< 1 Kings 11 >

1 But king Solomon loved many foreign women, including the daughter of Pharaoh, and women of Moab, and of Ammon, and of Idumea, and of Sidon, and of the Hittites.
Basi mfalme Sulemani aliwapenda wanawake wengi wa kigeni: binti wa Farao na wanawake wa Wamoabu, Waamori, Waedomu, Wasidoni, na Wahiti - Haya na
2 These were of the nations about whom the Lord said to the sons of Israel: “You shall not enter to them, and none of them shall enter to anyone of yours. For they will most certainly turn aside your hearts, so that you follow their gods.” And yet, to these Solomon was joined with a greatly enflamed love.
mataifa ambayo BWANA alikuwa amewaambia Waisraeli kwamba, “Msiwaoe, wala binti zenu kuolewa nao, kwani kwa hakika wataigeuza mioyo yenu ili mfuate miungu yao.” Lakini Sulemani aliwapenda wanawake hao.
3 And for him, there were seven hundred wives, as if they were queens, and three hundred concubines. And the women turned aside his heart.
Sulemani alikuwa na wanawake halali mia saba na masuria mia tatu. Wake zake waliugeuza moyo wake.
4 And when now he was old, his heart was perverted by the women, so that he followed strange gods. And his heart was not perfect with the Lord his God, as was the heart of his father David.
Kwa kuwa Sulemani alipozeeka, wake zake waliugeuza moyo wake kwa miungu mingine; hakuutoa moyo wake wote kwa BWANA, Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 For Solomon worshipped Ashtoreth, the goddess of the Sidonians, and Milcom, the idol of the Ammonites.
Kwani Sulemani alimfuata Ashtoreth, mungu mke wa Wasidoni, na alimfuata Milkom, ambayo ni sanamu chukizo ya Waamori.
6 And Solomon did what was not pleasing in the sight of the Lord. And he did not continue to follow the Lord, as his father David did.
Sulemani akafanya maovu mbele ya BWANA; hakumfuata BWANA kwa moyo wake wote, kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 Then Solomon built a shrine for Chemosh, the idol of Moab, on the mount that is opposite Jerusalem, and for Milcom, the idol of the sons of Ammon.
Kisha Sulemani akajenga mahali pa juu pa Kemoshi, ambayo ni sanamu chukizo ya Wamoabu, mashariki mwa Yerusalemu juu ya kilima, na vivyo hivyo na Moleki, Sanamu chukizo ya Waamoni.
8 And he acted in this manner for all his foreign wives, who were burning incense and immolating to their gods.
Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa sadaka kwa miungu yao.
9 And so, the Lord became angry with Solomon, because his mind had been turned away from the Lord, the God of Israel, who had appeared to him twice,
BWANA alichukizwa na Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umemwacha Mungu wa Israeli, ingawa alikuwa amejionyesha kwake mara mbili
10 and who had instructed him about this matter, lest he follow strange gods. But he did not observe what the Lord commanded to him.
na kumwamuru juu ya mambo haya, kwamba asiwaendee miungu wengine. Bali Sulemani hakutii kile ambacho BWANA alikuwa amemwamuru.
11 And so, the Lord said to Solomon: “Because you have this with you, and because you have not kept my covenant and my precepts, which I commanded to you, I will tear apart your kingdom, and I will give it to your servant.
Kwa hiyo BWANA akamwambia Sulemani, “Kwa kuwa umeyafanya haya haukulishika agano langu na maagizo ambayo nilikuamuru, basi nitaugawa ufalme kutoka kwako na kuwapatia watumishi wako.
12 Yet truly, I will not do it in your days, for the sake of your father David. From the hand of your son, I will tear it away.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, sitalifanya hilo wakati wa uhai wako, bali nitaugawa wakati ukiwa chini ya mwanao.
13 Neither will I take away the whole kingdom. Instead, I will grant one tribe to your son, for the sake of David, my servant, and Jerusalem, which I have chosen.”
Bado sitaugawanya ufalme wote; Nitampa mwanao kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu, ambayo nimeichagua.”
14 Then the Lord raised up an adversary to Solomon, Hadad of Idumea, from an offspring of the king who was in Idumea.
Kisha BWANA akamwinulia uadui Sulemani, Hadadi Mwedomu. Alikuwa anatoka kwenye familiia ya mfalme wa Edomu.
15 For when David was in Idumea, Joab, the leader of the military, had ascended to bury those who had been killed, and he had killed every male in Idumea.
Daudi alipokuwa Edomu, Yoabu mkuu wa jeshi alikuwa ameenda kuzika mfu, kila mtu aliyekuwa ameuawa kule Edomu.
16 And Joab remained in that place for six months, with all of Israel, until he had put to death every male in Idumea.
Yoabu na Israeli yote walibaki huko kwa miezi sita mpaka alipokuwa amewaua wanaume wote wa Edomu.
