< 1 Samuel 23 >

1 And they reported to David, saying, “Behold, the Philistines are fighting against Keilah, and they are plundering the grain stores.”
Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
2 Therefore, David consulted the Lord, saying, “Shall I go and strike down these Philistines?” And the Lord said to David, “Go, and you shall strike down the Philistines, and you shall save Keilah.”
akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
3 And the men who were with David said to him, “Behold, we continue in fear here in Judea; how much more so, if we go into Keilah against the troops of the Philistines?”
Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
4 Therefore, David consulted the Lord again. And responding, he said to him: “Rise up, and go into Keilah. For I will deliver the Philistines into your hand.”
Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
5 Therefore, David and his men went into Keilah. And they fought against the Philistines, and they took away their cattle, and they struck them with a great slaughter. And David saved the inhabitants of Keilah.
Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
6 And in that time, when Abiathar, the son of Ahimelech, was in exile with David, he had descended to Keilah, having an ephod with him.
(Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
7 Then it was reported to Saul that David had gone to Keilah. And Saul said: “The Lord has delivered him into my hands. For he is enclosed, having entered into a city which has gates and bars.”
Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
8 And Saul instructed all the people to descend in order to fight against Keilah, and to besiege David and his men.
Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
9 And when David had realized that Saul had secretly prepared evil against him, he said to Abiathar, the priest, “Bring the ephod.”
Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
10 And David said: “O Lord God of Israel, your servant has heard a report that Saul is planning to go to Keilah, so that he may overturn the city because of me.
Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
11 Will the men of Keilah deliver me into his hands? And will Saul descend, just as your servant has heard? O Lord God of Israel, reveal to your servant.” And the Lord said, “He will descend.”
Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
12 And David said, “Will the men of Keilah deliver me, and the men who are with me, into the hands of Saul?” And the Lord said, “They will deliver you.”
Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
13 Therefore, David, and his men of about six hundred, rose up, and, departing from Keilah, they wandered here and there, aimlessly. And it was reported to Saul that David had fled from Keilah, and was saved. For this reason, he chose not to go out.
Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
14 Then David stayed in the desert, in very strong places. And he stayed on a mount in the wilderness of Ziph, on a shady mount. Nevertheless, Saul was seeking him every day. But the Lord did not deliver him into his hands.
Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
15 And David saw that Saul had gone out, so that he might seek his life. Now David was in the desert of Ziph, in the woods.
Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
16 And Jonathan, the son of Saul, rose up and went to David in the woods, and he strengthened his hands in God. And he said to him:
Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
17 “Do not be afraid. For the hand of my father, Saul, will not find you. And you shall reign over Israel. And I will be second to you. And even my father knows this.”
Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
18 Therefore, they both struck a pact before the Lord. And David stayed in the woods. But Jonathan returned to his house.
Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
19 Then the Ziphites ascended to Saul at Gibeah, saying: “Behold, is not David hidden with us in very secure places in the woods on the hill of Hachilah, which is to the right of the desert?
Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
20 Now therefore, if your soul has desired to descend, then descend. Then it will be for us to deliver him into the hands of the king.”
Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
21 And Saul said: “You have been blessed by the Lord. For you have grieved for my situation.
Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
22 Therefore, I beg you, go forth, and prepare diligently, and act carefully. And consider the place where his foot may be, and who may have seen him there. For he thinks, concerning me, that I craftily plan treachery against him.
Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
23 Consider and seek out all his hiding places, in which he may be concealed. And return to me with certainty about the matter, so that I may go with you. But if he would even press himself into the earth, I will search him out, amid all the thousands of Judah.”
Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
24 And rising up, they went to Ziph before Saul. But David and his men were in the desert of Maon, in the plain to the right of Jeshimon.
Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
25 Then Saul and his allies went to seek him. And this was reported to David. And immediately, he descended to the rock, and he moved about in the desert of Maon. And when Saul had heard of it, he pursued David in the desert of Maon.
Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
26 And Saul went to one side of the mountain. But David and his men were on the other side of the mountain. Then David was despairing that he would be able to escape from the face of Saul. And Saul and his men enclosed David and his men in the manner of a crown, so that they might capture them.
Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
27 And a messenger came to Saul, saying, “Hurry and come, because the Philistines have poured themselves out upon the land.”
mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
28 Therefore, Saul turned back, ceasing in the pursuit of David, and he traveled to meet the Philistines. For this reason, they called that place, the Rock of Division.
Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
29 Then David ascended from there, and he lived in very secure places in Engedi.
Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.

< 1 Samuel 23 >