< 1 Corinthians 15 >

1 Now I make known unto you brethren, the gospel which I preached unto you, which also ye received, wherein also ye stand,
Sasa ninawakumbusha, akina kaka na akina dada, juu ya injili niliyowahubiria, ambayo mliipokea na kusimama kwayo.
2 by which also ye are saved, if ye hold fast the word which I preached unto you, except ye believed in vain.
Ni katika injili hii mmeokolewa, kama mkilishika imara neno nililowahubiri ninyi, isipokuwa mliamini bure.
3 For I delivered unto you first of all that which also I received: that Christ died for our sins according to the scriptures;
Kama kwanza nilivyo ipokea kwa umuhimu niliileta kwenu kama ilivyo: kwamba kutokana na maandiko, Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu,
4 and that he was buried; and that he hath been raised on the third day according to the scriptures;
kutokana na maandiko alizikwa, na kwamba alifufuka siku ya tatu.
5 and that he appeared to Cephas; then to the twelve;
Na kwamba alimtokea Kefa, kisha kwa wale kumi na wawili.
6 then he appeared to above five hundred brethren at once, of whom the greater part remain until now, but some are fallen asleep;
Kisha aliwatokea kwa wakati mmoja akina kaka na akina dada zaidi ya mia tano. Wengi wao bado wako hai, lakini baadhi yao wamelala usingizi.
7 then he appeared to James; then to all the apostles;
Kisha alimtokea Yakobo, kisha mitume wote.
8 and last of all, as to the [child] untimely born, he appeared to me also.
Mwisho wa yote, alinitokea mimi, kama vile kwa mtoto aliye zaliwa katika wakati usio sahihi.
9 For I am the least of the apostles, that am not meet to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
Kwa kuwa mimi ni mdogo kati ya mitume. Sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
10 But by the grace of God I am what I am: and his grace which was bestowed upon me was not found vain; but I labored more abundantly than they all: yet not I, but the grace of God which was with me.
Lakini kwa neema ya Mungu nipo kama nilivyo, na neema yake kwangu haikuwa bure. Badala yake, nilifanya bidii kuliko wote. Lakini haikuwa mimi, bali neema ya Mungu iliyo ndani yangu.
11 Whether then [it be] I or they, so we preach, and so ye believed.
Kwa hiyo kama ni mimi au wao, tuna hubiri hivyo na tunaamini hivyo.
12 Now if Christ is preached that he hath been raised from the dead, how say some among you that there is no resurrection of the dead?
Sasa kama Kristo alihubiriwa kama aliyefufuka kwa wafu, iweje baadhi yenu mseme hakuna ufufuo wa wafu?
13 But if there is no resurrection of the dead, neither hath Christ been raised:
Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo pia hakufufuka.
14 and if Christ hath not been raised, then is our preaching vain, your faith also is vain.
Na kama Kristo hakufufuka, hivyo mahubiri yetu ni bure, na imani yenu ni bure.
15 Yea, and we are found false witnesses of God; because we witnessed of God that he raised up Christ: whom he raised not up, if so be that the dead are not raised.
Na tumepatikana kuwa mashahidi wa uongo kumuhusu Mungu, kwa sababu tulimshushuhudia Mungu kinyume, kusema alimfufua Kristo, wakati hakumfufua.
16 For if the dead are not raised, neither hath Christ been raised:
Kama ikiwa wafu hawafufuliwi, Yesu pia hakufufuliwa.
17 and if Christ hath not been raised, your faith is vain; ye are yet in your sins.
Na kama Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure na bado mko kwenye dhambi zenu.
18 Then they also that are fallen asleep in Christ have perished.
Hivyo hata wale waliokufa katika Kristo pia wameangamia.
19 If we have only hoped in Christ in this life, we are of all men most pitiable.
Ikiwa kwa maisha haya peke yake tunaujasiri kwa wakati ujao ndani ya Kristo, watu wote, sisi niwakuhurumiwa zaidi ya watu wote.
20 But now hath Christ been raised from the dead, the firstfruits of them that are asleep.
Lakini sasa Kristo amefufuka kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale waliokufa.
21 For since by man [came] death, by man [came] also the resurrection of the dead.
Kwa kuwa kifo kilikuja kupitia mwanadamu, pia kupitia mwanadamu ufufuo wa wafu.
22 For as in Adam all die, so also in Christ shall all be made alive.
Kwa kuwa kama katika Adam wote wanakufa, hivyo pia katika Kristo wote watafanywa hai.
