< Psalms 83 >

1 A song. A Psalm by Asaph. God, do not keep silent. Do not keep silent, and do not be still, God.
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 For, behold, your enemies are stirred up. Those who hate you have lifted up their heads.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 They conspire with cunning against your people. They plot against your cherished ones.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 “Come,” they say, “let’s destroy them as a nation, that the name of Israel may be remembered no more.”
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 For they have conspired together with one mind. They form an alliance against you.
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 The tents of Edom and the Ishmaelites; Moab, and the Hagrites;
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, Ammon, and Amalek; Philistia with the inhabitants of Tyre;
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Assyria also is joined with them. They have helped the children of Lot. (Selah)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Do to them as you did to Midian, as to Sisera, as to Jabin, at the river Kishon;
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 who perished at Endor, who became as dung for the earth.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Make their nobles like Oreb and Zeeb, yes, all their princes like Zebah and Zalmunna,
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 who said, “Let’s take possession of God’s pasture lands.”
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 My God, make them like tumbleweed, like chaff before the wind.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 As the fire that burns the forest, as the flame that sets the mountains on fire,
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 so pursue them with your tempest, and terrify them with your storm.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Fill their faces with confusion, that they may seek your name, LORD.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Let them be disappointed and dismayed forever. Yes, let them be confounded and perish;
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 that they may know that you alone, whose name is the LORD, are the Most High over all the earth.
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.

< Psalms 83 >