< Psalms 48 >

1 A Song. A Psalm by the sons of Korah. Great is the LORD, and greatly to be praised, in the city of our God, in his holy mountain.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, is Mount Zion, on the north sides, the city of the great King.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 God has shown himself in her citadels as a refuge.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 For, behold, the kings assembled themselves, they passed by together.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 They saw it, then they were amazed. They were dismayed. They hurried away.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Trembling took hold of them there, pain, as of a woman in travail.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 With the east wind, you break the ships of Tarshish.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 As we have heard, so we have seen, in the city of the LORD of Armies, in the city of our God. God will establish it forever. (Selah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 We have thought about your loving kindness, God, in the middle of your temple.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 As is your name, God, so is your praise to the ends of the earth. Your right hand is full of righteousness.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Let Mount Zion be glad! Let the daughters of Judah rejoice because of your judgments.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Walk about Zion, and go around her. Number its towers.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Notice her bulwarks. Consider her palaces, that you may tell it to the next generation.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 For this God is our God forever and ever. He will be our guide even to death.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Psalms 48 >