< Matthew 15 >

1 Then there come to Jesus from Jerusalem Pharisees and scribes, saying,
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
2 Why do thy disciples transgress the tradition of the elders? for they wash not their hands when they eat bread.
“Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
3 And he answered and said unto them, Why do ye also transgress the commandment of God because of your tradition?
Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 For God said, Honor thy father and thy mother: and, He that speaketh evil of father or mother, let him die the death.
Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
5 But ye say, Whosoever shall say to his father or his mother, That wherewith thou mightest have been profited by me is given [to God];
Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
6 he shall not honor his father. And ye have made void the word of God because of your tradition.
basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
7 Ye hypocrites, well did Isaiah prophesy of you, saying,
Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
8 This people honoreth me with their lips; But their heart is far from me.
“‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 But in vain do they worship me, Teaching [as their] doctrines the precepts of men.
Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
10 And he called to him the multitude, and said unto them, Hear, and understand:
Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
11 Not that which entereth into the mouth defileth the man; but that which proceedeth out of the mouth, this defileth the man.
kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
12 Then came the disciples, and said unto him, Knowest thou that the Pharisees were offended, when they heard this saying?
Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
13 But he answered and said, Every plant which my heavenly Father planted not, shall be rooted up.
Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
14 Let them alone: they are blind guides. And if the blind guide the blind, both shall fall into a pit.
Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
15 And Peter answered and said unto him, Declare unto us the parable.
Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
16 And he said, Are ye also even yet without understanding?
Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
17 Perceive ye not, that whatsoever goeth into the mouth passeth into the belly, and is cast out into the draught?
Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
18 But the things which proceed out of the mouth come forth out of the heart; and they defile the man.
Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
19 For out of the heart come forth evil thoughts, murders, adulteries, fornications, thefts, false witness, railings:
Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
20 these are the things which defile the man; but to eat with unwashen hands defileth not the man.
Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
21 And Jesus went out thence, and withdrew into the parts of Tyre and Sidon.
Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
22 And behold, a Canaanitish woman came out from those borders, and cried, saying, Have mercy on me, O Lord, thou son of David; my daughter is grievously vexed with a demon.
Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
23 But he answered her not a word. And his disciples came and besought him, saying, Send her away; for she crieth after us.
Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
24 But he answered and said, I was not sent but unto the lost sheep of the house of Israel.
Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
25 But she came and worshipped him, saying, Lord, help me.
Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
26 And he answered and said, It is not meet to take the children’s bread and cast it to the dogs.
Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
27 But she said, Yea, Lord: for even the dogs eat of the crumbs which fall from their masters’ table.
Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
28 Then Jesus answered and said unto her, O woman, great is thy faith: be it done unto thee even as thou wilt. And her daughter was healed from that hour.
Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
29 And Jesus departed thence, and came nigh unto the sea of Galilee; and he went up into the mountain, and sat there.
Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
30 And there came unto him great multitudes, having with them the lame, blind, dumb, maimed, and many others, and they cast them down at his feet; and he healed them:
Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
31 insomuch that the multitude wondered, when they saw the dumb speaking, the maimed whole, and the lame walking, and the blind seeing: and they glorified the God of Israel.
Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
32 And Jesus called unto him his disciples, and said, I have compassion on the multitude, because they continue with me now three days and have nothing to eat: and I would not send them away fasting, lest haply they faint on the way.
Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
33 And the disciples say unto him, Whence should we have so many loaves in a desert place as to fill so great a multitude?
Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
34 And Jesus said unto them, How many loaves have ye? And they said, Seven, and a few small fishes.
Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
35 And he commanded the multitude to sit down on the ground;
Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
36 and he took the seven loaves and the fishes; and he gave thanks and brake, and gave to the disciples, and the disciples to the multitudes.
Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
37 And they all ate, and were filled: and they took up that which remained over of the broken pieces, seven baskets full.
Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
38 And they that did eat were four thousand men, besides women and children.
Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
39 And he sent away the multitudes, and entered into the boat, and came into the borders of Magadan.
Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.

< Matthew 15 >