17 Then Hadad fled, he and some men of Idumea from among the servants of his father with him, so that he might enter into Egypt. But Hadad was then a little boy.
Lakini Hadadi alichulukuliwa na Waedomu wengine na watumishi wa baba yake hadi Misri, kuanzia Hadadi alipokuwa mtoto mdogo.
18 And when they had risen up from Midian, they went into Paran, and they took with them some men from Paran. And they went into Egypt, to Pharaoh, the king of Egypt. And he gave him a house, and he appointed food for him, and he assigned land to him.
Waliondoka Midiani wakaja Parani, ambapo walichukuliwa na wanaume mpaka Misri, kwa Farao wa Misri, ambaye alimpa nyumba na ardhi yenye chakula.
19 And Hadad found great favor before Pharaoh, so much so that he gave to him as wife, the sister of his own wife, queen Tahpenes.
Hadadi alipata neema kubwa machoni pa Farao, kwa hiyoFarao akampatia mke, umbu wa mke wake mwenyewe, umbu la Tapenesi aliyekuwa Malkia.
20 And the sister of Tahpenes bore to him a son, Genubath. And Tahpenes raised him in the house of Pharaoh. And Genubath was living with Pharaoh and his sons.
Naye huyo umbu la Tapenesi alimzalia Hadadi mwana. Wakamwita jina lake Genubathi. Tapenesi akamlea katika ikulu ya Farao. Kwa hiyo Genubathi alikulia kwenye ikulu ya Farao pamoja na watoto wa Farao.
21 And when Hadad had heard in Egypt that David had slept with his fathers, and that Joab, the leader of the military, had died, he said to Pharaoh, “Release me, so that I may go to my own land.”
Naye alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kuwa Daudi alishalala na mababu zake na kwamba Yoabu mkuu wa majeshi alishakufa, Hadadi akamwambia Farao, “Acha niondoke nirudi nchini kwangu.”
22 And Pharaoh said to him, “But what is lacking to you with me, so that you would seek to go to your own land?” But he responded: “Nothing. Yet I beg you that you may release me.”
Lakini Farao alimwambia, “Umepungukiwa nini kwangu, kwamba sasa unatafuta kurudi nchini kwako?” Naye Hadadi akamjibu, “Hapana kitu lakini tafadhali niache niende.”
23 Also, God raised up against him an adversary, Rezon, the son of Eliada, who had fled from his lord, Hadad-Ezer, the king of Zobah.
Pia Mungu akamwinulia Sulemani adui mwingine, Rezoni mwana wa Eliada, aliyekuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri mfalme wa Soba.
24 And he gathered together men against him. And when David put those of Zobah to death, he became a leader of robbers. And they went away to Damascus, and they lived there. And they appointed him to be king of Damascus.
Rezoni alijikusanyia wanaume naye akawa mkuu wa jeshi dogo, Daudi ali owapiga wanaume wa Soba. Wale wanume Rezoni walienda Dameski kuishi huko, na Rezoni aliitawala Dameski.
25 And he was an adversary to Israel during all the days of Solomon. And such is the evil of Hadad and of his hatred against Israel. And he reigned in Syria.
Yeye akawa adui wa Israeli katika siku zote za mfalme Sulemani, zaidi ya madhara ambayo Hadadi alisababisha. Rezoni akawachukia Israeli na akawa juu ya Shamu
26 Also, there was Jeroboam, the son of Nebat, an Ephraimite from Zeredah, a servant of Solomon, whose mother was named Zeruah, a widowed woman. He lifted up his hand against the king.
Kisha Yeroboamu mwana wa Nebati, mwefraimu wa Sereda, akida wa Sulemani, ambaye jina la mama yake lilikuwa Serua, mjane, pia akainua mkono wake dhidi ya mfalme.
27 And this is the reason for his rebellion against him: that Solomon built up Millo, and that he filled in a deep hole in the city of David, his father.
Kisa cha kuinua mkono wake kinyume cha mfalme ilikuwa ni mfalme Sulemani kujenga Milo na kufunga mahali palipobomoka katika mji wa Daudi baba yake.
28 Now Jeroboam was a valiant and powerful man. And perceiving the young man to be ingenious and industrious, Solomon appointed him as first ruler over the tributes of the entire house of Joseph.
Yeroboamu alikuwa mtu hodari na shujaa. Sulemani akaona kuwa huyo kijana alikuwa na bidii, kwa hiyo akampa kuwa na mamlaka juu ya wafanyakazi katika nyumba ya Yusufu.
29 And it happened, in that time, that Jeroboam departed from Jerusalem. And the prophet Ahijah, the Shilonite, wearing a new cloak, found him on the way. And the two were alone in the field.
