< Psalms 142 >

1 Maschil. Of David. A prayer when he was in the hole of the rock. The sound of my cry went up to the Lord; with my voice I made my prayer for grace to the Lord.
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
2 I put all my sorrows before him; and made clear to him all my trouble.
Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
3 When my spirit is overcome, your eyes are on my goings; nets have been secretly placed in the way in which I go.
Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
4 Looking to my right side, I saw no man who was my friend: I had no safe place; no one had any care for my soul.
Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
5 I have made my cry to you, O Lord; I have said, You are my safe place, and my heritage in the land of the living.
Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 Give ear to my cry, for I am made very low: take me out of the hands of my haters, for they are stronger than I.
Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 Take my soul out of prison, so that I may give praise to your name: the upright will give praise because of me; for you have given me a full reward.
Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.

< Psalms 142 >