< Psalms 77 >

1 For the Chief Musician. To Jeduthun. A Psalm by Asaph. My cry goes to God! Indeed, I cry to God for help, and for him to listen to me.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 In the day of my trouble I sought the Lord. My hand was stretched out in the night, and did not get tired. My soul refused to be comforted.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 I remember God, and I groan. I complain, and my spirit is overwhelmed. (Selah)
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 You hold my eyelids open. I am so troubled that I cannot speak.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 I have considered the days of old, the years of ancient times.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 I remember my song in the night. I consider in my own heart; my spirit diligently inquires:
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 “Will the Lord reject us forever? Will he be favorable no more?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Has his loving kindness vanished forever? Does his promise fail for generations?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Has God forgotten to be gracious? Has he, in anger, withheld his compassion?” (Selah)
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 Then I thought, “I will appeal to this: the years of the right hand of the Most High.”
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 I will remember the LORD’s deeds; for I will remember your wonders of old.
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 I will also meditate on all your work, and consider your doings.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 Your way, God, is in the sanctuary. What god is great like God?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 You are the God who does wonders. You have made your strength known among the peoples.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 You have redeemed your people with your arm, the sons of Jacob and Joseph. (Selah)
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 The waters saw you, God. The waters saw you, and they writhed. The depths also convulsed.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 The clouds poured out water. The skies resounded with thunder. Your arrows also flashed around.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 The voice of your thunder was in the whirlwind. The lightnings lit up the world. The earth trembled and shook.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 Your way was through the sea, your paths through the great waters. Your footsteps were not known.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 You led your people like a flock, by the hand of Moses and Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

< Psalms 77 >