< Luke 19 >

1 And he went into Jericho, and when he was going through it,
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 A man, named Zacchaeus, who was the chief tax-farmer, and a man of wealth,
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 Made an attempt to get a view of Jesus, and was not able to do so, because of the people, for he was a small man.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 And he went quickly in front of them and got up into a tree to see him, for he was going that way.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 And when Jesus came to the place, looking up, he said to him, Zacchaeus, be quick and come down, for I am coming to your house today.
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 And he came down quickly, and took him into his house with joy.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 And when they saw it, they were all angry, saying, He has gone into the house of a sinner.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 And Zacchaeus, waiting before him, said to the Lord, See, Lord, half of my goods I give to the poor, and if I have taken anything from anyone wrongly, I give him back four times as much.
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 And Jesus said to him, Today salvation has come to this house, for even he is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 For the Son of man came to make search for those who are wandering from the way, and to be their Saviour.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 And while they were giving ear to these words, he made another story for them, because he was near Jerusalem, and because they were of the opinion that the kingdom of God was coming straight away.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 So he said, A certain man of high birth went into a far-away country to get a kingdom for himself, and to come back.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 And he sent for ten of his servants and gave them ten pounds and said to them, Do business with this till I come.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But his people had no love for him, and sent representatives after him, saying, We will not have this man for our ruler.
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 And when he came back again, having got his kingdom, he gave orders for those servants to whom he had given the money to come to him, so that he might have an account of what business they had done.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 And the first came before him, saying, Lord, your pound has made ten pounds.
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 And he said to him, You have done well, O good servant: because you have done well in a small thing you will have authority over ten towns.
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 And another came, saying, Your pound has made five pounds.
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 And he said, You will be ruler over five towns.
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 And another came, saying, Lord, here is your pound, which I put away in a cloth;
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 Because I was in fear of you, for you are a hard man: you take up what you have not put down, and get in grain where you have not put seed.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 He said to him, By the words of your mouth you will be judged, you bad servant. You had knowledge that I am a hard man, taking up what I have not put down and getting in grain where I have not put seed;
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Why then did you not put my money in a bank, so that when I came I would get it back with interest?
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 And he said to the others who were near, Take the pound away from him, and give it to the man who has ten.
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 And they say to him, Lord, he has ten pounds.
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 And I say to you that to everyone who has, more will be given, but from him who has not, even what he has will be taken away.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 And as for those who were against me, who would not have me for their ruler, let them come here, and be put to death before me.
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 And when he had said this, he went on in front of them, going up to Jerusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 And it came about that when he got near Beth-phage and Bethany by the mountain which is named the Mountain of Olives, he sent two of the disciples,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 Saying, Go into the little town in front of you, and on going in you will see a young ass fixed with a cord, on which no man has ever been seated; let him loose and take him.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 And if anyone says to you, Why are you taking him? say, The Lord has need of him.
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 And those whom he sent went away, and it was as he said.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 And when they were getting the young ass, the owners of it said to them, Why are you taking the young ass?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 And they said, The Lord has need of him.
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 And they took him to Jesus, and they put their clothing on the ass, and Jesus got on to him.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 And while he went on his way they put their clothing down on the road in front of him.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when he came near the foot of the Mountain of Olives, all the disciples with loud voices gave praise to God with joy, because of all the great works which they had seen;
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 Saying, A blessing on the King who comes in the name of the Lord; peace in heaven and glory in the highest.
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 And some of the Pharisees among the people said to him, Master, make your disciples be quiet.
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 And he said in answer, I say to you, if these men keep quiet, the very stones will be crying out.
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 And when he got near and saw the town, he was overcome with weeping for it,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 Saying, If you, even you, had knowledge today, of the things which give peace! but you are not able to see them.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the time will come when your attackers will put a wall round you, and come all round you and keep you in on every side,
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 And will make you level with the earth, and your children with you; and there will not be one stone resting on another in you, because you did not see that it was your day of mercy.
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 And he went into the Temple and put out those who were trading there,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 Saying to them, It has been said, My house is to be a house of prayer, but you have made it a hole of thieves.
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 And every day he was teaching in the Temple. But the chief priests and the scribes and the rulers of the people were attempting to put him to death;
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 But they were not able to do anything, because the people all kept near him, being greatly interested in his words.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >