< Genesis 5 >

1 This is the book of the generations of Adam. In the day when God made man, he made him in the image of God;
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 Male and female he made them, naming them Man, and giving them his blessing on the day when they were made.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 Adam had been living for a hundred and thirty years when he had a son like himself, after his image, and gave him the name of Seth:
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 And after the birth of Seth, Adam went on living for eight hundred years, and had sons and daughters:
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 And all the years of Adam's life were nine hundred and thirty: and he came to his end.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 And Seth was a hundred and five years old when he became the father of Enosh:
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 And he went on living after the birth of Enosh for eight hundred and seven years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 And all the years of Seth's life were nine hundred and twelve: and he came to his end.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 And Enosh was ninety years old when he became the father of Kenan:
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 And after the birth of Kenan, Enosh went on living for eight hundred and fifteen years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 And all the years of Enosh were nine hundred and five: and he came to his end.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 And Kenan was seventy years old when he became the father of Mahalalel:
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 And after the birth of Mahalalel, Kenan went on living for eight hundred and forty years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 And all the years of Kenan's life were nine hundred and ten; and he came to his end.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 And Mahalalel was sixty-five years old when he became the father of Jared:
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 And after the birth of Jared, Mahalalel went on living for eight hundred and thirty years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 And all the years of Mahalalel's life were eight hundred and ninety-five: and he came to his end.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 And Jared was a hundred and sixty-two years old when he became the father of Enoch:
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 And Jared went on living after the birth of Enoch for eight hundred years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 And all the years of Jared's life were nine hundred and sixty-two: and he came to his end.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 And Enoch was sixty-five years old when he became the father of Methuselah:
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 And after the birth of Methuselah, Enoch went on in God's ways for three hundred years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 And all the years of Enoch's life were three hundred and sixty-five:
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 And Enoch went on in God's ways: and he was not seen again, for God took him.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 And Methuselah was a hundred and eighty-seven years old when he became the father of Lamech:
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 And after the birth of Lamech, Methuselah went on living for seven hundred and eighty-two years, and had sons and daughters:
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 And all the years of Methuselah's life were nine hundred and sixty-nine: and he came to his end.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 And Lamech was a hundred and eighty-two years old when he had a son:
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 And he gave him the name of Noah, saying, Truly, he will give us rest from our trouble and the hard work of our hands, because of the earth which was cursed by God.
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 And after the birth of Noah, Lamech went on living for five hundred and ninety-five years, and had sons and daughters:
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 And all the years of Lamech's life were seven hundred and seventy-seven: and he came to his end.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 And when Noah was five hundred years old, he became the father of Shem, Ham, and Japheth.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

< Genesis 5 >