< Psalms 36 >

1 For the Chief Musician. By David, the servant of the LORD. A revelation is within my heart about the disobedience of the wicked: There is no fear of God before his eyes.
Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
2 For he flatters himself in his own eyes, too much to detect and hate his sin.
Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
3 The words of his mouth are iniquity and deceit. He has ceased to be wise and to do good.
Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 He plots iniquity on his bed. He sets himself in a way that is not good. He does not abhor evil.
Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
5 Your loving kindness, LORD, is in the heavens. Your faithfulness reaches to the skies.
Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
6 Your righteousness is like the mountains of God. Your judgments are like a great deep. LORD, you preserve man and animal.
Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
7 How precious is your loving kindness, God! The children of men take refuge under the shadow of your wings.
Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
8 They shall be abundantly satisfied with the abundance of your house. You will make them drink of the river of your pleasures.
Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
9 For with you is the spring of life. In your light we will see light.
Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
10 Oh continue your loving kindness to those who know you, your righteousness to the upright in heart.
Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
11 Do not let the foot of pride come against me. Do not let the hand of the wicked drive me away.
Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
12 There the workers of iniquity are fallen. They are thrust down, and shall not be able to rise.
Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.

< Psalms 36 >