< Psalms 59 >

1 For the Chief Musician. To the tune of “Do Not Destroy.” A poem by David, when Saul sent, and they watched the house to kill him. Deliver me from my enemies, my God. Set me on high from those who rise up against me.
Uniokoe dhidi ya adui zangu, Mungu wangu; uniweke mahali pa juu mbali na wale wanaoinuka dhidi yangu.
2 Deliver me from the workers of iniquity. Save me from the bloodthirsty men.
Uniweke salama mbali na wafanyao kazi ya uovu, na uniokoe dhidi ya watu wenye kiu ya damu.
3 For, behold, they lie in wait for my soul. The mighty gather themselves together against me, not for my disobedience, nor for my sin, LORD.
Maana, tazama, wanasubiria uvamizini waniue. Wafanya maovu wenye nguvu hujikusanya wenyewe pamoja dhidi yangu, lakini sio kwa sababu ya makosa yangu au dhambi yangu, Yahwe.
4 I have done no wrong, yet they are ready to attack me. Rise up, behold, and help me!
Wao wanajiandaa kunikimbiza ingawa sina kosa; amka unisaidie na unitazame.
5 You, LORD God of Armies, the God of Israel, rouse yourself to punish the nations. Show no mercy to the wicked traitors. (Selah)
Ewe, Yahwe Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, inika uwaadhibu mataifa yote; usiwe na huruma kwa mhalifu mwovu yeyote. (Selah)
6 They return at evening, howling like dogs, and prowl around the city.
Wao wanarudi jioni, wanabweka kama mbwa na kuuzungukia mji.
7 Behold, they spew with their mouth. Swords are in their lips, “For”, they say, “who hears us?”
Tazama, wanapiga kelele mbaya kwa midomo yao; panga ziko kwenye midomo yao, maana wanasema, “Ni nani anaye tusikia?”
8 But you, LORD, laugh at them. You scoff at all the nations.
Lakini wewe, Yahwe, utawacheka; wewe huwadhihaki mataifa yote.
9 Oh, my Strength, I watch for you, for God is my high tower.
Mungu, nguvu yangu, nitakuwa msikivu kwako; wewe ni mnara wangu mrefu.
10 My God will go before me with his loving kindness. God will let me look at my enemies in triumph.
Mungu atakutana nami akiwa na uaminifu wa agano lake; Mungu atanifanya nione shauku yangu juu ya adui zangu.
11 Do not kill them, or my people may forget. Scatter them by your power, and bring them down, Lord our shield.
Usiwaue, hivyo watu watasahau. Uwatawanye kwa nguvu zako na uwaangushe, Bwana ngao yetu.
12 For the sin of their mouth, and the words of their lips, let them be caught in their pride, for the curses and lies which they utter.
Kwa ajili ya dhambi za midomo yao na maneno ya midomo yao, wakamatwe katika majivuno yao, na kwa laana na uongo ambao wao huelezea.
13 Consume them in wrath. Consume them, and they will be no more. Let them know that God rules in Jacob, to the ends of the earth. (Selah)
Uwamalize katika gadhabu yako, uwamalize ili kwamba wasiwepo tena; wajue kuwa Mungu anatawala katika Yakobo na mwisho wa nchi. (Selah)
14 At evening let them return. Let them howl like a dog, and go around the city.
Wakati wa jioni wao hurudi, wakibweka kama mbwa wakiuzungukia mji.
15 They shall wander up and down for food, and wait all night if they are not satisfied.
Wanatangatanga wakitafuta chakula na wanabweka kama mbwa kama hawajatosheka.
16 But I will sing of your strength. Yes, I will sing aloud of your loving kindness in the morning. For you have been my high tower, a refuge in the day of my distress.
Lakini nitaimba kuhusu nguvu zako, na asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako imara! maana umekuwa mnara wangu mrefu na kimbilio la usalama katika siku ya taabu.
17 To you, my strength, I will sing praises. For God is my high tower, the God of my mercy.
Kwako, nguvu yangu, nitaimba sifa; kwa kuwa Mungu ni mnara wangu mrefu, Mungu wa uaminifu wa agano.

< Psalms 59 >