23 But each in his own order: Christ the firstfruits; then they that are Christ’s, at his coming.
Lakini kila moja katika mpango wake: Kristo, matunda ya kwanza, na kisha wale walio wa Kristo watafanywa hai wakati wa kuja kwake.
24 Then [cometh] the end, when he shall deliver up the kingdom to God, even the Father; when he shall have abolished all rule and all authority and power.
Ndipo utakuwa mwisho, pale Kristo atakapo kabidhi ufalme kwa Mungu Baba. Hii ni pale atakapo komesha utawala wote na mamlaka yote na nguvu.
25 For he must reign, till he hath put all his enemies under his feet.
Kwa kuwa lazima atawale mpaka atakapoweka maadui zake wote chini ya nyayo zake.
26 The last enemy that shall be abolished is death.
Adui wa mwisho kuharibiwa ni kifo.
27 For, He put all things in subjection under his feet. But when he saith, All things are put in subjection, it is evident that he is excepted who did subject all things unto him.
Kwa kuwa “ameweka kila kitu chini ya nyayo zake.” Lakini inaposema “ameweka kila kitu,” ni wazi kwamba hii haihusishi wale walioweka kila kitu chini yake mwenyewe.
28 And when all things have been subjected unto him, then shall the Son also himself be subjected to him that did subject all things unto him, that God may be all in all.
Wakati vitu vyote vimewekwa chini yake, kisha Mwana mwenyewe atawekwa chini kwake Yeye ambaye aliviweka vitu vyote chini yake. Hii itatokea ili kwamba Mungu Baba awe yote katika vyote.
29 Else what shall they do that are baptized for the dead? If the dead are not raised at all, why then are they baptized for them?
Au pia watafanya nini wale waliobatizwa kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kabisa, kwa nini tena wanabatizwa kwa ajili yao?
30 why do we also stand in jeopardy every hour?
Na kwa nini tuko katika hatari kila saa?
31 I protest by that glorying in you, brethren, which I have in Christ Jesus our Lord, I die daily.
Kaka na dada zangu, kupitia kujisifu kwangu katika ninyi, ambayo ninayo katika Kristo Yesu Bwana wetu, natangaza hivi: nakufa kila siku.
32 If after the manner of men I fought with beasts at Ephesus, what doth it profit me? If the dead are not raised, let us eat and drink, for to-morrow we die.
Inanifaidia nini, katika mtazamo wa wanadamu, kama nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, kama wafu hawafufuliwi? “Acha basi tule na kunywa, kwa kuwa kesho tunakufa.”
33 Be not deceived: Evil companionships corrupt good morals.
Msidanganywe: “Makundi mabaya huharibu tabia njema.
34 Awake to soberness righteously, and sin not; for some have no knowledge of God: I speak [this] to move you to shame.
“Muwe na kiasi! muishi katika haki! msiendelee kutenda dhambi. Kwa kuwa baadhi yenu hamna maarifa ya Mungu. Nasema hivi kwa aibu yenu.
35 But some one will say, How are the dead raised? and with what manner of body do they come?
Lakini mtu mwingine atasema, “Jinsi gani wafu wanafufuliwa? Nao watakuja na aina gani ya mwili?”
36 Thou foolish one, that which thou thyself sowest is not quickened except it die:
Wewe ni mjinga sana! Kile ulichopanda hakiwezi kuanza kukua isipokuwa kimekufa.
37 and that which thou sowest, thou sowest not the body that shall be, but a bare grain, it may chance of wheat, or of some other kind;
Na kile unachopanda sio mwili ambao utakuwa, bali ni mbegu iliyochipua. Inaweza kuwa ngano au kitu kingine.
38 but God giveth it a body even as it pleased him, and to each seed a body of its own.
Lakini Mungu ataipa mwili kama apendavyo, na katika kila mbengu mwili wake mwenyewe.
39 All flesh is not the same flesh: but there is one [flesh] of men, and another flesh of beasts, and another flesh of birds, and another of fishes.
Miili yote haifanani. Isipokuwa, kuna mwili mmoja wa wanadamu, na mwili mwingine wa wanyama, na wili mwingine wa ndege, na mwingine kwa ajili ya samaki.
40 There are also celestial bodies, and bodies terrestrial: but the glory of the celestial is one, and the [glory] of the terrestrial is another.
Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani. Lakini utukufu wa miili ya mbinguni ni aina moja na utukufu wa duniani ni mwingine.
