< Psalms 17 >

1 A Prayer. Of David. Let my cause come to your ears, O Lord, give attention to my cry; give ear to my prayer which goes not out from false lips.
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 Be my judge; for your eyes see what is right.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 You have put my heart to the test, searching me in the night; you have put me to the test and seen no evil purpose in me; I will keep my mouth from sin.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 As for the works of men, by the word of your lips I have kept myself from the ways of the violent.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 I have kept my feet in your ways, my steps have not been turned away.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 My cry has gone up to you, for you will give me an answer, O God: let your ear be turned to me, and give attention to my words.
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Make clear the wonder of your mercy, O saviour of those who put their faith in your right hand, from those who come out against them.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Keep me as the light of your eyes, covering me with the shade of your wings,
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 From the evil-doers who are violent to me, and from those who are round me, desiring my death.
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 They are shut up in their fat: with their mouths they say words of pride.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 They have made a circle round our steps: their eyes are fixed on us, forcing us down to the earth;
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 Like a lion desiring its food, and like a young lion waiting in secret places.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Up! Lord, come out against him, make him low, with your sword be my saviour from the evil-doer.
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 With your hand, O Lord, from men, even men of the world, whose heritage is in this life, and whom you make full with your secret wealth: they are full of children; after their death their offspring take the rest of their goods.
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 As for me, I will see your face in righteousness: when I am awake it will be joy enough for me to see your form.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< Psalms 17 >