seer. Ascend before me to the high place, so that you may eat with me today. And I will send you away in the morning. And I shall reveal to you everything that is in your heart.
Samweli akamjibu Sauli akisema, “Mimi ndiye mwonaji. Tangulia mbele hadi mahali pa juu, nami nitakueleza kila kitu kilichomoyoni mwako.
20 And concerning the donkeys, which were lost the day before yesterday, you should not be anxious, for they have been found. And all the best things of Israel, for whom should they be? Will they not be for you and for all your father’s house?”
Kama punda wenu waliopotea siku tatu zilizopita, msihofu kuhusu hao punda, kwa kuwa wamekwishapatikana. Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?”
21 And responding, Saul said: “Am I not a son of Benjamin, the least tribe of Israel, and are not my kindred the last among all the families from the tribe of Benjamin? So then, why would you speak this word to me?”
Sauli akamjibu na kusema, Siyo mimi Mbenyamini, kutoka kabila lililo dogo sana kwa makabila ya Israeli? Siyo ukoo wangu ulio mdogo sana kwa kabila la Benyamini? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?”
22 And so Samuel, taking Saul and his servant, brought them into the dining room, and he gave them a place at the head of those who had been invited. For there were about thirty men.
Hivyo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaingiza ukumbini, akawakalisha mahali pa heshima pa wale walioalikwa, idadi yao takribani watu thelathini.
23 And Samuel said to the cook, “Present the portion that I gave to you, and which I instructed you to set apart beside you.”
Samweli akamwambia mpishi, “Lete sehemu niliyokupatia, sehemu ambayo nilikwambia hivi, “Itenge.”'
24 Then the cook lifted up the shoulder, and he placed it before Saul. And Samuel said: “Behold, what remains, set it before you and eat. For it was preserved for you intentionally, when I called the people.” And Saul ate with Samuel on that day.
Basi mpishi alichukua paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu na kile kilichokuwa pamoja nalo, akaitenga mbele ya Sauli. Kisha Samweli akasema, “Angalia kile kilichokuwa kimetunzwa kwa ajili yako! Kula, kwa sababu kilitunzwa hadi wakati maalum ufike kwa ajili yako. Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.”' Kwa hiyo Sauli alikula pamoja na Samweli siku hiyo.
25 And they descended from the high place into the town, and he spoke with Saul in the upper room. And he set out a bed for Saul in the upper room, and he slept.
Walipokuwa wamekwisha shuka chini kutoka sehemu ya juu na kuingia mjini, Samweli akazungumza na Sauli darini.
26 And when they had risen in the morning, and it now began to be light, Samuel called to Saul in the upper room, saying, “Rise up, so that I may send you on.” And Saul rose up. And they both departed, that is to say, he and Samuel.
Na kulipopambazuka, Samweli alimwita Sauli darini na kusema, “Amka, kusudi nikusindikize uende zako,” Hivyo Sauli aliamka, na wote wawili, yeye na Samweli walitoka kwenda mtaani.
27 And as they were descending to the very limit of the city, Samuel said to Saul: “Tell the servant to go ahead of us, and to continue on. But as for you, stay here a little while, so that I may reveal the word of the Lord to you.”
Walipokuwa wakienda nje ya viunga vya mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi wako atanguliye mbele yetu(na alitangulia mbele), Lakini wewe sharti usubiri kidogo, nipate kukuambia ujumbe wa Mungu.”

< 1 Samuel 9 >