< Osee 13 >

1 According to the word of Ephraim he adopted ordinances for himself in Israel; and he established them for Baal, and died.
Efraimu alipozungumza, kulikuwa na tetemeko. Alijikuza katika Israeli, lakini akawa na hatia kwa sababu ya ibada ya Baali, naye akafa.
2 And now they have sinned increasingly, and have made for themselves a molten image of their silver, according to the fashion of idols, the work of artificers accomplished for them: they say, Sacrifice men, for the calves have come to an end.
Sasa wanafanya dhambi zaidi na zaidi. Wanatengeneza sanamu za chuma kutoka kwenye fedha zao, sanamu kwa kadiri ya ufanisi wao, zote ni kazi ya mafundi. Watu wanasema juu yao, 'Watu hawa watoao dhabihu na kumbusu ndama.'
3 Therefore shall they be as a morning cloud, and as the early dew that passes away, as chaff blown away from the threshing floor, and as a vapour from tears.
Kwa hiyo watakuwa kama mawingu ya asubuhi, kama umande unaoondoka mapema, kama makapi yanayotokana na upepo kutoka kwenye sakafu, na kama moshi utokao kwenye bomba.
4 But I am the Lord your God that establishes the heaven, and creates the earth, whose hands have framed the whole host of heaven: but I showed them not to you that you should go after them: and I brought you up out of the land of Egypt, and you shall know no God but me; and there is no Saviour beside me.
Lakini mimi ndimi Bwana, Mungu weko, tangu nchi ya Misri. Hutamjua Mungu mwingine bali mimi; wala zaidi yangu, hakuna mkombozi mwingine.
5 I tended you as a shepherd in the wilderness, in an uninhabited land.
Nilikujua jangwani, katika nchi yenye kame.
6 According to their pastures, so they were completely filled; and their hearts were exalted; therefore they forgot me.
Wakati ulipokuwa na malisho, ulishiba; na wakati uliposhiba, moyo wako ukainuliwa. Kwa sababu hiyo umenisahau.
7 And I will be to them as a panther, and as a leopard.
Nitakuwa kama simba; kama chui nitaangalia kando ya njia.
8 I will meet them by the way of the Assyrians, as a she-bear excited, and I will rend the caul of their heart, and the lions' whelps of the thicket shall devour them there; the wild beasts of the field shall rend them in pieces.
Nitawaangamiza kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake. Nami nitararua vifua vyao, na huko nitawaangamiza kama simba, kama vile mnyama wa mwitu atakayerarua vipande vipande.
9 O Israel, who will aid [you] in your destruction?
Nitawaangamiza, Israeli; nani atakayekusaidia?
10 Where is this your king? let him even save you in all your cities: let him judge you, of whom you said, Give me a king and a prince.
Mfalme wako yuko wapi, ili akuokoe katika miji yako yote? Wako wapi wakuu, ambao kwao umeniambia hivi, 'Nipe mfalme na wakuu'?
11 And I gave you a king in mine anger, and kept [him] back in my wrath.
Nimekupa mfalme kwa hasira yangu, nikamchukua kwa ghadhabu yangu.
12 Ephraim [has framed] a conspiracy of unrighteousness, his sin is hidden.
Uovu wa Efraimu umehifadhiwa; hatia yake imehifadhiwa.
13 Pains as of a woman in travail shall come upon him: he is your wise son, because he shall not stay in the destruction of [your] children.
Atakuwa na uchungu wa kujifungua, lakini ni mwana mjinga, kwa maana wakati wa kuzaliwa, hatatoka tumboni.
14 I will deliver [them] out of the power of Hades, and will redeem them from death: where is your penalty, O death? O Hades, where is your sting? comfort is hidden from mine eyes. (Sheol h7585)
Je, nitawaokoa na mkono wa kaburi? Je, nitawaokoa na kifo? Ewe Mauti yako wapi mapigo yako? Ewe kaburi kuko wapi kuharibu kwako? Huruma itafichwa na macho yangu. (Sheol h7585)
15 Forasmuch as he will cause a division amongst [his] brethren, the Lord shall bring upon him an east wind from the desert, and shall dry up his veins [and] quite drain his fountains: he shall dry up his land, and [spoil] all his precious vessels.
Ingawa Efraimu anafanikiwa kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja; upepo wa Bwana utapiga kutoka jangwani. Kijito cha maji cha Efraimu kitauka, na kisima chake hakitakuwa na maji. Adui yake atapora ghala lake la kila kitu cha thamani.
16 Samaria shall be utterly destroyed: for she has resisted her God; they shall fall by the sword, and their sucklings shall be dashed against the ground, and their women with child ripped up.
Samaria itakuwa na hatia, kwa sababu amemuasi dhidi ya Mungu wake. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watavunjwa, na wanawake wao wajawazito watatambuliwa wazi.

< Osee 13 >