41 There is one glory of the sun, and another glory of the moon, and another glory of the stars; for one star differeth from another star in glory.
Kuna utukufu mmoja wa jua, na utukufu mwingine wa mwezi, na utukufu mwingine wa nyota. Kwa kuwa nyota moja inatofautiana na nyota nyingine katika utukufu.
42 So also is the resurrection of the dead. It is sown in corruption; it is raised in incorruption:
Hivyo ndivyo ulivyo pia ufufuo wa wafu. Kinacho pandwa kinaharibika, na kinacho ota hakiharibiki.
43 it is sown in dishonor; it is raised in glory: it is sown in weakness; it is raised in power:
Kimepandwa katika matumizi ya kawaida, kinaoteshwa katika utukufu. Kimepandwa katika udhaifu, kinaoteshwa katika nguvu.
44 it is sown a natural body; it is raised a spiritual body. If there is a natural body, there is also a spiritual [body].
Kimepandwa katika mwili wa asili, kinaoteshwa katika mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, kuna mwili wa kiroho pia.
45 So also it is written, The first man Adam became a living soul. The last Adam [became] a life-giving spirit.
Hivyo pia imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika roho inayo ishi.” Adamu wa mwisho alifanyika roho itoayo uhai.
46 Howbeit that is not first which is spiritual, but that which is natural; then that which is spiritual.
Lakini wa kiroho hakuja kwanza bali wa asili, na kisha wa kiroho.
47 The first man is of the earth, earthy: the second man is of heaven.
Mtu wa kwanza ni wa dunia, alitengenezwa kwa mavumbi. Mtu wa pili anatoka mbinguni.
48 As is the earthy, such are they also that are earthy: and as is the heavenly, such are they also that are heavenly.
Kama vile yule aliyetengenezwa kwa mavumbi, hivyo pia wale waliotengenezwa kwa mavumbi. Kama vile mtu wa mbinguni alivyo, hivyo pia wale wa mbinguni.
49 And as we have borne the image of the earthy, we shall also bear the image of the heavenly.
Kama ambavyo tumebeba mfano wa mtu wa mavumbi, tutabeba pia mfano wa mtu wa mbinguni.
50 Now this I say, brethren, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God; neither doth corruption inherit incorruption.
Sasa nawaambia, kaka na dada zangu, kwamba mwili na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu. Wala wakuharibika kurithi wakutoharibika.
51 Behold, I tell you a mystery: We all shall not sleep, but we shall all be changed,
Tazama! Nawaambia ninyi siri ya kweli: Hatutakufa wote, bali wote tutabadilishwa.
52 in a moment, in the twinkling of an eye, at the last trump: for the trumpet shall sound, and the dead shall be raised incorruptible, and we shall be changed.
Tutabadilishwa katika wakati, katika kufumba na kufumbua kwa jicho, katika tarumbeta ya mwisho. Kwa kuwa tarumbeta italia, na wafu watafufuliwa na hali ya kutoharibika, na tutabadilishwa.
53 For this corruptible must put on incorruption, and this mortal must put on immortality.
Kwani huu wa kuharibika lazima uvae wa kutoharibika, na huu wa kufa lazima uvae wa kutokufa.
54 But when this corruptible shall have put on incorruption, and this mortal shall have put on immortality, then shall come to pass the saying that is written, Death is swallowed up in victory.
Lakini wakati huu wa kuharibika ukivikwa wa kutokuharibika, na huu wa kufa ukivaa wa kutokufa, ndipo utakuja msemo ambao umeandikwa, “Kifo kimemezwa katika ushindi.”
55 O death, where is thy victory? O death, where is thy sting? (Hadēs g86)
“Kifo, ushindi wako uko wapi? Kifo, uko wapi uchungu wako?” (Hadēs g86)
56 The sting of death is sin; and the power of sin is the law:
Uchungu wa kifo ni dhambi, na nguvu ya dhambi ni sheria.
57 but thanks be to God, who giveth us the victory through our Lord Jesus Christ.
Lakini shukurani kwa Mungu, atupaye sisi ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!
58 Wherefore, my beloved brethren, be ye stedfast, unmoveable, always abounding in the work of the Lord, forasmuch as ye know that your labor is not vain in the Lord.
Kwa hiyo, wapendwa kaka na dada zangu, iweni imara na msitikisike. Daima itendeni kazi ya Bwana, kwa sababu mnajua kuwa kazi yenu katika Bwana siyo bure.

< 1 Corinthians 15 >