< 2 Samuel 23 >

1 Now these are the last words of David. David the son of Jesse saith, And the man who was raised on high saith, The anointed of the God of Jacob, And the sweet psalmist of Israel:
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2 The Spirit of Jehovah spake by me, And his word was upon my tongue.
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 The God of Israel said, The Rock of Israel spake to me: One that ruleth over men righteously, That ruleth in the fear of God,
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4 [He shall be] as the light of the morning, when the sun riseth, A morning without clouds, [When] the tender grass [springeth] out of the earth, Through clear shining after rain.
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
5 Verily my house is not so with God; Yet he hath made with me an everlasting covenant, Ordered in all things, and sure: For it is all my salvation, and all [my] desire, Although he maketh it not to grow.
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
6 But the ungodly shall be all of them as thorns to be thrust away, Because they cannot be taken with the hand;
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
7 But the man that toucheth them Must be armed with iron and the staff of a spear: And they shall be utterly burned with fire in [their] place.
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
8 These are the names of the mighty men whom David had: Josheb-basshebeth a Tahchemonite, chief of the captains; the same was Adino the Eznite, against eight hundred slain at one time.
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
9 And after him was Eleazar the son of Dodai the son of an Ahohite, one of the three mighty men with David, when they defied the Philistines that were there gathered together to battle, and the men of Israel were gone away.
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10 He arose, and smote the Philistines until his hand was weary, and his hand clave unto the sword; and Jehovah wrought a great victory that day; and the people returned after him only to take spoil.
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
11 And after him was Shammah the son of Agee a Hararite. And the Philistines were gathered together into a troop, where was a plot of ground full of lentils; and the people fled from the Philistines.
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
12 But he stood in the midst of the plot, and defended it, and slew the Philistines; and Jehovah wrought a great victory.
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
13 And three of the thirty chief men went down, and came to David in the harvest time unto the cave of Adullam; and the troop of the Philistines was encamped in the valley of Rephaim.
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
14 And David was then in the stronghold; and the garrison of the Philistines was then in Beth-lehem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
15 And David longed, and said, Oh that one would give me water to drink of the well of Beth-lehem, which is by the gate!
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
16 And the three mighty men brake through the host of the Philistines, and drew water out of the well of Beth-lehem, that was by the gate, and took it, and brought it to David: but he would not drink thereof, but poured it out unto Jehovah.
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
17 And he said, Be it far from me, O Jehovah, that I should do this: [shall I drink] the blood of the men that went in jeopardy of their lives? therefore he would not drink it. These things did the three mighty men.
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
18 And Abishai, the brother of Joab, the son of Zeruiah, was chief of the three. And he lifted up his spear against three hundred and slew them, and had a name among the three.
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
19 Was he not most honorable of the three? therefore he was made their captain: howbeit he attained not unto the [first] three.
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
20 And Benaiah the son of Jehoiada, the son of a valiant man of Kabzeel, who had done mighty deeds, he slew the two [sons of] Ariel of Moab: he went down also and slew a lion in the midst of a pit in time of snow.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
21 And he slew an Egyptian, a goodly man: and the Egyptian had a spear in his hand; but he went down to him with a staff, and plucked the spear out of the Egyptian’s hand, and slew him with his own spear.
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
22 These things did Benaiah the son of Jehoiada, and had a name among the three mighty men.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
23 He was more honorable than the thirty, but he attained not to the [first] three. And David set him over his guard.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
24 Asahel the brother of Joab was one of the thirty; Elhanan the son of Dodo of Beth-lehem,
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
25 Shammah the Harodite, Elika the Harodite,
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
26 Helez the Paltite, Ira the son of Ikkesh the Tekoite,
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
27 Abiezer the Anathothite, Mebunnai the Hushathite,
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
28 Zalmon the Ahohite, Maharai the Netophathite,
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
29 Heleb the son of Baanah the Netophathite, Ittai the son of Ribai of Gibeah of the children of Benjamin,
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
30 Benaiah a Pirathonite, Hiddai of the brooks of Gaash.
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
31 Abi-albon the Arbathite, Azmaveth the Barhumite,
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
32 Eliahba the Shaalbonite, the sons of Jashen, Jonathan,
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
33 Shammah the Hararite, Ahiam the son of Sharar the Ararite,
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
34 Eliphelet the son of Ahasbai, the son of the Maacathite, Eliam the son of Ahithophel the Gilonite,
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
35 Hezro the Carmelite, Paarai the Arbite,
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
36 Igal the son of Nathan of Zobah, Bani the Gadite,
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
37 Zelek the Ammonite, Naharai the Beerothite, armorbearers to Joab the son of Zeruiah,
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
38 Ira the Ithrite, Gareb the Ithrite,
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
39 Uriah the Hittite: thirty and seven in all.
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.

< 2 Samuel 23 >