Wakati huo, Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii Ahiya Mshilo akamkuta barabarani. Sasa Ahiya alikuwa amevaa vazi jipya na kwamba hawa wawili walikuwa pekee yao kondeni.
30 And taking his new cloak, with which he was covered, Ahijah tore it into twelve parts.
Kisha Ahiya akalishika lile vazi jipya ambalo alikuwa nalo na akalichana katika vipande kumi na viwili.
31 And he said to Jeroboam: “Take ten pieces for yourself. For thus says the Lord, the God of Israel: ‘Behold, I will tear the kingdom from the hand of Solomon, and I will give to you ten tribes.
Akamwambia Yeroboamu. “Chukua vipande kumi, kwani BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Tazama, Nitaugawa ufalme toka katika mkono wa Sulemani nami nitakupa makabila kumi.
32 Yet one tribe shall remain with him, for the sake of my servant, David, as well as Jerusalem, the city which I have chosen out of all the tribes of Israel.
(lakini Sulemani atabaki na kabila moja, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na kwa ajili ya mji wangu Yerusalemu - mji ambao nimeuchagua toka kwenye kabila zote za Israeli),
33 For he has abandoned me, and he has adored Ashtoreth, the goddess of the Sidonians, and Chemosh, the god of Moab, and Milcom, the god of the sons of Ammon. And he has not walked in my ways, so that he would do justice before me, and so that he would carry out my precepts and judgments, as his father David did.
kwa kuwa ameniacha na kumwabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi Mungu wa Wamoabu, na Milikomu mungu wa watu wa Amoni. Wameziacha njia zangu, hawakufanya kilicho chema katika macho yangu, wala hawa kuzishika amri na maagizo yangu, kama alivyofanya Daudi baba yake.
34 But I will not take the entire kingdom from his hand. Instead, I will establish him as the ruler during all the days of his life, for the sake of my servant David, whom I chose, who kept my commandments and my precepts.
Hata hivyo. Stauchukua ufalme wote toka kwenye mkono wa Sulemani. Badala yake, nimemfanya kuwa mtawala katika siku zake zote za uhai wake, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu ambaye nilimchagua, mtu ambaye alizishika amri na maagizo yangu.
35 But I will take away the kingdom from the hand of his son, and I will give to you ten tribes.
Bali nitauchukua ufalme ukiwa chini ya mkono wa mwanae na nitakupa wewe, makabila kumi.
36 Then, to his son, I will give one tribe, so that there may remain a lamp for my servant David before me, for all days, in Jerusalem, the city which I have chosen, so that my name would be there.
Nitampa kabila moja mwana wa Sulemani ili kwamba Daudi mtumishi wagu atabaki kuwa nuru mbele yangu huko Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua ili niweke jina langu.
37 And I will take you up, and you shall reign over all that your soul desires. And you shall be king over Israel.
Nami nitakuchukua, nawe utatawala ili kutimiza haja yako, nawe utakuwa mfalme juu ya Israeli.
38 Therefore, if you will listen to all that I will command you, and if you will walk in my ways, and do what is right in my sight, keeping my commandments and my precepts, just as my servant David did, then I will be with you, and I will build for you a faithful house, in the way that I built a house for David, and I will deliver Israel to you.
Kama utasikiliza yote ninayokuagaza, na kama utatembea katika njia zangu na kufanya kinachopendeza mbele ya macho yangu, ukayashika maagizo na amri zangu, kama Daudi mtumishi wangu alivyofanya, ndipo nitakapokuwa na wewe na nitakujengea nyumba ya uhakika, kama niliyomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 And I will afflict the offspring of David over this, but truly not for all days.’”
Nitawaadhibu uzao wa Daudi, lakini si milele.”
40 Therefore, Solomon wanted to kill Jeroboam. But he rose up and fled away to Egypt, to Shishak, the king of Egypt. And he was in Egypt until the death of Solomon.
Kwa hiyo Sulemani akajaribu kumwua Yeroboamu. Lakini Yeroboamu akaamka na kukimbilia Misri, Kwa Shishaki mfalme wa Misri, naye akabaki Misri mpaka Sulemani alipokufa.
41 Now the rest of the words of Solomon, and all that he did, and his wisdom: behold, these are all written in the book of the words of the days of Solomon.
Na kwa mambo mengine yanayomhusu Sulemani, Yote ambayo alifanya na hekima zake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya
42 And the days that Solomon reigned in Jerusalem, over all of Israel, were forty years.
Sulemani? Sulemani alitawala Yerusalemu juu ya Israeli yote kwa miaka arobaini.
43 And Solomon slept with his fathers, and he was buried in the city of David, his father. And Rehoboam, his son, reigned in his place.
Naye akalala na mababu zake na alizikwa katika mji wa Daudi baba yake. Rehoboamu mwanae akawa mfalme mahali pake.

< 1 Kings 11 >