< Job 40 >

1
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Will he who is protesting give teaching to the Ruler of all? Let him who has arguments to put forward against God give an answer.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 And Job said in answer to the Lord,
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Truly, I am of no value; what answer may I give to you? I will put my hand on my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 I have said once, and even twice, what was in my mind, but I will not do so again.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Then the Lord made answer to Job out of the storm-wind, and said,
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Get your strength together like a man of war: I will put questions to you, and you will give me the answers.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Will you even make my right of no value? will you say that I am wrong in order to make clear that you are right?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Have you an arm like God? have you a voice of thunder like his?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Put on the ornaments of your pride; be clothed with glory and power:
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Let your wrath be overflowing; let your eyes see all the sons of pride, and make them low.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Send destruction on all who are lifted up, pulling down the sinners from their places.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Let them be covered together in the dust; let their faces be dark in the secret place of the underworld.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then I will give praise to you, saying that your right hand is able to give you salvation.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 See now the Great Beast, whom I made, even as I made you; he takes grass for food, like the ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 His strength is in his body, and his force in the muscles of his stomach.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 His tail is curving like a cedar; the muscles of his legs are joined together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are pipes of brass, his legs are like rods of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the chief of the ways of God, made by him for his pleasure.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 He takes the produce of the mountains, where all the beasts of the field are at play.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He takes his rest under the trees of the river, and in the pool, under the shade of the water-plants.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 He is covered by the branches of the trees; the grasses of the stream are round him.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Truly, if the river is overflowing, it gives him no cause for fear; he has no sense of danger, even if Jordan is rushing against his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Will anyone take him when he is on the watch, or put metal teeth through his nose?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >