< Genesis 8 >

1 And God kept Noah in mind, and all the living things and the cattle which were with him in the ark: and God sent a wind over the earth, and the waters went down.
Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
2 And the fountains of the deep and the windows of heaven were shut, and the rain from heaven was stopped.
Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
3 And the waters went slowly back from the earth, and at the end of a hundred and fifty days the waters were lower.
Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
4 And on the seventeenth day of the seventh month the ark came to rest on the mountains of Ararat.
katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
5 And still the waters went on falling, till on the first day of the tenth month the tops of the mountains were seen.
Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
6 Then, after forty days, through the open window of the ark which he had made,
Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina
7 Noah sent out a raven, which went this way and that till the waters were gone from the earth.
na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi.
8 And he sent out a dove, to see if the waters had gone from the face of the earth;
Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi.
9 But the dove saw no resting-place for her foot, and came back to the ark, for the waters were still over all the earth; and he put out his hand, and took her into the ark.
Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina.
10 And after waiting another seven days, he sent the dove out again;
Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina.
11 And the dove came back at evening, and in her mouth was an olive-leaf broken off: so Noah was certain that the waters had gone down on the earth.
Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia.
12 And after seven days more, he sent the dove out again, but she did not come back to him.
Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.
13 And in the six hundred and first year, on the first day of the first month, the waters were dry on the earth: and Noah took the cover off the ark and saw that the face of the earth was dry.
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka.
14 And on the twenty-seventh day of the second month the earth was dry.
Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.
15 And God said to Noah,
Ndipo Mungu akamwambia Noa,
16 Go out of the ark, you and your wife and your sons and your sons' wives.
“Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao.
17 Take out with you every living thing which is with you, birds and cattle and everything which goes on the earth, so that they may have offspring and be fertile and be increased on the earth.
Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”
18 And Noah went out with his sons and his wife and his sons' wives;
Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao.
19 And every beast and bird and every living thing of every sort which goes on the earth, went out of the ark.
Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.
20 And Noah made an altar to the Lord, and from every clean beast and bird he made burned offerings on the altar.
Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 And when the sweet smell came up to the Lord, he said in his heart, I will not again put a curse on the earth because of man, for the thoughts of man's heart are evil from his earliest days; never again will I send destruction on all living things as I have done.
Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.
22 While the earth goes on, seed time and the getting in of the grain, cold and heat, summer and winter, day and night, will not come to an end.
“Kwa muda dunia idumupo, wakati wa kupanda na wa kuvuna, wakati wa baridi na wa joto, wakati wa kiangazi na wa masika, usiku na mchana kamwe havitakoma.”

< Genesis 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark